PostGE2025 Uingereza yataka uchunguzi huru Matukio ya vifo Oktoba 29 nchini Tanzania

PostGE2025 Uingereza yataka uchunguzi huru Matukio ya vifo Oktoba 29 nchini Tanzania

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections
Ni maoni yake yaliyowafurahisha, lakini Tz ni taifa huru kama ilivyo uingereza. kama sisi hatuwezi kuwaagiza wafanye jambo kwaajili ya watu wao hata wao hawawezi kutuagiza jambo kwaajili ya watu wetu. Tumeshavuka huko.
Nilikuwa nakusoma sana humu kumbe nilijipotezea mudq tu. Kwani Israeli, China na urusi zilizotajwa kwenye hotuba yao siyo nchi huru? Au ni uhuru upi unaoringia huku ukiwa mwanachama wa kamati na umoja wa mataifa?
Hebu tafutq muda uyasome masharti ya kuwa mwanachama wa UN na idara zake kisha utuambie Tanzania ina uhuru unaouongelea?
Ishauri nchi yako ifuate na kuyaishi waliyokubaliana huko UN vinginevyo jiondoeni huko.
Msipime upepo huu wa nchi zenye ushawishi mkubwa duniani mtaangamia soon.
 

Serikali ya Uingereza imeifikisha Tanzania katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), ikitaka kufanyika kwa uchunguzi huru na wa kina kufuatia kile ilichokiita "ukatili wa kushtua" uliotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025, ikiwemo tuhuma za mauaji ya kinyume cha sheria na miili ya wahanga kufichwa.

Hoja hiyo imewasilishwa na Balozi wa Haki za Binadamu wa Uingereza, Eleanor Sanders, wakati wa mdahalo mkuu wa 61 wa Baraza hilo jijini Geneva, Uswizi Machi 2, 2026. Uingereza imetumia jukwaa hilo la kidiplomasia kuishinikiza Tanzania kutoa majibu juu ya mfululizo wa matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu yaliyoripotiwa nchini humo.

Katika tamko hilo, Balozi Sanders ameweka wazi kuwa Uingereza ina taarifa na ushahidi wa matukio ya kusikitisha yaliyojiri kufuatia mchakato wa uchaguzi, jambo ambalo limeutia doa utawala wa sheria na demokrasia nchini.

Pia soma PostGE2025 - Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025

"Lazima kuwepo na uchunguzi huru, wa wazi na jumuishi wa matukio haya ili kuhakikisha uwajibikaji na kwamba uhuru wa msingi na haki za kikatiba za Watanzania wote zinalindwa," amesisitiza Balozi Sanders.

Hatua hii ya Uingereza ‘kuishitaki’ Tanzania mbele ya Baraza la Haki za Binadamu wakati ambao Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, iliyoundwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ikiendelea kukutana na kufanya mahojiano na watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa sasa, wastaafu, na wadau mbalimbali ili kukusanya taarifa na ushauri wa kitaalamu juu ya kile kilichotokea.

Mbali na kuisaka haki nchini Tanzania, Uingereza imetumia fursa hiyo kukemea ukiukwaji wa haki maeneo mengine ikiwemo Gaza na Ukingo wa Magharibi ikiitaka Israel kuruhusu misaada na kusitisha ujenzi wa makazi; China, ikitaka kuachiliwa kwa watu waliowekwa kizuizini kiholela Xinjiang na kukomeshwa kwa kazi za suluba; na Ukraine, ikiendelea kuunga mkono mamlaka ya nchi hiyo dhidi ya uvamizi wa Urusi.
IMG_20260304_123156.jpg
IMG_20260304_123504.jpg
 

Serikali ya Uingereza imeifikisha Tanzania katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), ikitaka kufanyika kwa uchunguzi huru na wa kina kufuatia kile ilichokiita "ukatili wa kushtua" uliotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025, ikiwemo tuhuma za mauaji ya kinyume cha sheria na miili ya wahanga kufichwa.

Hoja hiyo imewasilishwa na Balozi wa Haki za Binadamu wa Uingereza, Eleanor Sanders, wakati wa mdahalo mkuu wa 61 wa Baraza hilo jijini Geneva, Uswizi Machi 2, 2026. Uingereza imetumia jukwaa hilo la kidiplomasia kuishinikiza Tanzania kutoa majibu juu ya mfululizo wa matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu yaliyoripotiwa nchini humo.

Katika tamko hilo, Balozi Sanders ameweka wazi kuwa Uingereza ina taarifa na ushahidi wa matukio ya kusikitisha yaliyojiri kufuatia mchakato wa uchaguzi, jambo ambalo limeutia doa utawala wa sheria na demokrasia nchini.

Pia soma PostGE2025 - Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025

"Lazima kuwepo na uchunguzi huru, wa wazi na jumuishi wa matukio haya ili kuhakikisha uwajibikaji na kwamba uhuru wa msingi na haki za kikatiba za Watanzania wote zinalindwa," amesisitiza Balozi Sanders.

Hatua hii ya Uingereza ‘kuishitaki’ Tanzania mbele ya Baraza la Haki za Binadamu wakati ambao Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, iliyoundwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ikiendelea kukutana na kufanya mahojiano na watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa sasa, wastaafu, na wadau mbalimbali ili kukusanya taarifa na ushauri wa kitaalamu juu ya kile kilichotokea.

Mbali na kuisaka haki nchini Tanzania, Uingereza imetumia fursa hiyo kukemea ukiukwaji wa haki maeneo mengine ikiwemo Gaza na Ukingo wa Magharibi ikiitaka Israel kuruhusu misaada na kusitisha ujenzi wa makazi; China, ikitaka kuachiliwa kwa watu waliowekwa kizuizini kiholela Xinjiang na kukomeshwa kwa kazi za suluba; na Ukraine, ikiendelea kuunga mkono mamlaka ya nchi hiyo dhidi ya uvamizi wa Urusi.
 
Ni maoni yake yaliyowafurahisha, lakini Tz ni taifa huru kama ilivyo uingereza. kama sisi hatuwezi kuwaagiza wafanye jambo kwaajili ya watu wao hata wao hawawezi kutuagiza jambo kwaajili ya watu wetu. Tumeshavuka huko.
Don't forget kwamba hata Iran na Venezuela ni mataifa huru.
 
Geneva, UN HRC

Mawasilisho wa Uingereza mjini Geneva yalikuwa haya hapa chini kuhusu Tanzania :

UK Human Rights Council 61 : UK Statement for the Item 2 General Debate​

UK Statement for the Item 2 General Debate. Delivered by the UK's Human Rights Ambassador, Eleanor Sanders.
Published2 March 2026

Location:GenevaDelivered on:2 March 2026 (Transcript of the speech, exactly as it was delivered)
Eleanor Sanders

Mr President,

We are grateful for the High Commissioner’s update.

The humanitarian situation in Gaza remains of serious concern. We urge Israel to allow and facilitate rapid and unimpeded passage of humanitarian aid in line with international law. We call on all parties to implement the 20-point peace plan and respect the ceasefire. In the West Bank, rising violence and settlement activity risk instability and undermines prospects for peace.

Tanzania saw shocking violence following its elections in October, including evidence of extra-judicial killings and concealment of dead bodies. There must be an independent, transparent and inclusive investigation of these events to ensure accountability and that the fundamental freedoms and constitutional rights of all Tanzanians are protected.

We appreciate your efforts to engage China, including on the findings of his Office’s Xinjiang Assessment from 2022. But we are concerned by continued evidence of China’s transition from using re-education camps to using prisons and labour transfer schemes. We call on China to address reports of forced labour, and restrictions on religious and cultural freedoms; China must release all arbitrarily detained individuals.

Finally, we support unequivocally Ukraine’s sovereignty, independence and territorial integrity. We continue to support the work of UN mechanisms and their reporting - those responsible for violations and abuses of human rights must be held accountable.

Thank you.
Published 2 March 2026
Uingereza ndio chanzo cha mzozo wa Palestine na Israel, ndio waliokuwa wanatawala eneo lile la Palestine kama wakoloni sasa wanashindwa kuutatua. Wameshindwa Gaza wataweza Tanganyika? Hata hapa Tanzania uingereza ndio chanzo cha mgogoro pale Zanzibar.
 
Don't forget kwamba hata Iran na Venezuela ni mataifa huru.
Ni tofauti kabisa na sisi, huku kwetu mlalamikaji ni chadema ya TAL na kule Venezuela na Iran walalamikaji ni Marekani na Israel, tofauti kabisa buana!!!.
 
Ni tofauti kabisa na sisi, huku kwetu mlalamikaji ni chadema ya TAL na kule Venezuela na Iran walalamikaji ni Marekani na Israel, tofauti kabisa buana!!!.
Marekani na Israel huo ni umwamba tu wa kuziingia nchi, internal politics zilivyokuwa Venezuela hazina tofauti kabisa na za TZ. Walalamikaji wa TZ wanatoka nyanja tofautitofauti though na CHADEMA ni moja ya walalamikaji, this is a very good excuse kama nchi ingekuwa na resources za maana wababe wangeshaingia kitambo ila hapa kinachokuja kufanyika ni kumbinya Samia mpaka anye utumbo.
Very soon atakunya utumbo.
 
Hata akistaafu, hili litamfuata hadi siku anaingia kaburini! uliza akina DURTETE kwani walikuwa madarakani walipokamatwa?
TENA itakuwa powa, maana baada ye yeye kuondoka anakuja msiyempenda mheshimiwa sana TAL Rais wa JMT
Na tutazitaifisha Mali zake alizoibia watanganyika hasa zile zinazoonekana zilizoko bara
 
Wachague wadili na Pascal au wawajibu kuhusu mauaji waliyofanya October 29
 

Serikali ya Uingereza imeifikisha Tanzania katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), ikitaka kufanyika kwa uchunguzi huru na wa kina kufuatia kile ilichokiita "ukatili wa kushtua" uliotokea baada ya uchaguzi wa Oktoba 2025, ikiwemo tuhuma za mauaji ya kinyume cha sheria na miili ya wahanga kufichwa.

Hoja hiyo imewasilishwa na Balozi wa Haki za Binadamu wa Uingereza, Eleanor Sanders, wakati wa mdahalo mkuu wa 61 wa Baraza hilo jijini Geneva, Uswizi Machi 2, 2026. Uingereza imetumia jukwaa hilo la kidiplomasia kuishinikiza Tanzania kutoa majibu juu ya mfululizo wa matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu yaliyoripotiwa nchini humo.

Katika tamko hilo, Balozi Sanders ameweka wazi kuwa Uingereza ina taarifa na ushahidi wa matukio ya kusikitisha yaliyojiri kufuatia mchakato wa uchaguzi, jambo ambalo limeutia doa utawala wa sheria na demokrasia nchini.

Pia soma PostGE2025 - Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025

"Lazima kuwepo na uchunguzi huru, wa wazi na jumuishi wa matukio haya ili kuhakikisha uwajibikaji na kwamba uhuru wa msingi na haki za kikatiba za Watanzania wote zinalindwa," amesisitiza Balozi Sanders.

Hatua hii ya Uingereza ‘kuishitaki’ Tanzania mbele ya Baraza la Haki za Binadamu wakati ambao Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani ya Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, iliyoundwa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ikiendelea kukutana na kufanya mahojiano na watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa sasa, wastaafu, na wadau mbalimbali ili kukusanya taarifa na ushauri wa kitaalamu juu ya kile kilichotokea.

Mbali na kuisaka haki nchini Tanzania, Uingereza imetumia fursa hiyo kukemea ukiukwaji wa haki maeneo mengine ikiwemo Gaza na Ukingo wa Magharibi ikiitaka Israel kuruhusu misaada na kusitisha ujenzi wa makazi; China, ikitaka kuachiliwa kwa watu waliowekwa kizuizini kiholela Xinjiang na kukomeshwa kwa kazi za suluba; na Ukraine, ikiendelea kuunga mkono mamlaka ya nchi hiyo dhidi ya uvamizi wa Urusi.
Waambieni kwanza wakafanye uchunguzi huru huko Gaza ambako watoto wameuliwa kwa mabomu na waliosalia wanakufa kwa kukosa chakula.

Tanzania ni nchi huru isiyofungamana na upande wowote. Ina Katiba yake ambayo inatoa mamlaka kwa Rais kuunda tume ya kuchunguza jambo lolote.

Tuache kuwashobokea hawa wakoloni wetu. Hata wenyewe mbkna wana shida nyingi tu? Wala sisi hatujawahi kuitwa kwenda kuwachunguza!!
 
Hako ka mama kako kataishia jela na tu nakwambia. Au kamestaafu au bado, lazima kataenda lupango
Akili za kimasikini hizo. Unawaza mtu fulani atapata madhara halafu hayamfiki hayo madhara. Basi ndo mnasubiriiia wenyewe na kupeana matumaini
 
Hata akistaafu, hili litamfuata hadi siku anaingia kaburini! uliza akina DURTETE kwani walikuwa madarakani walipokamatwa?
TENA itakuwa powa, maana baada ye yeye kuondoka anakuja msiyempenda mheshimiwa sana TAL Rais wa JMT
Poleni sana. Mna maumivu makali sana kwa kusubiri mtu adhurike
 
Jinai haijawahi kufa atafikiwa tu hata awe wapi na wote waliohusika sasa unastaafu na kuanza kuishi kwa hofu na msongo wa mawazo
Matumaini hewa!
Mkapa aliua sana tu na watu walijipa matumaini hivyo hivyo
 
Huyo ni mama yake Abdul
Acha kujipendekeza Kwa mama Wanu

Uchawa usikusahaulishe Hadi mama yako
Wanastaafu waliopewa ridhaa na wanachi
Tukaneni weeeee lkn haibadli kitu kama hamjipangi kwa mikakati yenu wenyewe. Kutegemea Mzungu awafanyie mshapoteana
 
Back
Top Bottom