Hivi Lizaboni ni lazima uchangie kila hoja? Hata hivyo kama unataka kuchangia kila hoja ielewe hoja kwanza basi. Suala hapa ni ivi hatuna vipaumbele? Shaule zetu, zahanati zetu, wakulima wetu, watoto wetu, wafanyakazi wetu, n.k. wamefikiriwa kabla ya kuwekeza kwenye gym ya bunge wakati wabunge wanakaa kwenye mahoteli yaliyo na gyms, na pia muda wanaokuwepo Dodoma ni mdogo sana, na pia ni rahisi kwao tena kwa hela ndogo tu kufanya mazoezi kwenye gym za jumuia - public gyms. Kwanini basi wabunge wetu wasiwakumbuke watoto wetu wasio na maabara katika shule zetu za sekondary za umma? NA kibaya zaidi hiyo gym haijajengwa - ni white elephant kama mtoa mada alivyodai.
Watanzania tuna shida nyingi sana kuliko hili la wabunge kuwa na gym.
Jamani watanzania tumechoka kubeba mzigo huu wa wabunge sasa, mara posho, mara shangingi, mara hiki vyote vikidhihirisha ubinafsi wa waabunge wetu, kuweni binadamu jamani wabunge wananchi wana shida kubwa kweli kweli halafu mbaya zaidi hiyo ni kodi ya mlalahoi hata yule anayepata mshahara wa shilingi 200,000 kwa mwezi. Oneni aibu ndugu zetu msiwalazimishe watanzania kufikia hatua ya kuingia barabarani tofauti ya asili yetu ya upole ( ustaarabu ) - ambao nyie mnaita amani.
Lizaboni tunaweza kuwajengea wabunge wetu gym hata ya trilion moja, lakini ni wakati muafaka? Baba unanunua suti ya laki saba watoto wanakosa ada ya shule jamani! Wabunge wetu kuweni watu wenye utu na huruma kwa wapiga kura wenu.