SEHEMU YA 72
MZALENDO
Damiani hakuwa na haja ya kumzuia sabi asiingie , kwani japo alikuwa hamuamini bwana huyu kwa asilimia mia moja , lakini jina lake kuwepo katika orodha ya wazalendo , lilimfanya amfungulie na hakuvaa tena ile sura ya Stephano lamberk bali alikuwa ni damiani mwenyewe .
“ Damiani!!!! ulikuwa ni mshangao kutoka kwa sabi mara baada ya kufunguliwa geti na mtu ambaye alikuwa akimjua , rafiki yake wa kitambo kutoka nchini Thailland ,.
“ sabi , karibu sana “ aliongea damiani huku akiwa ameweka tabasamu usoni mwake waliongozana wote kwa pamoja mpaka ndani na damiani alimkaribisha kwa hug rafiki yake sabi huku wote wakionekana kukumbukia kipindi walichokuwa pamoja wakiwa nchini Thailland .
“ ni muda mrefu sabi “
“ ni kweli damiani “.
“uliingia lini nchini Tanzania? “ aliuliza damiani .
“ mara baada tu ya kumaliza masomo yangu ya kipepelezi ndio nilirudi rasmi “
“ni kitambo kumbe , na ndio maana ulipata nafasi nzito serikalini “
“ ndio lakini nadhani mpaka sasa unajua kwanini nipo pale ikulu “.
“ hapana sijui “
“ utashindwaje kujua wakati wewe ndio mkuu wetu wa kitengo “
“ unamaannisha nini kuhusu hilo “
“ namaasha ‘ MZALENDO’
“mzalendo !?”
“ ndio damiani , najua mpaka sasa unataarifa kamili ya nini kinaendelea hapa nchini , na nafikiri ushajua machache juu ya mzalendo “
“ ni kweli , lakini hlo swala la kuwa mkuu wa kitengo limenichanganya “
“ utaelewa damiani , ilimradi nipo hapa nitakueleza kila kitu kilichotokea, natoka nchini Thailland na kurejea Tanzania , mpaka kuingia ikulu naamini pia utanieleza safari yako ya China mpaka kurudi nchini “ aliongea sabi na kisha alianza kumuhadithia damiani .
*****
Moja ya mambo yalionitia nguvu katika harakati zangu za kusomea maswala ya upelelezi ni swala la kifo cha baba yangu mzee mboneche , swala hili kwangu lilikuwa kama ni motisha , na ndio maana sikukata tamaa kabisa , nilikuwa na nia moja tu ya kuhakikisha nawapata waliohusika na mauaji ya baba yangu , japo jambo lililokua mbele yangu lilionekana kuwa gumu sana , lakini kwangu niliamiani kwa namna moja ama nyingine lazima nifanye kitu .
Mara baada ya mimi kuagana na damian , sikutaka kubweteka kwani nilitumia muda mwingi katika kujifua kimapigano ,lakini pia katika mafunzo ya kipelelezi , nilitumia Zaidi ya miezi kadhaa mbele ndio nilirudi rasmi ndani ya taifa la Tanzania .
Ilikuwa ni siku ya jumamosi ndio siku niliotua ndani ya uwanja wa ndege wa Julias Kamabarage Nyerere, mara baada ya kutua ndani ya uwanja huu kutokea terminal namba tatu nilisogea mpaka upande wa taksi , lakini ile nazikaribia tu kuna jamaa mmoja aliekuwa amevalia kofia ya NIKE alinisogelea na kama unavyojua maneno ya watu wa taksi , bwana yule ambae alikuwa na mwonekano wa kiutu uzima lakini sio sana , alikuwa ni makadirio ya miaka kuanzia therethini kwenda mbele , alinichangamkia huku akiipigia debe taksi yake , na mimi kwakua ndio ilikuwa shida yangu basi sikua na haja ya kuchukua taksi nyingine , niliingia ndani ya taksi hio na moja kwa moja tulitoka ndani ya eneo hilo , gari zilisonga, mita kadhaa wakati tukiwa tunaingia kwenye flyover , ndio nilisikia sauti ya bwana huyu ikiwa imebadilika .
“ Karibu sana Tanzania Sabi Mboneche” ndio mtu huyu ambae nilimjua kama dereva taksi ndivyo alivynikaribisha tena sauti yake ikiwa imebadilika haikuwa ile ya mwendesha taksi tena hii ilisikika ikiwa na usiriasi ndani yake .
“Umelifahamuje jina langu ?”
“ Nakufahamu vyema Sabi , tulikuwa tukikufatlia kwa muda mrefu tokea kifo cha baba yako brigedia Mboneche “
” Mlikuwa mkinifatilia nyie ni nani “
“ utajua kila kitu sabi, na nimekuja hapa kukupokea nikupeleke sehemu husika ili kupata majibu ya maswali yako yote “
“ sihitaji majibu naomba unishushe nitapanda teksi nyingne “.
“hutaki kujua chanzo cha kifo cha baba yako? , au hilo sio jambo lililokurudisha nchini “
“umejuaje yote hayo , wewe ni nani ?”
“MZALENDO “
“ mzalendo ?“
“ ndio mimi ni moja ya mwanachama wa mzalendo na wewe pia ni moja ya wanachamam wa wazalendo na ulikuwa ukisubiriwa tu “
“ sijakuelewa bado “
“ utanielewa tutakapo fika sehemu husika “
Aliongea dereva yule wa taksi na baada ya muda mfupi tulikuwa tukipita maeno ya Ubungo , sikujua ni sehemu gani bwana huyu alikuwa akinipeleka , sikuwa nikimuamini mtu , kwani moja ya kauli ya baba alioniacha nayo ni kutokumuamini mtu , na mimi sikuwa nikimuamini mtu kabisa , nilijua swala lililomuua baba lilikuwa ni swala nyeti mnoo na na mimi ilipaswa kuwa makini na kila hatua ninayo piga , lakini swala la mtu huyu kujitambulisha kwangu , lakini sio kujitambulisha kwangu tu ,alionekana akijua mambo yangu mengi , alinifanya nizidi kushangaa sana , sikutarajia kama mambo yangu niliokuwa nikiyafanya kimya kimya yalikuwa yakijulikana, nilijiua kila kitu nilichokuwa nikikifanya nilikifanya kwa siri kubwa mnno , lakini mtu huyu alikuwa akinijua vyema ,swala hilo kwangu lilinishangaza , na ndio sababu ya mimi kutulia tu kwenye gari hio ili kuona mwisho wake , nilikuwa nipo tayari kwa lolote , kwani tokea naingia nchini nilikuwa nmejipanga kwa hali yoyote nitakayo kutana nayo na swala hili kwangu niliona ni moja ya sehemu tu ya hali ambazo nilikuwa nimekwisha kuzitarajia .
Ni ndani ya kama dakika arobaini na tano hivi tulikua ndani ya eneo la kibaha , kwakweli japo nilikuwam nimeamua kila kitu kufatishana na mtu huyu ambaye nilikuwa simjui bado , lakini wasiwasi ulinizidia , kwani eneo tulilokuwepo lilinishangaza pia .
“ tunakwenda wapi ?”
“ kambini “ aliongea mwanuame huyu aliekuwa akijiita mzalendo .
“ huku ndio kambini ?”.
“ ndio , hupaswi kuwa na wasiwasi sabi , upo mikononi salama , nakuona jinsi ulivyo nawasiwsi”
“ wasiwasi ni lazima , ndio kwanza nmeingia nchini , na jambo la kwanza kukutana nalo ni swala hilo , unafikiri nitaachaje kuwa nawasiwasi”.
“unacho ongea ni sawa kabisa , na mimi nataka utoe hofu , kwani sehemu tunayo enda ni sehemu salama Zaidi , lakini wewe pia ni moja ya watu tuliokuwa tukiwasubiria “.
Baada ya kufika kwa Mathiasi tuliingia barabara ya vumbi upande wa kushoto , na gari ilipiga mwendo na ndani ya madakika kadhaaa tulikuwa mbele ya jumba moja lililozungushiwa ukuta , lililokuwa na alama juu kabisa ya ‘N’ .
Baada ya kufika mbele ya jengo hili hatimae geti lilifunguliwa na sisi tuliingia ndani , na hapo ndipo niliposhangazwa zaidi na mandhari ya eneo hilo .
Mtu alienipokea ndani ya eno hilo alikuwa ni Master P , nakumbuka wakati naingia ndani ya eneo hilo , ilikuwa ni saa tisa hivi mchana jua likiwa linawaka kali .
“karibu bwana sabi mboneche , kwenye kambi ya ‘ MZALENDO’” aliongea bwana huyu na kuzidi kunichanganya .
“hapa panahusika na nini , na kwanini nipo hapa “
“hilo sio swali la wewe kuuliza , umekuja mwenyewe kwa hiali yako hapa “ aliongea master p na kunifanya nipandwe na hasira , maana sio kweli kwamba nimekuja mwenyewe ndani ya eneo hilo , kwani mwendesha taksi ndio alienileta .
“ najua unamaswali mengi sana yakuuliza , na nikuhakikishie kwamba ndani ya muda mfupi maswali yako yatajibiwa , kwasasa unatakiwa kukutana na makamu wetu wa ‘MZALENDO’.
Sikutaka kuongea sana mara baada , kwani nilifatisha kila kitu nilichokuwa nikiambiwa kwa wakati huo , na ni kweli nilikuwa nina maswali mengi , na nilishangaa pia mpangilio wa hapo ndani ,ilionekana kama kambi ya jeshi .
Baada ya kutembea mita kadhaa ndani ya vyumba ndani jumba hilo , hatimae niliingizwa kwenye ofisi ambayo niliambiwa ndio makamu alipo na hapo ndipo nilipo pigwwa na butwaa .
Aliekuwa mbele yangu alikuwa ni Madam Wema, mke wa raisi wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania.
“ karibu sana Sabi Mboneche “
“asante sana madam “ nilijibu kwa wasiwasi huku nikikaa .
“ ni mara yangu ya kwanza kuonana na wewe ana kwa ana “
“ ndio madam , hata mimi sikutegemea kama nitaonana na wewe eneo hili “
“ huna haja ya kunishangaa sabi , nikupe pole na safari “
“ asante sana “
“nipo hapa kwa ajili ya kukujibu maswali yako “.
“nitakushuru sana madam “
“naomba nikuulize swali kabla sijaendelea ?”
“ hakuna shaka madam unaweza kuuliza “
“ je unaamini baba yako alikufa kifo cha kawaida “nilishagnaa lakini sikuwa na budi kujibu .
“ hapana , baba yangu ameuliwa “
“ unajua aliemuua baba yako ?”
“ hapana , na nipo hapa nchini kwa ajili ya kujua ni nani aliehusika kumuua baba yangu “
“walio husika kumuua baba yako ni U-97”
“U-97?”
“ ndio Ni ufupisho wa unity 97 au UMOJA NAMBA TISINI NA SABA “
“ ndio nini madam ?”
“hii ni taarifa fupi ya UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ,” alinipa flash
“ kwa muda wako utapitia na utaelewa nusu ya umoja huo”
‘ lakini niseme kwamba sababu ya baba yako kufariki kwasababu alijua mambo ambayo hakutakiwa ajue , kiufupi alikuwa amejua karibia nusu ya umoja namba tisini na saba na hio ndio iliompelekea kuchomwa sindano ya sumu “
“ ilikuwaje baba yangu akajua yote hayo ?”.
“hio ni taarifa utakayo ipata kwenye mafaili utakayokuta kwenye hio flashi , inahusu mchakato mzima wa umoja huo hapa nchini , lakini jambo lilolofanya baba yako kufatilia umoja huo ni kutokana na amri kutoka kwa raisi bendera , kwani mheshimiwa alijua kuwa taarifa ya awali aliokuwa nayo juu ya umoja NAMBA TISINI NA SABA ilikuwa sio sahihi , kulikuwa na mambo ya ziada na ndio yaliompelekea baba yako kuanza kufatilia na pale alipokuwa akiukaribia ukweli ndipo alipo uwawa “
“ madam kwakweli ndio naanza kujua , na jambo hili limenishangaza mno , lakini linaonekana kuwa kubwa mno “
“ sio jambo dogo sabi na ndio maana upo hapa , sisi unaotuona hapa tupo hapa kwa ajili ya kuendeleza mapambano ya kujua ni nini maana ya umoja huu ndani ya nchi yetu lakini pia kuundoa kabisa , na hilo ndio jukumu la MZALENDO .
“hili nifaili lenye taarifa zote zinazohusiana na mzalendo “ alinipatia flashi nyingine .
“ mwisho , nadhani umepokea mafunzo ya kutosha hivyo jiandae kwa mapambano ya kuendeleza kile ambacho baba yako hakukimaliza “
“ nina swali madam “
“ mh”
“wakati baba yupo hatua za mwisho za uhai wake alinipa namba ambazo nilipiga simu , na kupitia namba hizo nilipata kupokea maelekezo ya kwenda nchini Thailand , nataka kujua kama na nyie mnahusika juu ya namba hizo ?”
“ hizo namba hazipo chini ya mpango wa MZALENDO bali zipo chini ya mpango X(tunauita mpango x kwasababu hatuujui jina ,, rejea ripoti Ajenti zakayo ).
“mpango x ?”
“ ndio , kwa taarifa za awali mpango huu ulikuwa ukiratibiwa na Daniel mtalemwa na marehemu bruno lamberk , na mpaka sasa hatujui juu ya mpango huu mpaka mtu ambae tunatarajia atakuja kuendeleza “
“ kuna mtu ambae ameandaliwa juu ya mpango x?”
“ Damiani Rabani “.
“Damiani Rabani ?”
“ unamfahamu ?”
“ ndio nimekutana nae nchini Thailland akiwa na historia inayofanana kiasi kama yangu , lakini kuna mambo ambayo tulikuwa tunatofatiana , tulikuwa marafiki , lakini kwasasa yupo nchini China “.
“ni vyema kama mlionana , huyo ndie mtu tunaemtegemea ili sisi kama wana umoja huu wa MZALENDO tuanze kazi na mimi nipo kama kivuli tu kwani kazi yangu itakamilika pale damiani atakapo kidhi vigezo vya kuwa kiongozi wa MZALENDO , lakini wakati tunamsubiria damiani kuna misheni yako ya kwanza ambayo unapaswa kuifanya “
“ misheni gani hio madam ?”
“ unapaswa kuingia ikulu ili iwe rahisi ya kuwasiliana na mimi “.
“ kuingia ikulu ?”
“ndio , unapaswa ufanye juu chini mheshimiwa raisi akuamini na hatimae kukupa uongozi ndani ya ikulu hio itafanya kazi yetu kuwa rahisi “
.”litawezanaje hilo ?”
“ mpango wa misheni hio ushaandaliwa , na maelekezo yote utapewa na mpaka sasa nikwambie sina la ziada la kuongea na wewe kila kitu utakielewa kupitia hizo faili ,”
Madam wema baada ya kuongea maneno hayo aliondoka , na mimi nilizungushwa ndani ya kambi hio ya MZALENDO na kuangalia kila kitu kilichokuwa kikipatikana humo , kiufupi ni sehemu ambayo ilikuwa ikijjitegemea sana , kwani ilikuwa na kila kitu kwanzia maswala ya kiteknolojia , siraha , mpaka sehemu za kufanyia mazoezi .
Baada ya hapo nilirudishwa mjini huku nikiambiwa eneo hilo nitafika kwa mwaliko maalumu .
ITAENDELEA
SEHEMU YA 73
THE LIST(ORODHA )
Baada ya kutoka hapo nilielekea moja kwa moja hotelini ,sikutaka kufika nyumbani moja kwa moja , nilienda hotelini , nilikuwa na hamu kubwa ya kujua nini kipo ndani ya hizo faili ambazo madam wema alinipatia , nilitaka kujua Zaidi kuhusu huu UMOJA NAMBA TISINI NA SABA ,.umoja ambao umehusika na kifo cha baba yangu .
Baada ya kufika hoteli ya Landmark niliweka makazi hapo kwa siku moja ili kufatilia swala hilo , baada ya kukaa nilitoa laptop yangu ya kampuni ya apple na kisha nilichomeka flash ile na kufungua , na ni kweli nilikutana na faili la U-97 katika faili hili kulikuwa na mambo kadha wa kadha yaliofanywa na raisi bendera katika kutokomeza umoja huu , huku jambo kubwa la umoja huu lililokuwa likijulikana ni swala la madawa ya kulevya , kwani umoja huu ulihusishwa na madawa ya kulevya , jambo ambalo lilinishangaza ,.
Nilishangaa Zaidi baada ya kuona moja ya watu ambao walikuwa wapo kwenye umoja huu akiwemo raisi mstaafu Athumani Ndalu , lakini pia na viongozi wengine pamoja na matajiri .
Lakini pia ripori ilionesha iliishia kutoa hitimisho kwamba umoja huu sio kama Tanzania tunavyoufahamu , Brigedia Mboneche na mheshimiwa bendera ndio wanaujua undani wa umoja huu kwani wao ndio waliokua na ripoti kamili ya umoja huu . lakini ukweli huo umeambatanishwa kwenye nyaraka ambazo haijulikani ni nani amekabidhiwa nyaraka hizo ambazo zimepewa jina kama KAULI YA MWISHO YA RAISI KABLA YA KIFO.
Hio ndio ripoti iliokuwa kwenye flash , baada ya kumaliza kusoma ripoti hio huku moyo wangu ukienda mbio , kwani japo nilitarajia jambo ambalo naenda kukumbana nao lilikuwa jambo kubwa , lakni sikuwa nikidhania kuwa jambo hilo litakuwa kubwa namna hio .
Niligeuka kwenye faili la MZALENDO
Taarifa iliopo kwenye faili hili ilikuwa ni siku kamili ya kuanzishwa kwa umoja huu ambapo ilikuwa ni mwaka wa nne wa awamu ya kwanza wa utawala wa raisi bendera , huku mwanzilishaji akiwa yeye mwenyewe ,sababu za kuanzishwa kwa umoja huo ni kutokana na kwamba ndani ya usalama wa taifa(TSS) kulikuwa na mashushu wengi wa U-97 hivyo jaribio lolote la kuondosha umoja huo lisingefanikiwa hio ilikuwa sababu kuu , lakini kigezo cha kuwa MZALENDO kilikuwa ni watu ambao hawajawahi kuhudumu katika fani ya usalama wa taifa, yaani vijana wapya , huku sababu ya kuhusisha vijana hao ni ili kuhakikisha kuondosha umoja huu unafakikiwa pasipo ya maadui kujua mienendo yao .
Pia kulikuwa na orodha ya watu kumi ambao ndio agent wa MZALENDO watakao husika katika kuiondosha U-97 ndani ya taifa la Tanzania , huku katika orodha hio jina langu lilikuwepo , na la damiani , Janeth , Merina sosteness , Patrick henry mushi , Abasi shayo , Zakayo , Elvice benard , Pancho na Karim .
Hayo ndio majina ya watu wanaohusika na orodha ya MZALENDO na kiongozi katika orodha hio alikuwa ni damiani rabani(akikidhi vigezo) .
Hakukuwa na kingine cha ziada .
Basi baada ya siku kadhaa kupita ndio nilipatiwa mpango wa misheni ya kuingia ikulu , tukio la misheni hii lilikuwa likifanyika siku ambayo ni maazimisho ya miaka hamsini ya ndoa ya mheshimiwa raisi na madam wema , na ndani ya tukio hili nilihitajika kupigwa risasi kumlinda raisi , na mtu atakae tekeleza tukio hilo alikuwa ni bwana karim , mtaalamu wa maswala ya kuendesha drone.
Hilo ndio tukio lililotokea siku ile sasa kama unakumbuka ,, ilikuwa ni misheni maalumu ya mimi kuingia ikulu .
Kwenye moja ya vitu vilivyonisisimua Zaidi ni teknolojia ambayo ilikuwa ikimilikiwa na MZALENDO teknolojia ya kijivika sura ya mtu mahali popote pale baada ya kufanya tukio na ndio maana hata suzzane alishindwa kujua ni nani haswa muhusika wa matukio yale baadala ya kukamata watu wengine ambao hawakuwa wakihusika , hio yote iliwezeshwa na teknolojia iliokuwa ikijulikana kwa jina la FTP( FACE TEMPO PICKER ).
****
“ nadhani mpaka hapo utakuwa umeelewa sasa nilivyosema , kuwa wewe ndio kiongozi wetu “.
“ ndio sabi”
“ kukutana kwetu kulikuwa kwa bahati sana nchni Thailland , kumbe kuna watu waliokuwa wakituangalia muda wote “
“ ni kweli kabisa sabi , tunakazi kubwa sana ilioko mbele yetu “ .
“tena kubwa sana , umoja huu upo ndani ya serikali hivyo itakuwa ngumu sana lakini inawezekana “
“ nadhani tutaongea siku zijazo , lakini kwa usalama wa kile tunacho kifanya inabidi tusionekane kuwa na ukaribu “.
“ ni kweli kabisa , kwa haya yanayo endelea inabidi tuwe makini sana , huu umoja unaonekana upo kila mahali “
“ nina mambo mawili ambayo yamenifanya kukutafuta damiani “ aliongea sabi , na huo ni muda ambao damiani alinyanyuka kwenda kuchukua chupa yenye mvinyo na kumiminia sabi kwenye glass na yeye kwenye glass .
“ nadhani huu utakuwa wakati mzuri wa sisi kuongea hayo mambo “ aliongea sabi huku akitabasamu , alikuwa akikumbuka mengi waliofanya wakiwa na sabi nchini thailland , japo alikuwa na wasiwsi juu ya sabi , lakini kutokana na hsitoria yake sasa alikuwa akimuamini sana , na damu yake ilikuwa ikitembea kwa kasi kila anapokumbuka collabo watakayo enda kufanya kutokomeza UMOJA NAMBA TISINI NA SABA .
“ la kwanza ni juu ya merina “ aliongea sabi na kumfanya damiani akae vizuri .
“ vipi kuhusu merina , unamfahamu ?”
“ ushasahau kwamba na yeye yupo kwenye orodha ya MZALENDO ?”
“sijasahu , lakini sidhani unachotaka kusema kinahusiana na hilo ?”
“ ni kweli , ni juu yako wewe na merina .. namaanisha uhusiano wenu “.
“ kwanini unauliza hivyo sabi ?”
“yule mwanamke anakupenda damiani na hilo ni jambo ambalo linanitia waswasi mpaka sasa “
“Nalifahamu hilo , lakini kwanini likutie wasiwasi , ni jamnbo la kawaida kumpenda mtu “
“ kumpenda mtu au kupendana ?”
“ unamaanisha nini ?”
“ nataka kujua kama wewe pia unampenda “ aliongea sanbi na hapo alimfanya damiani aanze kujifikiria ,, kiufupi hakutegemea swali kama hilo mapema namna hio , hata yeye alikuwa hana uhakika kwamba alikuwa akimpenda sana merina kama yeye anavyompenda .
“ndio “
“ ndio nini damiani ?”
“ umeuliza kama nampenda .. ndio nampenda “ sabi alijikuta akivuta pumzi .
“ unamfahamu patrick mtoto wa raisi henry “.
“ ndio namfahamu ?”
“ anampenda sana huyo mwanamke , na yupo tayari kufanya lolote lile ili awe na merina , na anajua uwepo wako hapa Tanzania na yupo tayari kukupoteza ili awe na merina ,, hilo ndio swala linalonipa wasiwasi “.
“damiani wewe ni rafiki yangu na Patrick pia ni rafiki yangu , namjua sana Patrick na anachozungumza nina uhakika anamaanisha , hivyo naomba swala hili ulifikirie kwa mapana yake pasipo kuacha kitu chochote kinachohusu maisha yako kwa sasa , maamuzi utakayofanya naamini yatakuwa na tija kwenye mpango wetu , hilo nadhani ndio kipaumbele kwa sasa “ aliongea sabi
“ nitalifanyia hilo kazi sabi , usiwe na shaka “ aliongea damiani na sabi aliitika kwa kichwa .
“ swala la pili ni wewe kuwa stephano lamberk , na damiani kwa wakati mmoja , najua teknolojia imekuwa sana na safari yako ya china nadhani ilikuwa ya mafanikio makubwa sana “
“ China imeendelea sana katika swala zima la teknolojia sabi , mimi mwenyewe sikuamini mara ya kwanza lakini , niseme mpaka sasa naiogopa sana teknolojia , kwani kitendo cha mimi kuja nchini kwa jina la stephano lamberk mwenywe ni swala ambalo linanifanya kila mtu ninaemuona nione ni feki “
“ hahaha.. kwakuwa wewe mwenyewe ulikuwa feki “
“ ndio “
“sina muda sana lakini utanieleza kwa kina juu ya hilo, lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba suzzane mpaka sasa anajua stephano lamberk ni damiani , japo hana uthibtisho lakini ana uhakika “.
“nililitegemea hilo sabi na nimejiandaa vyema “
“ ni vizuri sasa kama utajiweka wazi kama damiani na sio stephano lamberk tena “
“ni kweli kabisa “
“hii ni barua kutoka ikulu , mheshimiwa anahitaji kuonana na wewe siku ya kesho “
“ anahitaji kuonana na mimi ?”
“ ndio sijui ana dhumuni gani , laakini hakikisha unafika “
“ nitafika “
Basi baada ya maongezi hayo sabi aliondoka na kurejea ikulu , kwani kazi iliokuwa imempeleka hapo alikuwa ashaimaliza .
******
“okey merina , unaweza ukaniambia , mahusiano yako na damiani yalianza lini ?” lilikuwa ni swali kutoka kwa janeth kwenda kwa merina , na merina alijikuta akishindwa kujibu swala hilo , kwani ni kweli mpaka wakati huo ni kama yeye ndie aliekuwa akimpenda damiani pasipo kujua kuwa mwanaume huyo alikuwa akimpenda pia , hivyo hata swala la uhusiano , lilikuwa hata halijaanza na hivyo jibu hakuwa nalo .
“hilo swali siwezi kujibu ni maswala yangu binafsi , na nimekuja hapa kuongea na damiani sio wewe professa “ aliongea merina na kumfanya janeth akunje nne na kufanya kijisketi alichovaa kionyeshe mapaja yake yalio nona, na kama wewe ni mwanaume rijali ungewaona warembo hawa , basi ungeishia kusema kwamba kijana damiani ana bahati sana .
“okey merina , ni kweli naweza nisipaswe kujua , mahusiano yako na damiani , lakini mbona damiani hajawahi kukutaja kama ashawahi kuwa na mpenzi anaeitwa merina “ janeth hakutaka kuwa mzembe na yeye alirusha kombora .
“ mpaka akutajie , wewe ni nani yake , hayo ni mambo yake binafsi na wewe ni mfanya kazi wake , kwanini akuambie maswala yake yanayohusu mahusiano “
“ siwezi kuweka mambo yangu binafsi kwako pia , lakini kukuambia tu ni kwamba mimi na damiani mapenzi yetu yalianzia nchini China , na mpaka sasa tunaendelea “.
“unasemaje ?” merina aliuliza hilo swali huku tayari machozi yakiwa yashaanza kumtoka ,moja ya sifa ya mwanadada huyu ni kuwa na machozi ya karibu .
“ndio hivyo merina , nisamehe sijakusudia kukuumiza , lakini naamini wewe na damiani sio wapenzi ,kwani hajawahi kukutaja na isitoshe muda wote alikuwa akikuona hapa kwa sura ya stephano lamberk, unafikri angekuwa anakupenda angejificha kwako “.
Maneno aliongea janeth yalikuwa yamemuingia vyema sana merina , na kila neno alilolizungumza kwake aliona ni ukweli mtupu , hakuwa na lingine la kuongea zaidi ya kunyanyuka nakuondoka huku akijikaza machozi yasimtoke , kwani hakutaka kuonana na wafanya kazi wa kampuni hio akiwa na machozi .
Baada ya merina kutoka hapo alikimbilia gari yake , na baada tu ya kuingia alishindwa kujiuzia kwani alianza kulia kilio cha kwikwi , alikaa hapo kwa muda wa madakika kadhaa huku janeth aliekuwa juu ya goroa akimwangalia .
Baada ya madakika hayo alilitoa gari na kuelekea nyumbani kwake, japo alikuwa na maumivu moyoni lakini alijitahidi kuendesha gari kwa umakini ili asije akasababisha ajali.
****
Damiani mara baada ya kuachana na sabi , jambo moja ambalo alikumbuka kulifanya wakati huo ni swala la kuangalia kilichomo kwenye ile flashi aliokabidhiwa na madam wema , alikuwa na hamu mmno nakujua ni kipi bruno alimuachia , hivyo alitoka hapo sebleni na moja kwa moja alielekea kwenye chumba chake.
Baada ya kufika alitoa flash ile kwani alikuwa ameihifadhi kwenye kabati na kisha akaisogelea tarakishi yake iliokuwa ndani ya chumba chake hicho kwani kuna sehemu aliokuwa ametenga kama kijiofisi.
Baada ya kuichomeka , alienda moja kwa moja kuifungua flashi hio na hapo ndipo alipokutana na faili moja tu lililoko kwenye mfumo wa ‘zip’ yaani limefungwa , alijaribu kufungua faili hilo lakini alishindwa kwani lilikuwa likihitaji password kulifungua.
Alitulia kwa madakika kadhaa akifikiria password gani ya kuingiza hapo , na hapo ndipo alipokumbuka nyaraka alizopewaga na bruno , alizifata kwenye ‘safe box’ na kuzitoa kisha kaingiza password ambayo ilikuwa ikitumika kwenye kadi ya benki ya CRDB bank na ni kama aliotea vile kwani faili lile lilifunguka.
Kwa hamu kama zote za kutaka kujua nini kipo kwenye faili hilo aliangalia , na kitu alichokuta ilikuwa ni file kwanza lilikuwa na jina lililokuwa limeandikwa SELLINE AMBER , jina ambalo mara baada ya kulisoma tu alikumbuka aliliona kwenye nyaraka za mwanzo kabisa alizokuwa amepwa na bruno.
Alifungua faili hilo ambalo lilikuwa kwenye mfumo wa ‘Document ’ na kitu ambacho kilimshangaza ni kwamba faili hili lilikuwa na KB moja tu ukubwa wake , lilifunguka na ndani ya faili hilo kulikuwa na neno moja tu lilikuwa limeandikwa kwa herufi kubwa .’DANTE – CHEST CARD ( TANZANIA SWISS BANK BRANCH )’
Hayo ndio maneno pekee yalioandikwa kwenye faili hilo ,kwa mara ya kwanza alianza kujiuliza maneno hayo yalikuwa yakihusu nini , lakini hakuelewa kwa mara moja ,alikaa na kuanza kufikiria na nikama kuna kitu alikuwa akikimbuka lakini kilikuwa kinakuja na kupotea , kila alipo jaribu kukumbuka , alishindwa kabisa .
“ huenda kuna ‘clue’ kwenye hizi nyaraka za bruno “ aliongea na kisha alitoa kila kitu akaangalia kimoja kimoja kwenye zile karatasi alipita lakini hakupata jibu , na wakati akiendelea kusoma zile karatasi kuna jambo alilikumbuka na kujiona ni kama mjinga , alikumbuka kadi ya uswisi ilikuwa kwenye nyaraka hizo , haraka haraka aliangalia kadi hio na neno la kwanza kuliona lilikuwa ni ‘ DANTE’.
“ Yess ni hii “ aliongea
“chest card kadi ya kuhifadhia vitu vyenye thamani benki, hii sio kadi ya ATM ni chest card” alijiongelesha .
Baada ya kuvumbua fumbo hilo hap hapo aiingia , mtandaoni na kutafuta neno DANTE SWISS BANK IN TANZANIA na ndani ya muda mfupi alikuwa amepata kila kitu mpaka eneo husika .
Sehemu yenyewe ilikuwa ni ndani ya jengo la TPA sokoine , hakutaka kuchelewa alijiandaa dakika chache na kisha aliingia kwenye gari lake akiwa na sura ya stephano lamberk na moja kwa moja alielekea posta , ndani ya madakika kadhaa alikuwa nje kabisa ya jengo hilo akiegesha gari , alienda floor ya chini na kuangalia sehemu bank hio inapatikana floor ipi na aliona ipo floor namba saba , aliingia kwenye lift na kuja kutokezea kwenye floor hio , na kulikuwa na wafanyakazi wachache na baadhi ya watu ambao walionekana wapo mahali hapo kwa ajili ya huduma , hakujihangaisha nao , kwani alienda moja kwa moja mapokezi na kuulizia utaratibu huku akitoa ile kadi na mwanadada yule alievalia sare zake , huku akipendezeshwa na miwani , aliiangalia na kisha alimpa maelekezo ya kwenda upande wa kulia , sehemu ambayo kulikuwa na mhudumu mwingine ambae alikuwa na tarakishi kubwa akionekana kuwa bize , baada ya kufika alitoa ile kadi na kisha alimpatia na bwana yule wa kiume alivalia tisheti ambayo ilikuwa na nembo ya benki hio , aliafanya yake na ndani ya muda mfupi alikuwa ashamaliza .
“ nifate tafadhari , aliongea bwana yule kwa heshima kabisa kwani alkuwa akimjua bwana stephano lamberk kwa pesa zake , hivyo alikuwa akimnyenyekea .
“ ni hapa boss wangu ,, namba za boksi ni hizo mbili za mwisho kwenye kadi yako , utaingiza hio kadi na boksi itafunguka “
“ nashukuru “
Damiani baada ya maelekezoo hayo aliingia na kweli alipata boksi ile na aliingiza kadi kwa maelekezo yale na ndani ya dakika aliambiwa aingize namba ya siri na hapo ndipo alipo babaika kwani alikuwa hajui , ila aliona aingize namba ile ile ya mwanzo ya CRDB na ikakubali .
Baada ya kukubali tu boksi ile ilifunguka na ndani kulikuwa na bahasha moja tu ya khaki , alichukua bahasha ile na kisha akatoka nayo na moja kwa moja alienda mpaka kwenye gari yake , na baada ya kuingia tu alitoa vitu vilivuyomo mle ndani .
Ilikuwa ni hati ya nyumba iliokuwa inajina la bruno lamberk nyumba iliokuwa ikipatikana eneo la mbezi beach , lakini pia kulikuwa na picha kama picha ya mlima Kilimanjaro halafu chini yake kulikuwa na maandishi kama tarehe lakini sio tarehe , zilikuwa ni herufi ukiangalia kwa umakini na damian kwa akili yake haraka haraka aligundua ni passcode .
“aliwasha gari na hapo nia yake kubwa ilikuwa ni kwenda moja kwa moja eneo la mbezi beach , aliendesha gari yake kwa spidi kidogo na ndani ya madakika kadhaa alikuwa eneo hilo , na kwakua hakua mzoefu sana alienda moja kwa moja mpaka kwa mwenyekiti wa mtaa , na akamuonesha hio hati , mwenyekiti wa mtaa huyo alikuwa ni bwana mmoja mfupi mwenye kitambi .
“karibu sana , tulikuwa tukikusubiri “ aliongea bwana huyo na kumfanya damiani ashangae , lakini hakutaka kuongea mengi , kwani bwana yule aliinuka na kuongozana na mzee yule alietembea kwa shida na kitambi chake , na kama dakika tano walikuwa kwenye jumba moja kubwa sana lilokuwa upande wa kulia upande wa kaskazini kutoka baharini .
“ni hapa mheshimiwa “ aliongea mzee yule
“ na damiani aliingiza mkono mfukoni na kutoa noti kumi na kumpatia mzee yule , na mzee alikenua hadi jino la mwisho .
Damiani aliingia kwenye nyumba hii ambayo ilikuwa kabisa na mlinzi , na ndani ya nyumba hii ilikuwa na mandhari nzuri kabisa , akifatana na yule mzee .
“kuna mtu anakaa hapa ?”
“ hapana , ila tulikuwa tukiifanyia usafi mara kwa mara kwani ndio maelekezo kutoka kwa mwenye nyumba aliotuachia “
“kuna maelekezo mengine ?”
“ hakuna ni , wewe ndio mwenye nyumba yako na kwasasa tunakukabidhi kila kitu na mkataba wetu wa kuiangalia nyumba hii umeisha leo “
“ basi nashukuru “
Basi mzee yule aliondoka na kumuacha damiani akianza kuangalia mle ndani , ilikuwa ni moja ya nyumba nzuri sana ,na kubwa ya kisasa , yenye gorofa tatu kwenda juu , mwenyewe aliisifia hio nyumba , ile ya kwake ya makongo juu haikuwa nzuri kama hii .
Aliingia ndani huku akipokelewa na fanicha(samani) , kuna kitu alikiona chini , yalikuwa ni maganda ya kondomu pamoja na chupa za bia , na moja kwa moja alijjua lazima yule mzee kama sio yeye basi kuna watu aliokuwa akiwapa waje kufanya yao humo ndani , kwani nyumba ilionekana kabisa ilikuwa inakaliwa na mtu , lakini hakutaka kujisumbua Zaidi juu ya hilo .
Kwani kwa siku hio jambo lililompeleka hapo lilikuwa ni jambo moja tu , kujua picha ile inamaanisha nini , aliingia kwenye vyumba baadhi , na chumba cha tatu kuingia ndio chumba alichokutana na picha ile ya mlima Kilimanjaro , hiki kilikuwa ni chumba ambacho alikuwa akilala bruno , ni chumba kikubwa kweli na cha kisasa mno .
Alitoa ile picha ya ukutani , na hapo nipo alipokutana na sehemu ya kuingiza namba , aliingiza namba zilizokuwa kwenye ile picha na ndani ya dakika kadhaa tu sehemu ile ilijitenga na kutengeneza mlango kama wa lift , jambo ambalo lilimshangaza damiani , kwani muda huo alikuwa yupo gorofa ya mwisho juu .
Aliingia ndani na lift ile ilianza kushuka taratibu na ni sekunde kadhaa ilisimama na kufunguka na mbele yake kulikuwa na mlango ambao haukua na komeo wala ila pembeni yake ulikuwa na sehemu ya kuweka kidole yaani fingerprint damiani alijaribu kuweka .
“ACCESS DENIED PLEASE ENTER SECURITY BY PASS CODE “ maandishi yalisomeka na hapo damiani ndipo alipojua kuwa zile password zilikuwa ni za kubypass hio system .
Aliingiza na hapo hapo mlango ule ulifunguka .
“WECOME IN LEGACY ROOM DAMIANI RABANI
ITAENDELEA JUMAPILI MCHANA NICE WIKIEND
NO: 0687151346 Watsapp