Ufisadi mwingine waibuliwa Bungeni!

Ufisadi mwingine waibuliwa Bungeni!

Wanatia hasira hasaaaa.....Kwani hiyo gym wanaulazima nayo gani si waende za kulipia huko binafsi, hadi gym watengenezewe na hela za walipa kodi? vya bure tuu..

Hivi ni lini na sisi wananchi tutajengewa gym kule Tandale kwa Bibi Nyau au kule Manzese Uwanja wa Fisi. Hivi kweli kabisa serikali hii ya CCM inaidhinisha mabilioni ya shilingi kujenga hiyo miundombinu ya anasa wakati watoto wetu wanasomea chini ya mti na kukaa juu ya udongo? Wananchi tuache kulalamika sana bila kuchukua hatua. Tujiandikishe kwa waingi ili tuwaondoe hawa panya madarakani mwaka ujao.

darasa chini ya mkuyu.jpg
Darasa chini ya mkuyu

View attachment 163735
Wanafunzi wakisomea juani

wanafunzi wamekalia udongo.jpg
Wanafunzi wakiwa wamekalia udongo

wanafunzi wamekalia matofali.jpg
Wanafunzi wakiwa wamekalia madawati ya matofali
 
Wanatia hasira hasaaaa.....Kwani hiyo gym wanaulazima nayo gani si waende za kulipia huko binafsi, hadi gym watengenezewe na hela za walipa kodi? vya bure tuu..

Mkuu, madudu haya yanatia hasira sana. Tujiandikishe kwa wingi ili mwaka ujao tuwaondoe hawa panya madarakani. Inatia hasira sana kuona ufisadi wa kutisha kama huu huku wananchi tukiwa bado tunawachekea hawa panya wa magamba wakati wanamaliza mahindi kwenye kihenge. Dawa ya kuepukana na adha hii ni kuunguza kibanda kizima kwa moto ili tujenge kihenge kipya mwaka ujao.
 
bavicha kwa matusi hamjambo, yani huwezi kuchangia bila matusi

Jirudishie akili angalau kwa leo tu ujue tunachokiongea hapa. Mazezeta kama nyie ndio mtasababisha nchi hii iingie vitani. Unadhani wananchi watakubali kuona fedha zao zikiliwa hivi wanyamaze milele? Tumia akili mkuu.
 
ili mradi mnaendelea kuuabudu mwenge,akili zenu zitaendelea kuwa butu.

Uchawi ule ule aliotambikiwa mwl.nyerere ili mahakama za kikoloni ziwe bubu ni uchawi ule ule uliobebwa kwenye mwenge mwendelee kumulikwa ili macho na masikio yenu yaone na yasikie lakini yasifahamu.

Mwenge huo mwenge mbio mbio!

mkuu umenena lililokua wazo langu,nilitaka kusema hvyohvyo mwenye ndo uchawi wenyewe ati,cku ukiwekwa makumbusho ndo cku ya watanzania kuzinduka usingizin.
 
Mwisho wao utakua 2015 pale Chadema tutakapokua magogoni ni aibu kubwa sana kila sehemu ni kuchepuka chepuka tu kuweni nahuruma japo kidogo au hamtaki tukingia madarakani japo tukute account
 
Tanzania hata ukikwapua matilioni hutafanywa kitu chochote, alimradi uwe ccm! Pia wabunge wetu ni wasanii hakuna mfano, kwao ni kujikomba kwa mafisadi na chama tawala basi! Wamewasahau watanzania kabisa!
 
Unaweza kuugua na kufa ukifuatilia mambo ya serikali hii isiyojua inakoelekea
 
Kama nyumba ya kuishi inagharimu zaidi ya Bilioni mbili, je kuhusu gym yenye vifaa vya kisasa kibao?

Lizabon,wewe ki uhalisia unaishi ktk nyumba yenye thamani ya sh ngapi?Unazungumzia nyumba ya 2billion?kuwa ni jambo la kawaida?Wacha kutetea maovu ndugu yangu kwani Tanzania ni ya Wa Tanzania.
 
Hivi ni lini na sisi wananchi tutajengewa gym kule Tandale kwa Bibi Nyau au kule Manzese Uwanja wa Fisi. Hivi kweli kabisa serikali hii ya CCM inaidhinisha mabilioni ya shilingi kujenga hiyo miundombinu ya anasa wakati watoto wetu wanasomea chini ya mti na kukaa juu ya udongo? Wananchi tuache kulalamika sana bila kuchukua hatua. Tujiandikishe kwa waingi ili tuwaondoe hawa panya madarakani mwaka ujao.

View attachment 163733
Darasa chini ya mkuyu

View attachment 163735
Wanafunzi wakisomea juani

View attachment 163736
Wanafunzi wakiwa wamekalia udongo

View attachment 163737
Wanafunzi wakiwa wamekalia madawati ya matofali

Inahudhunisha sana,kwa serikali yetu kufulbia macho shida wazipatazo watoto wetu,
 
Msigwa anesema kuwa usitegemee mabadiliko wakati akili ndogo inapoongiza akili kubwa!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kabla vumbi la ufisadi wa bilion 200 halijatua, ufisadi mwingine wa kutisha umeibuliwa tena bungeni. Ufisadi huu unahusisha matumizi ya Tsh bilion 2.8 kwa kisingizio cha ujenzi wa gym ya bunge inayodaiwa kugharimu kiasi hicho cha fedha.

Licha ya kwamba gym hiyo ni white elephant, haiwezekani gym moja tu igharimu fedha nyingi kiasi hicho. Watanzania wenzangu, hivi ni lini serikali hii 'sikivu' ya CCM itaacha kutafuna fedha za wanananchi? Wakati wanafunzi wanasomea chini ya miti na kuketi sakafuni au juu ya matofali, serikali hii isiyokuwa na khaya inawezaje kutafuna fedha za umma kiasi hiki? Fedha hizi kama zingeelekezwa kwenye ujenzi wa madawati, madarasa, maabara ya shule za kata au nyumba za walimu, haya matatizo yangebaki historia. Lakini kwa kuwa serikali ni 'sikivu', wakaona njia sahihi ni kufisidi fedha za umma kwa kutumia kisingizio cha kujenga gym!

Yaani hawa walafi waibe fedha za umma watengeneze vitambi halafu watumie tena fedha za umma kupunguza vitambi hivyo? Marvelous!!

mm wakati mwingine najiulizaga ihi serikali yetu inaishi kifahari kama serikali ya obama??? msafara wa magari yakifahari! warsa kwenye mahoteli makubwa! miposho minono! kutengeneza tshet na skafu mpaka hand bag! sherehe za muungano mabilion ya pesa na mbwembwe za vifaru! nakumbuka kwenye bunge la katiba wajanja walitaka kutafuna bilioni 8 za siwa! bado tukaambiwa kuweka viti na kukarabati bunge kwa ajili ya wajumbe wa katiba zaidi ya bilioni 28 zilitumika? amakweli nchi ihi ni shamba la bibi.
 
Lizabon,wewe ki uhalisia unaishi ktk nyumba yenye thamani ya sh ngapi?Unazungumzia nyumba ya 2billion?kuwa ni jambo la kawaida?Wacha kutetea maovu ndugu yangu kwani Tanzania ni ya Wa Tanzania.

mkuu lizabon,na wenzake ni wanufaika wakubwa wa ufisidi.inashangaza mtu mwenye akili timamu kutetea wizi!!!!!!awa ndio,,,,,:hungry::hungry::hungry::hungry::hungry:!!!!!!!!!!!
 
Kwa ratiba ya shughuli zao wataitumia saa ngapi hiyo gym... haya matatizo ya kuiga nadhani walitembelea bunge la nchi moja ya ulaya wakaona kuna gym katika jengo la bunge, bila kutafakari wakaja na wazo la kujenga gym... mtu kama Komba gym itamsaidiaje?
 
Hakuna cha kulalamika hapo wanafunzi wataendelea kukaa chini wakati tuna miti chungu nzima,wajawazitu wataendelea kujifungulia kusikofaa wakati tuna madini,dhahabu,gesi etc,yote haya ni maandalizi ya kupata pesa za kuhonga wapiga kura 2015,kazi kweli kweli
 
Kama nyumba ya kuishi inagharimu zaidi ya Bilioni mbili, je kuhusu gym yenye vifaa vya kisasa kibao?

Wee nyamaza kimya weny akili waandike. Unaijua gym? Vifaa vya kisasa vipi? Hiyo gym ina rockets za kulipulia makalio yenu?
 
hiyo 2.8 b ni pamoja na nguo na raba za mazoezi alizozawadiwa makinda?? hy gym ni shiidaaaa aanze kwenda komba
 
Hii habari imenisikitisha sana sure nimeumia mnooo kuna watanzania wanaishi kwa shida jamanI acheniiiii
 
Back
Top Bottom