muuza ubuyu
JF-Expert Member
- Nov 23, 2010
- 3,542
- 3,588
-Wanatumia pesa zote hizo kwa ajili ya gym ili iweje?
-Sioni hata mmoja anayeenda na mke wake bungeni!
-Sote tunaona wanavyohangaika na vibinti mpaka wanachukuana picha mnato!
-Ahaaaaaaaaa, naona wanahangaika sana na vitambi vyao kuwashughulikia 'wapiga kura' wao hivyo inabidi waingie kwenye msitu wa gym ili wawe fit!
-Tunasubiri kwa hamu kuona 'album' zao mpya wakisalimia wapiga kura wao huku wakionekana kuwa na stamina hatari baada ya kutengeneza gym kwa pesa kibao ambazo ni kodi zetu mimi na wewe huku wenzangu na mimi heshima yetu ndani ya 'master room' ikizidi kushuka kutokana na mihangaiko mikubwa ya mchana kutwa ili kulipa kodi iliyotengeneza gym ya kuwajengea heshima wabunge wetu mbele ya vimada vyao!
NASEMA TENA: NASUBIRI PICHA ZAO WAKIWA NA NGUVU KAMA ZA SIMBA WAKIWASHUGHULIKIA VIMADA WAO. SI GYM BWANA?!
-Sioni hata mmoja anayeenda na mke wake bungeni!
-Sote tunaona wanavyohangaika na vibinti mpaka wanachukuana picha mnato!
-Ahaaaaaaaaa, naona wanahangaika sana na vitambi vyao kuwashughulikia 'wapiga kura' wao hivyo inabidi waingie kwenye msitu wa gym ili wawe fit!
-Tunasubiri kwa hamu kuona 'album' zao mpya wakisalimia wapiga kura wao huku wakionekana kuwa na stamina hatari baada ya kutengeneza gym kwa pesa kibao ambazo ni kodi zetu mimi na wewe huku wenzangu na mimi heshima yetu ndani ya 'master room' ikizidi kushuka kutokana na mihangaiko mikubwa ya mchana kutwa ili kulipa kodi iliyotengeneza gym ya kuwajengea heshima wabunge wetu mbele ya vimada vyao!
NASEMA TENA: NASUBIRI PICHA ZAO WAKIWA NA NGUVU KAMA ZA SIMBA WAKIWASHUGHULIKIA VIMADA WAO. SI GYM BWANA?!
Kabla vumbi la ufisadi wa bilion 200 halijatua, ufisadi mwingine wa kutisha umeibuliwa tena bungeni. Ufisadi huu unahusisha matumizi ya Tsh bilion 2.8 kwa kisingizio cha ujenzi wa gym ya bunge inayodaiwa kugharimu kiasi hicho cha fedha.
Licha ya kwamba gym hiyo ni white elephant, haiwezekani gym moja tu igharimu fedha nyingi kiasi hicho. Watanzania wenzangu, hivi ni lini serikali hii 'sikivu' ya CCM itaacha kutafuna fedha za wanananchi? Wakati wanafunzi wanasomea chini ya miti na kuketi sakafuni au juu ya matofali, serikali hii isiyokuwa na khaya inawezaje kutafuna fedha za umma kiasi hiki? Fedha hizi kama zingeelekezwa kwenye ujenzi wa madawati, madarasa, maabara ya shule za kata au nyumba za walimu, haya matatizo yangebaki historia. Lakini kwa kuwa serikali ni 'sikivu', wakaona njia sahihi ni kufisidi fedha za umma kwa kutumia kisingizio cha kujenga gym!
Yaani hawa walafi waibe fedha za umma watengeneze vitambi halafu watumie tena fedha za umma kupunguza vitambi hivyo? Marvelous!!