kifinga
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 5,249
- 9,577
Alafu
kule israeli wala hawana mpango na hizi vitu wao wamefanya kama sehem ya kupigia pesa huu ulokole wa wakina gwajima na lusekelo hata hawana time nao wao wana dini yao ya kuvaa kile kikofiaHuwa najiuliza kilitokea nini hadi watu wakapokwa historia yao.
Wakauziwa huu utapeli unaoitwa dini pamoja na Miungu yake kwa gharama kubwa hata ya maisha yao.
Sasa hivi watu wengi hasa wa nchi masikini ndio wamebaki kuabudu huu utapeli.Hata public figures wasioamini kwenye hayo mambo huwa wanaigiza kuamini ili waonekane wapo pamoja na wafia dini mradi wapate wanachokitaka kutoka kwao.
Yesu hakuwa na uungu kwa namna yoyote ile, alikuwa mtu wa kawaida na alishajifia zamani na kuozea kaburini[possibly aliuawa kwa makosa ya uhaini].
Wanaomsubiri sijui wanasubiri atoke wapi.
Kabla ya kifo chake Yesu alisema angerudi kabla ya kufa kwa watu waliokuwa wakimsikiliza.Cha kushangaza leo ni miaka 2017 hajaonekana popote.Kama kuna mtu anayemsubiri Yesu arudi au anayesubiri siku ya kiama ifike, huyo ni wa kumtibu.