UJENZI: Kuzuia maji katika jengo

UJENZI: Kuzuia maji katika jengo

greater than

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2018
Posts
1,759
Reaction score
3,222
SEHEMU YA KWANZA
A. Maji ndiyo kitu namba moja kinachoongoza katika uharibifu na kudhorotesha uimara wa jengo.

Basi leo nitaangazia juu ya uzuizi wa maji kuweza kuharibu jengo alimaarufu kama "water proofing"

B. Madhara ya maji katika jengo

kabla ya kujadili waterproofing, kwanza hebu nikujuze juu ya madhara makubwa ya maji katika Jengo
  • Kuoza kwa Samani/Mbao
  • Kutu katika vyuma / Nondo
  • Kupukutisha Zege / Tofali
  • Uharibifu wa vifaa vya umeme
  • Shoti ya umeme
  • Kuharibika kwa Dari
  • Mazalia ya wadudu
  • Mazalia ya mimea
  • Chanzo cha ukungu/Fangasi katika jengo
  • Husaidia kusambaza chumvi
  • Kutitia kwa jengo
  • Husababisha nyufa
Hizi zote huperekea jengo kufanyiwa marekebisho ya mara kwa mara nje ya kipindi kilichopaswa

C. Sehemu zenye kufikiwa na maji
  • Msingi wa Jengo
  • Kuta za Basement
  • Kuta za Jikoni/Chooni
  • Milango ya jikoni/Chooni
  • Paa za Zege na paa kujificha
  • Kuta za nje ya jengo
  • Vibaraza na vibaraza vya juu (Balconies)
D. Namna ya Maji kufikia
Namna kuu za maji kulifikia jengo lako ni
  • Mvua
  • Maji yayopita pembeni ya jengo
  • Maji ya Ardhini
  • Maji yanayotumika katika jengo ( Jikoni,Chooni,Carwash,Sauna)
E. Wahanga wakubwa
  • waliojenga kwenye mikondo ya maji
  • waliojenga Mabondeni
  • Majengo yenye huduma zenye kuhusisha maji ; Migahawa,Carwash
  • Wenye paa za zege /Kulala
  • Waliojenga karibu na bahari
  • Wenye mifumo ya maji ndani ya nyumba
  • Waliojenga kwenye ardhi ya kichanga ambapo kuna njia za chini kwa chini za maji
Itaendelea....

Nakaribisha maswali na maoni
 
Back
Top Bottom