Ufafanuzi wa kisheria watolewa kufuatia kujiondoa kwa Jaji Elinaza Luvanda kesi ya uhujumu uchumi na ugaidi wa Freeman Mbowe na wenzake..

kwingine nimekuelewa ila hapa...

endelea kutoa ufafanuzi wa kisheria...

je hati ikikosewa inatoa mwanya wa kuondolewa kwa kosa?

JIBU:
Absolutely, YES.

1. Kwa sababu, mashtaka hayo yanakosa sifa na vigezo vya kisheria kuitwa mashtaka na kesi hiyo inaishia hapo ktk hatua hiyo katika USO WA MAHAKAMA....

Hiyo ndiyo kazi ya Jaji/mahakama, yaani kuamua shauri kwa mujibu wa sheria...

2. Kwa polisi yaweza kuwa tofauti. Kama watakuwa bado wanadhani lipo kosa kwa mtuhumiwa huyo, ni jukumu lao kufuata sheria na taratibu za kipolisi kuanzisha mashtaka upya...

Kumbuka, HATI YA MASHTAKA [charge sheet] ndiyo sura nzima ya kesi/shauri lililofika mahakamani...

Kuikosea kwa namna yoyote ile, kwa Justice system iliyo serious & fair, basi hiyo inakuwa ni hatua ya kwanza kumpa faida (advantage) mshtakiwa kuupiga TKO upande wa mashtaka..

Haya ndiyo makosa wayafanyayo mara kwa mara waendesha mashtaka wa serikali ya Tanzania aidha kwa makusudi au kwa kutojua au kwa sababu ya nature ya kesi zenyewe wanazozipeleka mahakamani kuwa za hila, siyo halisi...
 
Umeshajiuliza kama kuna ushahidi Jamhuri wanasema wanao?, Unafikiri Jaji ageweza kuuacha tu ukaenda na maji?. Jibu ni hapana. Haki ni kwa pande zote mbili haki haipo kwa mshitakiwa tu bali hata mshitaki anayo haki ya kushitaki, unafikiri Jaji angeweza kuivunja iyo haki kirahisi hivyo?

Swali lingine ni mnaposema haki ya Mh. Mbowe imevunjwa ni haki gani hiyo?, Kama ni haki ya yeye kuachiwa huru hiyo haki haiwezekaniki bila Jamhuri kusikilizwa ushahidi wao, sasa utasikilizwaje ndani ya hati ya mashtaka yenye walakini?, Suluhisho ni nini ili Jamhuri asikilizwe?,

Hayo maswali ukiyatafakari utapata standing ya Mh. Luvanda J. wala haitakupa wasi wasi ulio nao sasa ukifahamu kuwa
Popote linapotajwa neno haki ijulikane ni pande mbili sio pande moja Mkuu.
Hivi haya unayoandika unayatoa wapi? ni sheria ipi unayotumia kuandika haya? ni sheria au rule ipi inayomzuia jaji kutoa haki kwa mshtakiwa kama hati ya mashtaka imekosewa, huo ushahidi kama wanautaka lazima ufuate taratibu toka mwanzo sio kulazimisha tu wakati hatua za mwanzo zimekosewa, huyu jaji mnatumia nguvu nyingi kumlinda bila sababu.

Unavyosema haki ya Mbowe haiwezi kupewa kama jamhuri bado ina ushahidi ni uongo, haya ni mawazo yako binafsi hayapo kisheria, hivi kama Chadema wangekuwa wameishtaki jamhuri na hati ya mashtaka Chadema wakaikosea unadhani jaji angetoa maelekezo kama aliyotoa kwa upande wa jamhuri? hii kesi ni ya kisiasa usihangaike kuwalinda wateule wa CCM.
 
Kufuatia kujitoa kwa Jaji Elinaza Luvanda anayesikiliza shauri linalowakabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa ndugu Freeman A. Mbowe na wenzake watatu katika kesi ya uhujumu uchumi na ugaidi iliyoko mahakamu kuu DSM, baada ya mshitakiwa namba 3 Freeman Mbowe kuonesha "kutokuwa na imani" naye, wengi tumekuwa tukitoa maoni yetu hewani bila kuwa na reference ya kisheria.

Katika video hii, mawakili wa mahakama kuu wasomi ndugu Peter Madeleka na Fatuma Karume wanatupa ufahamu wa kisheria jinsi mambo yalivyo na baada ya kuwasikiliza, kila mtu awe huru kutoa maoni yake sasa iwapo ilikuwa ni halali kwa Jaji huyu kujitoa au vinginevyo.

Ipo kazi...hii itaishia kwa serikali kudhalilishwa. Na bahati yao Tundu Lissu hayupo, wangeenda kuchekea chooni
 
Hivi haya unayoandika unayatoa wapi? ni sheria ipi unayotumia kuandika haya? ni sheria au rule ipi inayomzuia jaji kutoa haki kwa mshtakiwa kama hati ya mashtaka imekosewa, huo ushahidi kama wanautaka lazima ufuate taratibu toka mwanzo sio kulazimisha tu wakati hatua za mwanzo zimekosewa, huyu jaji mnatumia nguvu nyingi kumlinda bila sababu.
Asante sana kwa ufafanuzi wenye maswali ya kumjengea ufahamu atakaye kujua...

Mimi nimeandika mara nyingi humu kuelimisha wagumu wa kuelewa, kuwa, katika shauri hili ishu ni;

1. Siyo ushahidi upo au haupo;

2. Siyo kuwa Mbowe ni gaidi au siyo gaidi

BALI ishu hapa inayoleta mzozo na sintofahamu hii ni namna waendesha mashtaka wa serikali walivyoandaa na kuanzisha mashtaka haya ambayo reflection yake inaonekana kwenye hati ya mashtaka [charge sheet]...

Yaani kwa lugha rahisi kabisa, mtu yeyote mwenye kudadisi aweza kusema, HATI YAO YA MASHTAKA [CHARGE SHEET] ni "KAMA" inathibitisha rumours zilizozagaa mitaani kuwa kesi hiyo ni ya kumbambikiza, ni ya UONGO ni ya KUMKOMOA tu Freeman Mbowe...

Kwa hapa JF & other social medias, jaribu kuwasikiliza au kuwasoma wote wanaojaribu kuitetea serikali na upuuzi huu...

Yaani wote hawana hoja kabisa. They are all shooting in the air....!!
 
Asante sana kwa ufafanuzi wenye maswali ya kumjengea ufahamu atakaye kujua...

Mimi nimeandika mara nyingi humu kuelimisha wagumu wa kuelewa, kuwa, katika shauri hili ishu ni;

1. Siyo ushahidi upo au haupo;

2. Siyo kuwa Mbowe ni gaidi au siyo gaidi

BALI ishu hapa inayoleta mzozo na sintofahamu hii ni namna waendesha mashtaka wa serikali walivyoandaa na kuanzisha mashtaka haya ambayo reflection yake inaonekana kwenye hati ya mashtaka [charge sheet]...

Yaani kwa lugha rahisi kabisa, mtu yeyote mwenye kudadisi aweza kusema, HATI YAO YA MASHTAKA [CHARGE SHEET] ni "KAMA" inathibitisha rumours zilizozagaa mitaani kuwa kesi hiyo ni ya kumbambikiza, ni ya UONGO ni ya KUMKOMOA tu Freeman Mbowe...

Kwa hapa JF & other social medias, jaribu kuwasikiliza au kuwasoma wote wanaojaribu kuitetea serikali na upuuzi huu...

Yaani wote hawana hoja kabisa. They are all shooting in the air....!!
Kesi yoyote ili usikilizwaji wake ukamilike inakuwa na steps, na hizo step lazima zote zifuatwe kwa ukamilifu wake na kwa usahihi unaohitajika, kukosea step yoyote kati ya hizo kesi inaamuliwa kwa ku favour upande wa pili.

Sasa huyu jaji kawafundisha serikali jinsi ya kuandika charge sheet hadharani simply bcoz nae ni muajiriwa wa serikali hiyo hiyo, I doubt kama angefanya hivyo kwa upande wa upinzani kulingana na record zao.

Hii kesi haiwezi kutenganishwa na siasa, ni ya kisiasa ndio maana ina mambo mengi ya ajabu ajabu, hawa wanaojidai kutumia "taaluma" kwenye kesi ya kisiasa ni utapeli tu, huu utetezi wanaoleta hapa ni kuficha aibu, nothing else.
 
Kesi yoyote ili usikilizwaji wake ukamilike inakuwa na steps, na hizo step lazima zote zifuatwe kwa ukamilifu wake na kwa usahihi unaohitajika, kukosea step yoyote kati ya hizo kesi inaamuliwa kwa ku favour upande wa pili.

Sasa huyu jaji kawafundisha serikali jinsi ya kuandika charge sheet hadharani simply bcoz nae ni muajiriwa wa serikali hiyo hiyo, I doubt kama angefanya hivyo kwa upande wa upinzani kulingana na record zao.

Hii kesi haiwezi kutenganishwa na siasa, ni ya kisiasa ndio maana ina mambo mengi ya ajabu ajabu, hawa wanaojidai kutumia "taaluma" kwenye kesi ya kisiasa ni utapeli tu, huu utetezi wanaoleta hapa ni kuficha aibu, nothing else.
That's right...

Uongo hauwezi kutengenezewa maelezo yaliyonyooka ugeuke use ukweli...

Hata wapewe kufanya regrouping mara mia, hawataweza kuugeuza uongo uwe ukweli...!!
 
Kwa vijana wa Chadema, Jaji kujitoa kwenye kesi wanafikiri is a big deal, lakini kumbe ni jambo la kawaida kabisa. Nina rafiki yangu hapa Mwanza ana kesi na mimi ndie mshauri wake kwenye hiyo kesi na wote hatujasomea sheria na hatujui sana sharia, lakini juzi tumepeleka hoja ya kutokuwa na imani na Hakimu na Hakimu amejitoa temepangiwa Hakimu mwingine.
Wewe ni kijana wa mbogamboga siyo?? Punguza mbwembwe...
 
Kwa nini serikali imepeleka hati mbovu ya mashtaka?
Ndiyo ujue kwamba hawa akina Kibatala, Lissu na kundi la wanasheria wa upinzani moto wa kuotea mbali kwa sababu kushinda kwao mahakamani na haya makesi yasiyoisha kumewanoa na kuwafanya very competent!!
 
Huyo jaji hakujiondoa.
Huyo jaji ALIKATALIWA
LET US KEEP THE RECORD STRAIGHT
That's right...

Kukataliwa hufuatiwa na tendo la kuondolewa kwa nguvu (ukikataa) au unapima sababu zilizotolewa na kisha unajiondoa mwenyewe kwa hiari...

Kwa hiyo, "kujiondoa" siyo tendo moja bali ni "mchakato" wenye step kadha wa kadha ili kukamilika kwa tendo hilo..
 
sawa tu na Gaidi ambaye yuko jela mwenyewe na wewe uko raha mustarehe nyumbani
POLENI
Hivi mnamaliza lini matanga ya Mwanachama wenu maarufu, Kada mtiifu Hamza Mohamed ambae kaacha pengo ambalo halitazibika.
Labda akili zako zitaanza kuuzoea msiba huu mkubwa na hatimae kuweza kutulia.

1631035459885.png
 
Tatizo sio hakimu kujiotoa, ni hati ya mashtaka.
Hatukulaumu kwa vile umesema haujasoma sheria, tunakulaumu kujitia kimbelembele na kumpa ushauri rafiki yako na hali ya kuwa unajijua kama wewe ni mbumbu.
Huyo rafiki kwa kutegemea ushauri wako hata kama hana kosa ataishia jela tu.
What's your point anyway? Kwamba ni kosa kumkataa Hakimu au Jaji kwasababu ni mimi na sahihi kwa Mbowe sio? Nyumbu kweli ni nyumbu!!!!
 
Sasa wote hamjui sheria na wewe ndo mshauri huoni kama ni bomu tu linasubiri kulipuka?
Hoja yangu hapo ni kuwa kumkataa Hakimu au Jaji sio big deal kama tu vijana twa Chadema tunavyotaka kuaminisha watu kuwa kwakuwa Mbowe kamkataa Jaji na Jaji akajitoa basi Mbowe au mawakili wake wamefanya jambo kuuuuuubwa!!! Kumbe hata sisi maamuma wa sheria tuliishafanyaGA!!! Kushinda au kushindwa, hayo ni matokeo!
 
Is not about vijana wa CHADEMA. It's about mtu yeyote ukiwemo wewe "mtu wa CCM" kujua na kuelewa inapotokea hivi ktk kesi yoyote kisheria inakuwa na maana gani...

Ni bahati mbaya sana kwako unayejinasibu kama Mwanasheria na mshauri wa kisheria unatoa argument inayonukia itikadi za kisiasa badala ya kutumia ufahamu wako wa sheria kuelimisha wasio na basics za kisheria...
Bahati mbaya umekomenti bila kusoma vizuri nimeandika nini. That's the problem of myopic thinking of Chadema Youth like you.
 
Kwa vijana wa Chadema, Jaji kujitoa kwenye kesi wanafikiri is a big deal, lakini kumbe ni jambo la kawaida kabisa. Nina rafiki yangu hapa Mwanza ana kesi na mimi ndie mshauri wake kwenye hiyo kesi na wote hatujasomea sheria na hatujui sana sharia, lakini juzi tumepeleka hoja ya kutokuwa na imani na Hakimu na Hakimu amejitoa temepangiwa Hakimu mwingine.
Kama Mshauri ni wewe basi Jamaa yako anaenda Kula Mvua za Kutosha
 
Back
Top Bottom