naunga mkono hoja. inawezekana kabisa kuutoa huu ukoo wa panya ni kwa kuingia msituni.Mkuu, huu ukoo wa panya unaudhi sana, mpaka wanahamasisha vita! Ipo siku watanzania tutakuja kuingia msituni (ule aliopo Kapteni Komba) tupambane na hawa panya mpaka kieleweke.
Well said, Mystery.
Sifa kubwa ya kuwa mwana CCM ni "uhamnazo".
Kweli mkuu, nyumba ya gavana wa benki kuu ilipigwa rangi mpya kwa thamani ya billioni 2.8 na kina MSALANI wanaoishi kwenye mabanda sombetini wakashangilia kwelikweli kuwa ni halali kabisa kiasi hicho kutokomea kwa ukarabati mdogo tu kama huo, kweli ccm ni wachawi haswa! Kuweza kuwaloga watanzania wengi ukawakandamiza na kuwaibia, kuwapora, kuwapiga, , kuwaua na kuwadhalilisha jinsi unavyotaka ba bado wakakuabudu kunahitaji miujiza.
Lakini mkuu haya tunayataka sisi wenyewe,(mimi na wewe) ingekuwa haya yanatokea halafu mi na wewe tunatimua kivumbi pale Posta mpya cha Kama siku 3 hivi, kuchoma moto gari za serikali na uharibifu mwingineo kushinikiza walaji wa Mali ya umma wawajibishwe unadhani haya yangetokea? Tena sio kufanya hivyo mara moja, uwe mtindo wa Mzalendo kupinga kwa nguvu zote pindi anaposikia Mali ya umma inafujwa.Naamini hakuna serikalini ambae angekuwa na mawazo ya kufuja Mali za uma. Lkn tunabariki tu, shughuli ipo kwa hakika.
Kapteni KombaGym nani apige chuma?
Said Mkumba na Maji Marefu,Nkamia,Mwigulu wanataka vifua kwani bungeni kuna Ulinzi wa mabaunsa?
Kabla hatujaanza kuchangia hebu tupe BOQ ya jengo hilo ( BILLS OF QUANTITES).Kabla vumbi la ufisadi wa bilion 200 halijatua, ufisadi mwingine wa kutisha umeibuliwa tena bungeni. Ufisadi huu unahusisha matumizi ya Tsh bilion 2.8 kwa kisingizio cha ujenzi wa gym ya bunge inayodaiwa kugharimu kiasi hicho cha fedha.
Licha ya kwamba gym hiyo ni white elephant, haiwezekani gym moja tu igharimu fedha nyingi kiasi hicho. Watanzania wenzangu, hivi ni lini serikali hii 'sikivu' ya CCM itaacha kutafuna fedha za wanananchi? Wakati wanafunzi wanasomea chini ya miti na kuketi sakafuni au juu ya matofali, serikali hii isiyokuwa na khaya inawezaje kutafuna fedha za umma kiasi hiki? Fedha hizi kama zingeelekezwa kwenye ujenzi wa madawati, madarasa, maabara ya shule za kata au nyumba za walimu, haya matatizo yangebaki historia. Lakini kwa kuwa serikali ni 'sikivu', wakaona njia sahihi ni kufisidi fedha za umma kwa kutumia kisingizio cha kujenga gym!
Yaani hawa walafi waibe fedha za umma watengeneze vitambi halafu watumie tena fedha za umma kupunguza vitambi hivyo? Marvelous!!
Kabla hatujaanza kuchangia hebu tupe BOQ ya jengo hilo ( BILLS OF QUANTITES).
Kama nyumba ya kuishi inagharimu zaidi ya Bilioni mbili, je kuhusu gym yenye vifaa vya kisasa kibao?