Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Tunafungua ma file yote waliokwapua mikopo Nbc, import support fund,na waliokopa nssf na ppf.
 
Mzee wangu Mengi wewe ni Level ya juu sana katika nchi hii,hakuna mtu mwenye uwezo wa kukusumbua kwa lolote,
Kama kweli hii ni account yako naomba uelewe wakati umefika ukae pembeni, na ujiondoe kabisa kwenye haya maigizo!
na kama kuna mtu anatumia account bila wewe kusoma anayo post tafadhali futa kabisa hiyo account,
kama ni account feki naomba unisamehe sana!

attachment.php
Wewe hebu kwanza twambie hii post ya Mengi aliitoa lini? Hii post ina miezi zaidi ya sita kama si saba hivi unairudisha hapa ili iweje?
Mtu anaweza kudhani una mkosoa mengi kumbe lengo lako ni kutoa kashifa kwa wengine!
Hii post ya Mengi ni ya muda mrefu sana na haya yalishapita na serikali ya sasa haida muda wa malumbano na wewe unajifanya kuandika kinfiki!

Moderator Mhariri Paw naomba mtazame hii post na ilishaletwa humu kitambo!
Hebu acheni uchochezi na kuendeleza ujinga muda wa sasa ni wakujenga nchi!
 
Last edited by a moderator:
Huu ujumbe wa tangu 12/31/2014 ndio mnauibua leo.

Kweli UKAWA wameweweseka😅😅😅...CCM ni ile ile. CCM mbele kwa mbele.
Ndio maana nasema huyu Bavicha anajidai mnafiki kumsihi Mengi kumbe lengo lake ni kutoa kejeli na kuendeleza uchochezi....!
Post ya zamani anairudisha sijui ili apate nini?
 
Hivi ukifanya mtihani kwa jina lingine inabadili ukweli kuwa umefeli au umefaulu wakati mtihani ulifanya wewe?
Hii post hata kama ni ya karne ya kumi cha kujiuliza ni kweli Mheshimiwa ndiye yeye alipost. Kama ni yeye kweli sishangai kwa nini aliamua kumwoa mjukuu wake.
Namwomba ajifunze kujubaliana na ukweli.
 
Mkuu hiyo kitu ali tweet siku nyingi sana nadhani mwaka jana kabla hata ya scandal ya Tegeta Escrow account so just relax.
 
lazima amchukie muhongo anakuja sasa kufuta vitalu vya madini.
sia ajabu nyumbu au vimburu kupiga kelele kwenye mitandao
 
Mengi alimprove Muhongo wrong kwa kufungua kampuni ya Swala na kufanikiwa kuchimba Gesi na sasa kagundua hazina kubwa sana ya mafuta huko Chekereni wilaya ya Moshi vijijini Mkoani Killimanjaro.
 
Mengi alimprove Muhongo wrong kwa kufungua kampuni ya Swala na kufanikiwa kuchimba Gesi na sasa kagundua hazina kubwa sana ya mafuta huko Chekereni wilaya ya Moshi vijijini Mkoani Killimanjaro.

Wee naweee.
 
Hahaha ukiwa Mjaluo sio lazima uwe mbishi, pale ICD ni noma, hahah
mengi yupo kwenye watu waliotumbuliwa?ndio nachoitaji ututhibitishie.
nasukuru kwa kupatia kabila langu aswaaa ila ubishi cio asili yetu haaahaaa
 
Hii kitu ni ya siku nyingi sana wandugu. Ilikwisha chuja kabisa. Wakati ule Muhongo anakataa udalali wa wazawa.
 
Hii makitu mbona ya siku mingi sana? Enzi zile JK anamsepesha professa
 
mengi yupo kwenye watu waliotumbuliwa?ndio nachoitaji ututhibitishie.
nasukuru kwa kupatia kabila langu aswaaa ila ubishi cio asili yetu haaahaaa

Hahaha connect dots hapo ni yule jamaa muuza ice cream bila Shaka
 
hiyo ni photoshop kwenye TL ya mengi hakuna ushuzi kama huu!
 
Back
Top Bottom