Jaji Elinaza Luvanda ajiondoa kuendesha kesi ya Mbowe na wenzake baada ya washtakiwa kudai hawana imani naye

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Baada ya Jaji Luvanda kutupa mapingamizi yote yaliyotolewa na Mawakili wanaomtetea Mbowe na wenzake, Mbowe amesimama na kumtaka Jaji Luvanda ajiondoe kuendesha kesi hiyo kwani ameonyesha upendeleo na taarifa zinasema ana maelekezo ya kupindisha sheria ili amfunge Mbowe na wenzake.

Jaji Luvanda amesema hati ya mashtaka ni batili amewashauri Mawakili wa serikali wakaibadilishe, Mawakili upande wa utetezi wamegoma wamemwambia kama hati ya mashtaka ni batili basi futa kesi Jaji akakataa ila amekubali kujiondoa kuendesha kesi.

====

Jaji Elinaza Luvanda wa Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa na aliyekuwa anaisikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi namba 16/2021 yenye mashtaka sita yakiwemo ya Ugaidi, amejitoa kusikikiza kesi hiyo.

Sababu ya kujitoa katika kesi hiyo ni kutokana na mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kuieleza mahakama hiyo kuwa yeye na washtakiwa wenzake watatu hawana imani na Jaji huyo katika kutenda haki dhidi ya kesi yao.

Kesi imehairishwa mpaka jaji mwingine atakapopatikana. Pia awali Jaji Elinaza Benjamin Luvanda alikataa kutoa uamuzi wake leo juu ya mapingamizi ya upande wa utetetezi mpaka atapopata hansard / kumbukumbu za majadiliano ya Bunge kuhusu sheria ya ugaidi.

Wote walikubaliana kuwa kesi hii ina masilahi mapana kwa umma wote waliopo ndani ya Mahakama na nje.

Hoja 3 za upande za upande wa utetezi zilikuwa zinashambulia madhaifu na kasoro ya hati ya mashtaka. Hoja ya kwanza ilikubaliwa na jaji wakati hoja ya pili ilikubaliwa kwa nusu yake na jaji wakati hoja ya tatu ya kutupiliwa mbali au kufutwa kesi, jaji aliikataa.

Na kwa msingi huo mtuhumiwa Freeman Mbowe kwa niaba ya wenzake akasimama na kusema hawana imani na Jaji Elinaza Benjamin Luvanda kuendelea kusikiliza kesi hiyo, na mheshimiwa Jaji E.B Luvanda akaafiki ombi hilo na kujiengua kusikiliza kesi hii.

Source : Mwananchi Digital

luvanda.jpg

UPDATE: Jaji Luvanda akubali
Jaji Elinaza Luvanda aliyekuwa anaisikiliza kesi ya Uhujumu Uchumi nyenye mashtaka 6 yakiwemo ya ugaidi, amejitoa kusikiliza kesi hiyo, sababu ya kujitoa kwake, ni kutokana na mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, Mhe. Freeman Mbowe na wenzake kuwa hawana imani na Jaji huyo.

Pia soma >
Mahakama ya Uhujumu Uchumi: Mvutano mkali kesi ya Mbowe na wenzake. Hatma ya kesi kujulikana Septemba 6
. "Jaji Mwenzangu Luvanda" Machozi ya samaki majini hayatakufikia wewe na kizazi chako mpaka cha nne, tekeleza maagizo
. CHADEMA tusimpe vitisho Jaji Luvanda, mpaka sasa hajapendelea pande yoyote. Kibatala na jopo lake walichemka
 
Baada ya Jaji Luvanda kutupa mapingamizi yote yaliyotolewa na Mawakili wanaomtetea Mbowe na wenzake, Mbowe amesimama na kumtaka Jaji Luvanda ajiondoe kuendesha kesi hiyo kwani ameonyesha upendeleo na taarifa zinasema ana maelekezo ya kupindisha sheria ili amfunge Mbowe na wenzake.
Taarifa zote za Jaji Luvanda tunazo, amekanyaga pabaya sana
 
Jaji asikubali upuuuzi na ushenzi huu wa Mawakili wa Mbowe na Mbowe mwenyewe.

Huko ni kumtusi Jaji na Mahakama,

Mbowe na mawakili wake hawana sababu ya msingi zaidi ya kutaka kumyumbisha Jaji, tuhuma wanazo zitoa dhidi ya Jaji ni za kipuuuzi na hazina uthibitisho wowote zaidi ya kudhania na kuhisia tu, hakuna hoja hapo, kwa hiyo anamtaka Jaji ambaye ni RAFIKI YAKE ili asikilize kesi yake.

kwa hiyo imefikia sasa Mtuhumiwa kuchagua Jaji wa kusikiliza kesi yake aisee! hata marekani hakuna kitu kama hicho.

ninacho sema Jaji angeweza kujitoa kama tuhuma zinazo tolewa na Mbowe zina uthibitisho la sivyo Jaji aendelee tu kungurumisha kesi.......asikubali kubabaishwa na hoja za kipuuzi na za kuokoteza na zenye lengo la kuchelewesha haki kutendeka.
 
Jaji asikubali upuuuzi na ushenzi huu wa Mawakili wa Mbowe na Mbowe mwenyewe.
Huko ni kumtusi Jaji na Mahakama,
Mbowe na mawakili wake hawana sababu ya msingi zaidi ya kutaka kumyumbisha Jaji, tuhuma wanazo zitoa dhidi ya Jaji ni za kipuuuzi na hazina uthibitisho wowote zaidi ya kudhania na kuhisia tu, hakuna hoja hapo, kwa hiyo anamtaka Jaji ambaye ni RAFIKI YAKE ili asikilize kesi yake.
Unataka tuweke ushahidi wa aliyoagizwa Luvanda hapa?
 
Jaji asikubali upuuuzi na ushenzi huu wa Mawakili wa Mbowe na Mbowe mwenyewe.
Huko ni kumtusi Jaji na Mahakama,
Mbowe na mawakili wake hawana sababu ya msingi zaidi ya kutaka kumyumbisha Jaji, tuhuma wanazo zitoa dhidi ya Jaji ni za kipuuuzi na hazina uthibitisho wowote zaidi ya kudhania na kuhisia tu, hakuna hoja hapo, kwa hiyo anamtaka Jaji ambaye ni RAFIKI YAKE ili asikilize kesi yake.

Sasa kama mtuhumiwa kasema wazi hana imani na wewe utalazimisha?? Kwani nchi hii haina majaji mengine?? Aibu ni yeye kulazimisha kuendesha hiyo kesi wakati amekataliwa.
 
Unataka tuweke ushahidi wa aliyoagizwa Luvanda hapa ?
Awasilishe mahakamani kama anao ushahidi juu ya hayo anayo mtuhumu nayo, sio kumchafua Jiji bila ushahidi.

Kama hakuna ushahidi Jaji aendelee.

Kibatala anazidi kumchimbia shimo bila yeye kujielewa maskini Mbowe!!!

Hoja ya kitoto kweli hiyo eti unamkataa Jaji?!! Tena unatoa tuhuma za kizushi na majungu ya kumchafua Jaji?

Halafu hao mawakili wanamfundisha ujinga kama huo!!
 
Back
Top Bottom