Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 31,540
- 88,485
Nani kakwambia kwamba Mungu karuhusu kusaliti ndoa au kuoa wake wengi eti kwa sababu tu hao uliowataja walifanya hivyo? Kwa taarifa yako Suleiman aliua baadhi ya ndugu zake ili apate ufalme na Mungu akambariki akawa mfalme kwahiyo unataka kusema kwamba baada ya hapo Mungu aliruhusu kuua na kuua siyo dhambi tena kwa sababu Suleiman aliua si ndiyo? Nijibu hili
Lameki katika Mwanzo 4:19 "Lameki alioa wanawake wawili" , Ibrahimu, Yakobo, Daudi, Sulemani, na wengine, wote walikuwa na wake wengi.
Katika 2 Samweli 12:8, Mungu, akizungumza kupitia ya nabii Nathani, alisema kwamba kama wake na mahawara wa Daudi hawakuwa wa kutosha, naye angempa Daudi zaidi. Sulemani alikuwa na wake 700 na masuria 300 (kimsingi wake wa hali ya chini). Kwa hiyo, inaonekana kwamba Mungu aliweza kuruhusiwa mitala kulinda na kukimu wanawake ambao hawakuweza kupata mume kwa vyovyote vile. mitala iliwezesha upanuzi wa jamii kwa kasi zaidi, kutimiza amri ya Mungu ya "Nanyi zaeni, mkaongezeke; zaeni sana katika nchi, mkaongezeke ndani yake" (Mwanzo 9:7). Wanaume wana uwezo wa kuwatia mimba wanawake wengi katika kipindi kimoja, na kusababisha ubinadamu kukua kwa kasi zaidi kuliko kama kila mume alikuwa tu anazalisha mtoto mmoja kila mwaka.

