UKAWA haya lazima yajadiliwe

UKAWA haya lazima yajadiliwe

Mimi nimeshangaa kutumia mabilioni ya pesa kwenye mambo mengine
na kusahau posho na chakula kwa mawakala
nimeshangaa sana

Kwa hiyo mawakala waliamua kulinda lango la adui yao wakati wameenda kushambulia? Ukawa ya Mbowe ni basi ilimradi mfuko wake uneemeke huku akitegemea chama chake kikue kwa siasa za matukio
 
Freeland
Watu tuliamini chama bado kichanga ndio maana wengi tukawa na moyo wa kujitolea.

Lakini kwa sasa na haya mambo ya hovyo hovyo ndio tunajua ulaghai wa Chadema hasa Mbowe.
 
Last edited by a moderator:
Watu tuliamini chama bado kichanga ndio maana wengi tukawa na moyo wa kujitolea.


Lakini kwa sasa na haya mambo ya hovyo hovyo ndio tunajua ulaghai wa Chadema hasa Mbowe.

Usijali mkuu....Ni kupokezana vijiti

Asante kwa kujitolea

Wengine tutaendelea kujitolea
 
Kwa hiyo mawakala waliamua kulinda lango la adui yao wakati wameenda kushambulia? Ukawa ya Mbowe ni basi ilimradi mfuko wake uneemeke huku akitegemea chama chake kikue kwa siasa za matukio

Mbona CCM mnalalamika sana?
 
Mkuu....Constructive criticisms zitapokelewa....Akuna tatizo katika hilo
Lowasa ana haki ya kuwa mwanachama kama ulivyo wewe huko CCM
Ukiamua kukaa pembeni kaa pembeni.....wengine wengi watajiunga.....si lazima uwe wewe
Chama chetu kinaendeshwa kupitia mifumo rasmi....Sio JF
Wewe subiri ndio utatambua kama CHADEMA imepoteza umaarufu
Mbowe ni Mwenyekiti wetu,....Sisi tumeapa kukilinda chama na Viongozi wake
 
Mkuu @ Idawa hoja ya Ufisadi peke yake ingekuwa inakubalika na wengi SLAA angetangazwa mshindi 2010 Jiulize kwanini hakushinda tuachane na SIASA zakukariri
 
Mbona CCM mnalalamika sana?

Hapana mkuu nimejikuta happy sana, yaani watu wako offensive line ila wanajikuta wanatakiwa kucheza kwa kulilinda lango la adui yao? wanaaendaaaa, wakiiingia kwenye 18 ya adui yao wanageuka na kuupiga mpira kwa nguvu kurudi kwa kipa wao badala ya kumshut adui. Maumivu yanabaki kwa kocha huku akimulaumu refarii badala ya kuwahoji wachezaji wake mwenyewe.
 
Unatia aibu !. Kama hujui ni bora kukaa kimya kuliko kuongea nonsense !. Chadem ina jumla ya wabunge 71 na CUF 48....hivi wewe huoni 71 ni kubwa kuliko 48 ?

CUF wameongeza kwa wabunge wa kuchaguliwa lakini CDM wana overall kura nyingi za ubunge na ndio maana wamepata wabunge wengi zaidi wa viti maalumu...

By the way we kilaza hata 2010 CUF walikuwa na wabunge wengi wakuchaguliwa kupita CDM....CUF walikuwa na 24 na CDM 23....

FL brodah!!!
usilewe ushabiki.
CDM imekuwa ama imeanza kudidimia this time?
bunge lililopita CDM ndio ilikwa na viti vingi vya ubunge na hadi kiongozi wa kambi ya upinzani alitoka CDM.
this year CDM ilijikita katika kumtafuta rais ikasahau wabunge kbs, matokeo yake tumeona CUF ikiibuka kidedea na kuwa na viti vingi ililinganishwa na CDM. CUF walijikita zaid katika kukuza chama, na kuhakikisha wanapata idadi kubwa ya wabunge ingawa pia walikuwa anamnadi rais wa umoja
kwenye bunge hili kiongozi wa kambi ya upinzani atatoka CUF ili halina ubish na usishangae kabisa coming election kwa upofu wenu CDM ikajikuta pabaya zaid
 
Kuna tetesi mawakala wa CDM kahama walitoka Arusha,, usiku wakuamkia uchaguzi wakakamatwa wakaswekwa rumande chama kikabaki hakina mawakala vituoni,,,
mkuu tulikuwa tukijaribu kuhoji mambo mengi sana ili kujenga na kurahisisha namna ya kuitoa CCM lakini tuliitwa ccm au wasaliti lakini tuliona hatari ya kushindwa na kuja kutoa visingizio rahisi...
CCM ni chama chenye uzoefu na chaguzi na kinajua ni vipi namna ya kuwin,, JPM ilikuwa karata nzuri kwao na walilipanga hili wazee ila tukadanganyana kaibuka kwa bahati mbaya..
kuishinda CCM inahitaji uwe umekomaa na akili nyingi na si akili hizi tunazoziona na huu utoto uliojaa wa vijana wenye tamaa ya kuwa viongozi kwa kete tu ya watu kuichoka CCM.. kwa manufaa ya taifa hili hizi akili za vijana wa CDM na viongozi wao sio watu wakuwapa nchi...
 
samura

CCM ndio wenye hati miliki ya nchi?
 
Last edited by a moderator:
samurai

Kwa maelezo yake wewe ni CCM uchungu wa chadema unautoa wapi?.....siutulie tu km unadhani wanajifurahisha?
 
Last edited by a moderator:
Shark

Mama Regina Lowassa 'alipewa' ubunge wa viti maalum kabla ya kuukataa. Alipigiwa kura wapi?
 
Last edited by a moderator:
Malalamiko yapo mengi tu
unless hizo taratibu hazikueleweka

la mawakala je ulijua mawakala walikaa njaa?

mkuu labda tuwe specific na eneo na eneo mm kituo nilichopigia kura mawakala walipayta chakula vzr ila ambacho inabidi tujiulize je chakula cha mawakala nanai alitoa? maana nilickia huo mzigo waliachiwa wabunge na madiwan wa maeneo husika hilo pekee nadhan si sawa!!!
 
The Boss

THE BOSS rudi kule kwe thread ya sokoine unaitwa Hata kikongwe faiza foxy amekuumbua acha ulimbukeni rudi ukajibu kule kwanza, yaonyesha ulizaliwa 1992 kwenye azimio la Zanzibar
 
Last edited by a moderator:
Mama Regina Lowassa 'alipewa' ubunge wa viti maalum kabla ya kuukataa. Alipigiwa kura wapi?????
Yaani siku zote jaribu kujiongeza kidogo kwenye kufikiria.
Mikoa iko 31, CDM imepewa nafasi 33, huoni kama kuna nafasi zitabaki?
 
Nachojua wakati wa uteuzi wa wagombea wa ubunge majimbo mbalimbali ukiendelea kipindi kile, na wadada wa viti maalum nao walikua wakichaguana vilevile, tena kupitia sanduku la kura. Sasa sielewi hii imetoka wapi tena. Kwamba yale maoni ya wana-CDM kwenye sanduku la kura hayakuzingatiwa??

Utaratibu wa kuchagua viti maalum na wagombea ubunge kwenye majimbo kwa CDM ni wa kipuuzi sana yani mkutano unaokaa kupitisha wagombea maeneo mengi ni watu 10 tu hawafiki hata 20 sasa hapo unategemea nini? watu chini ya 20 ni rahisi sana kurubuniwa na hata kupewa vitisho tu maana watu wenyewe wamejichokea ni wale wa ndio mzee.

Kama chama kitaendelea na huo utaratibu wasitegemee kupata ushindi mkubwa majimboni chukua mfano jimbo lina wapiga kura 30,000 kwenye mchakato wa kura za maoni CCM mtu anapitishwa kwa kura 9,000 wakati kwa chadema mtu anapitishwa kwa kura 11 wanapoingia kwenye uchaguzi mkuu hakuna ushindani hapo tayari mmoja ana mtaji wa kura 9,000 kwani kwa asilimia kubwa waliompitisha kura za maoni lazima watamchagua na kwenye uchaguzi mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom