Ujenzi: Kuzuia maji katika jengo

Ujenzi: Kuzuia maji katika jengo

greater than

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2018
Posts
1,759
Reaction score
3,222
SEHEMU YA PILI
Namna ya kuzuia maji katika jengo
1.Mfumo wa kuchepusha maji mbali na jengo
2.Uwepo wa gutter
3.Matilio zenye kuzuia maji

1.MFUMO WA KUCHEPUSHA MAJI KATIKA KIWANJA
Njia hii inatakiwa kutumika katika kukabiliana na maji yanayogusa sehemu za chini katika jengo lako,sehemu hizo ni kama Msingi,Plinth,vibaraza na kuta (usawa wa chini).
Hii ndiyo namna nyepesi na gharama nafuu zaidi katika kupambana na maji
Namna kufanikisha hivi ni
i). Kutoweka Bustani (maua/nyasi) sambamba na ukuta
ii). Kuweka kibaraza katika mzunguko wote wa kuta/eneo la jengo
iii). Kuweka mitaro inayo chepusha maji mbali na jengo
iv). Kuweka mambomba yanayo chepusha maji ardhini mbali na Msingi
v). Kuweka vizuizi vya maji katika njia ambapo maji yanatokea kabla hayajafika kwenye msingi

2.UWEPO WA GUTTER
Gutter ni kifaa kinachowekwa/fungwa kwenye ukingo wa paa kwa dhumuni la kukusanya maji ya mvua.
Katika paa za mgongo Tembo,hizi huwa na muundo wa cylinder nyembamba na huwa ya plastick au bati
Katika paa za zege huwa kuna mistari inawoekwa mwishoni mwa kibaraza,ambapo huwa kama gutter
Uweo wa gutter huambatana na Uwepo wa pipe za chini, ambazo hukusanya maji ya kwenye gutter na kupeleka chini.

3. WATER PROOFING MATERIALS
Kuna Matilio ya aina nyingi ambazo huwa zinafanya kazi ya kuzuia maji.ambazo ni

i). Matilio zenye asili ya saruji
•Hizi huundwa kwa mchanganyiko wa saruji+Mchanga+Kaolin na polymers
•Hutumika kulinda sehemu za ndani za jengo i.e vyooni,jikoni
•Mfano; Sikacemflex na sikalastic 510
•Badala ya saruji ya kawaida,tumia matilio hizi kujengea marumaru ya chooni au jikoni
  • Plasta ya ndani unaweza changanya matilio hizi na mortar ya kawaida

ii). Acyrilic coating
•Hutokna na acrylic polymers na hupatikana katika Mfumo wa kimiminika au spray.
•Hufungashwa kwenye ndoo,huwa katika rangi tofauti
•Hupakwa katika paa za zege,hupakwa kwenye kuta za handaki/basement
•Gharama yake ni kubwa
iii). Polyuretherane
•Nayo ni ina asili ya kimiminika na huwekwa kwa kupakwa kama rangia kupulizwa
•Ina dumu zaidi,ila inahitaji utaalam zaidi katika kuwekwa
•Nzuri kwenye nyufa
•XYPEX FCM

iii) Crystalline
Kwenye hii,chemicals huingia ndani ya ukuta au zege na kutengeneza crystals zenye kuzuia maji kupita
•XYPEX PATCH N PLUG
•XYPEX MEGAMIX

iv). Bitumen/Rami
•Ile rami ya kawaida ,ni kizuizi kizuri sana cha maji na majengo mengi ya zamani yametumia hii katika paa zao za zege.
  • Kuna tambala (membrane ) ya Rami ambapo sikuhizi zinatumika sana kwenye ujenzi
  • Huchomwa kwenye paa za zege
  • Lakini pia huchomwa kwenye kuta za Basment/handaki
  • Kuna Rangi za Bitumen,nazo zipo karibia kila duka la ujenzi,hupakwa kwenye misingi au kuta za parapet za kwenye paa
V). Silicone
  • Hizi ni maalum kwa ajili ya kuzipa mianya iliyopo kwenye makutano ya fremu za madirisha na ukuta,au fremu na kioo
Matilio ni zipo za aina nyingi,uchaguzi wake hutegemea
  • asili ya kitu kinachotakiwa kulindwa,kama ni chuma,mbao,tofali
  • Gharama : kuna matilio ni gharama sana ,ambapo kwa mjenzi wa kipato kidogo anaweza asimudu
  • Upatikanaji : Nje ya Dar,matilio nyingi za ujenzi zinakuwa ngumu kupatikana
  • Uwezo wa Fundi/Mjenzi wako
Wapi unaweza kupata matilio hizo,
  • Kwa Dar,nenda maduka yaliyopo Gerezani
  • Maduka ambao ni mawakala wa bidhaa za Sika na Xypex
  • Ofisi za nabaki Afrika
delta-thene-abdichtung-verarbeitung-10.jpg

Ukuta wa basement ukifunikwa na MEMBRANE YA RAMI
delta-protekt-mauerwerkssperre-3.jpg

Baada ya mkanda wa Zege,membrane ya Rami imewekwa ili kuzuia maji yasije kupanda kwenye ukuta
bituminous-coating-on-the-footing.jpg

Vitako vya misingi ya nguzo vikiwa vimepakwa Rami
acrylic-polymer-waterproofing-coating-500x500.jpg

Upakaji wa Acrylic katika paa
house_foundation_cross_section_no_text_ac2743fc.png

Mfumo wa kukusanya maji chini ya ardhi,kukwepesha yasiende kwenye msingi

Nakaribisha Maswali na maoni...

Unachangamoto inayotokana na maji,,tuma picha ili uweze kupata ushauri bila gharama
 
Pembeni ya kuta za msingi kunapakwa lami na juu kunawekwa karatasi, vipi kuhusu chini ya msingi(kitako)?.
 
Karibu dukani kwetu mwenge tunazo product za waterproof zote ambazo mtaalamu ameelezea piga 0768054537
 
Pembeni ya kuta za msingi kunapakwa lami na juu kunawekwa karatasi, vipi kuhusu chini ya msingi(kitako)?.
Swali zuri ...
sasa ipo hivi
  • Kwenye Msingi/kuta maji hupanda juu kwa Msukumo wa kapilari/capillary pressure
  • Msukumo wa kapilari ni hali ya maji kupanda juu inapokuwa kwenye njia nyembamba
  • Njia/tube kadri inavyokuwa nyembamba ndiyo maji yanaweza kwenda juu zaidi.
  • Kwenye tofali /zege zenye ubora mbovu huwa na vitundu vidogo ambavyo hupandisha maji kwenda juu
  • Maji haya huweza kupanda umbali wa sentimita 70 kwa vitundu vidogo sana.
Kumbuka msingi unashauriwa uzame ndani kwa Sentimita zisizopungua 60.
  • Lakini kumbuka msingi kwa nje hupanda sentimita 30 hadi 40,ambapo inafanya jumla ya sentimita 100 hadi 110
  • Kwahyo maji kupitia chini ya msingi ni ngumu kufikia jengo
2. Tofali za kwenye msingi unashauriwa uchukue zile imara ,
  • Zenye ratio nzuri ya mchanga na simenti
  • zilizoshindiliwa na mashine
3. Wengine tofali zilizoandaliwa na chemicals za waterproof, au kupakwa chemicals hizo kabla ya kuwekwa ardhini
wss-property-capillary-action.jpg

Tube kadri inavyokuwa nyembamba ndiyo inavyopqndisha maji juu
 
Swali zuri ...
sasa ipo hivi
  • Kwenye Msingi/kuta maji hupanda juu kwa Msukumo wa kapilari/capillary pressure
  • Msukumo wa kapilari ni hali ya maji kupanda juu inapokuwa kwenye njia nyembamba
  • Njia/tube kadri inavyokuwa nyembamba ndiyo maji yanaweza kwenda juu zaidi.
  • Kwenye tofali /zege zenye ubora mbovu huwa na vitundu vidogo ambavyo hupandisha maji kwenda juu
  • Maji haya huweza kupanda umbali wa sentimita 70 kwa vitundu vidogo sana.
Kumbuka msingi unashauriwa uzame ndani kwa Sentimita zisizopungua 60.
  • Lakini kumbuka msingi kwa nje hupanda sentimita 30 hadi 40,ambapo inafanya jumla ya sentimita 100 hadi 110
  • Kwahyo maji kupitia chini ya msingi ni ngumu kufikia jengo
2. Tofali za kwenye msingi unashauriwa uchukue zile imara ,
  • Zenye ratio nzuri ya mchanga na simenti
  • zilizoshindiliwa na mashine
3. Wengine tofali zilizoandaliwa na chemicals za waterproof, au kupakwa chemicals hizo kabla ya kuwekwa ardhini
View attachment 3576288
Tube kadri inavyokuwa nyembamba ndiyo inavyopqndisha maji juu
Maelezo mazuri. Kwahiyo nikishachimba msingi ni mambo gani yakuanza nayo kabla ya kujenga msingi wenyewe?.
 
Elimu haina mwisho.
Kazi ni kipimo cha utu
 
Back
Top Bottom