Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,336
- 10,895
Sasa sikupi andiko bali nakupa maandiko ambayo yanaonyesha kwamba Mungu alitaka ndoa ya mume mmoja na mke mmoja tu
Moja Mungu aliona kwamba si vema Adam awe peke yake akamfanyia msaidizi wake akamlaza usingizi kisha akautoa ubavu wake mmoja na akautumia kumuumba mwanamke mmoja tu naye ni Evah na hakumuongezea mke mwingine
Mbili mwanamume atawaacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe nao watakuwa mwili mmoja kumbuka ni mkewe siyo wakeze
Tatu mwanamume ampende mkewe na mwanamke amtii mumewe kumbuka tena ni mkewe siyo wakeze Nne kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe
Haya hayo yote ni maandiko nimeyatoa kwenye biblia kiufupi vile ambavyo Mungu alimuumbia Adam mwanamke mmoja tu ambaye ni Evah ndivyo alivyotaka ndoa zote ziwe hiyo ya kusema karuhusu makuhani na wachungaji tu ndo uone jinsi gani alivyoweka msisitizo kwamba kuwa na mke mmoja ndo muhimu
Kwahiyo wewe ubavu wako ni mwanamke mmoja tu na siyo zaidi hao wengine utakaowaongeza utakuwa unawadanganya wao na unajidanganya wewe pia na ukibishia hayo maandiko maana yake unabishia kwa jinsia zote mbili na nimekwambia Mungu hawezi kuhalalisha dhambi eti hata ingekuwa imefanywa na nani au na watu wengi kiasi gani yeye siku zote atasimamia amri zake tu
Unajua Biblia imegawanyika katika Vitabu vingapi Mkuu.
Biblia imegawanyika katika Makundi matano ya Vitabu.
1. Vitabu vya Hadithi na Historia.
Hapa kuna kitabu cha Mwanzo, Hesabu, Yoshua, Wamuzi, Ruthi, Samwel1,2. Wafalme I,2. Mambo ya nyakati, Ezra na Nehemia.
2. Vitabu vya Torati
Kutoka,Mambo ya walawi na Kumbukumbu la Torati.
3. Vitabu vya Zaburi.
Zaburi ya Daudi, Mithali, Mhubiri, Wimbo uliobora na Maombolezo.
4. Vitabu vya Manabii Wadogo.
Yeremia, Isaya, Ezekiel, Yona, Obadia N.k.
5. Vitabu vya injili.
Mathayo, Marko, Luka, Yohana, Thomas, Injili ya Magnalena n.k.
Kama hujui makundi hayo ni wazi Biblia huijui.
Sio kila fungu kwenye Biblia ni Sheria. Kunatofauti kati ya Mafundisho na Sheria za Mungu. Kwa kawaida Injili ni mafundisho yanayoelezea Sheria. Pia vitabu vya Historia kama vile Mwanzo aya zake si sheria bali zinatupa ujumbe na mafundisho mbalimbali katika sheria.
Sheria inasifa ya kukataza jambo fulani. Ndio maana utakuta neno ''USI'' Usiibe, Usizini. Usiue, n.k.
Hakuna sehemu inayosema usioe mwanamke zaidi ya mmoja zaidi ya sheria inayomhusu Askofu ambaye hutakiwa kuoa mke mmoja tena bikra.
Wewe unadhani kila jambo kwenye Biblia ni sheria. Hapo utakuwa umepotoka. Sheria zipo kwenye vitabu vya Torati ambavyo ni kutoka, Mambo ya Walawi na Kumbukumbu La Torati. Sheria yoyote isiyotoka hapo ni batili. Na inachukuliwa kama Mapokeo tuu.
Nataka kusema nini hapa. Sheria haimkatazi mtu kuoa wake wengi na wala hakuna hukumu ya jambo kama hilo kwenye Biblia.
Ni kama wakristo wanavyokataza kutoa Talaka wakati Torati inaruhusu. Ni jambo baya kuipinga torati kwa kitabu kisicho cha torati.
Hata Yesu alitoa maoni na mapendekezo yake lakini sio sheria hivyo unaweza kuyafuata au usiyafuate. Mwenye Mamlaka ya kutoa sheria ni Mungu na wala si binadamu.
Hizo Aya zote ulizonukuu ni maono na mapendekezo ya hao manabii. Waislam huyaita Sunnah. Kumbuka Torati ni maneno ya Mungu moja kwa moja wala si maoni au mapendekezo au mafundisho kama ya mitume wakina Paulo au Petro au Mtume muhamad.

