Ufafanuzi: Majina John Heche Vs Wegesa Suguta

Ufafanuzi: Majina John Heche Vs Wegesa Suguta

Nakubaliana na Mwita Maranya Wakurya wanakuwa na majina mengi,nakumbuka kuna jamaa tulisoma nao walikuwa na kesi kama hiyo (majina ya kilugha na majina ya dini)
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wanaJF,

Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.

Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.

Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.

Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.

Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.

Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.

Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.

Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.

John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.

Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.

Nawatakia jioni njema.


Mwita Maranya: Vipi yule John Heche Suguta ambaye kwa sasa anaitwa Manchare Suguta (Mwanasheria wa NEMC)? Alijiunga na JWTZ mwaka 2002 mwezi March tarehe 4 kwa mafunzo ya kijeshi nikiwa na maana kwamba alikuwa askari kamili mnamo tarehe 30.08.2012 baada ya kuhitimu mafunzo hayo na kula kiapo cha utii kule Kunduchi DSM. Baada ya hapo alipelekwa kikosi cha 42KJ Songea ambako alikaa kwa muda mrefu kidogo na kuacha jeshi kisha kuja chuo kikuu cha Tumaini DSM ambako alichukua shahada yake ya sheria. Kwa sasa ananichanganya sana kwani amebedili jina kutoka John Heche Suguta hadi kuwa Manchare Suguta. Huyu bwana hata Force number zake nadhani bado nazikumbuka.

Kama naongopa naomba Mwitamaranya anisahihishe na kama kuna mwenye ufafanuzi zaidi atujuze.

Peooooplesssss power
 
Ndugu wanaJF,

Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.

Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.

Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.

Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.

Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.

Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.

Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.

Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.

John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.

Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.

Nawatakia jioni njema.

Mwita...

Amakweli wa Kurya mna mambo... Vita ni Vita Mura!

Ili bidi nipitie upya tamko la Makamo Mwenyekiti wa BAVICHA Bi Juliana ili nijiridhishe kama alivyomtaja Mwenye Kiti Heche kama Suguta..alisea kama amefoji jina au alikuwa pia aki mua dress kwa jina lake jengine la Kikristo la William Suguta. Maana hii mijiguvu uliyoitumia sioni mantiki yake hasa Muktadha wa Tamko la Bi Juliana.

Vita ni Vita Mura!

Kikwebo.
 
Mwita Maranya: Vipi yule John Heche Suguta ambaye kwa sasa anaitwa Manchare Suguta (Mwanasheria wa NEMC)? Alijiunga na JWTZ mwaka 2002 mwezi March tarehe 4 kwa mafunzo ya kijeshi nikiwa na maana kwamba alikuwa askari kamili mnamo tarehe 30.08.2002 baada ya kuhitimu mafunzo hayo na kula kiapo cha utii kule Kunduchi DSM. Baada ya hapo alipelekwa kikosi cha 42KJ Songea ambako alikaa kwa muda mrefu kidogo na kuacha jeshi kisha kuja chuo kikuu cha Tumaini DSM ambako alichukua shahada yake ya sheria. Kwa sasa ananichanganya sana kwani amebedili jina kutoka John Heche Suguta hadi kuwa Manchare Suguta. Huyu bwana hata Force number zake nadhani bado nazikumbuka.

Kama naongopa naomba Mwitamaranya anisahihishe na kama kuna mwenye ufafanuzi zaidi atujuze.

Peooooplesssss power

Mwita Maranya: Vipi yule John Heche Suguta ambaye kwa sasa anaitwa Manchare Suguta (Mwanasheria wa NEMC)? Alijiunga na JWTZ mwaka 2002 mwezi March tarehe 4 kwa mafunzo ya kijeshi nikiwa na maana kwamba alikuwa askari kamili mnamo tarehe 30.08.2002 baada ya kuhitimu mafunzo hayo na kula kiapo cha utii kule Kunduchi DSM. Baada ya hapo alipelekwa kikosi cha 42KJ Songea ambako alikaa kwa muda mrefu kidogo na kuacha jeshi kisha kuja chuo kikuu cha Tumaini DSM ambako alichukua shahada yake ya sheria. Kwa sasa ananichanganya sana kwani amebedili jina kutoka John Heche Suguta hadi kuwa Manchare Suguta. Huyu bwana hata Force number zake nadhani bado nazikumbuka.

Kama naongopa naomba Mwitamaranya anisahihishe na kama kuna mwenye ufafanuzi zaidi atujuze.

Peooooplesssss power
 
Ndugu wanaJF,

Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.

Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.

Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.

Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.

Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.

Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.

Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.

Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.

John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.

Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.

Nawatakia jioni njema.

Kama ningefananisha hili swala la soka basi you are the man of the match! mkuu umemaliza kila kitu tuendelee kujenga chama acha masalia waendelee kugugumia maumivu!
 
Mwita Maranya: Vipi yule John Heche Suguta ambaye kwa sasa anaitwa Manchare Suguta (Mwanasheria wa NEMC)? Alijiunga na JWTZ mwaka 2002 mwezi March tarehe 4 kwa mafunzo ya kijeshi nikiwa na maana kwamba alikuwa askari kamili mnamo tarehe 30.08.2012 baada ya kuhitimu mafunzo hayo na kula kiapo cha utii kule Kunduchi DSM. Baada ya hapo alipelekwa kikosi cha 42KJ Songea ambako alikaa kwa muda mrefu kidogo na kuacha jeshi kisha kuja chuo kikuu cha Tumaini DSM ambako alichukua shahada yake ya sheria. Kwa sasa ananichanganya sana kwani amebedili jina kutoka John Heche Suguta hadi kuwa Manchare Suguta. Huyu bwana hata Force number zake nadhani bado nazikumbuka.

Kama naongopa naomba Mwitamaranya anisahihishe na kama kuna mwenye ufafanuzi zaidi atujuze.

Peooooplesssss power
Discuss issues not personalities, hata ukishamjua itasaidia nini hapa JF?
 
kwanini asitumie jina lake lile moja??? huu ni usanii na unapaswa kuhojiwa
 
Kwani we mwita ni nan ake wegesa, kwanin yy aloiba majina asije hapa kufafanua? Mwaka wenu huu kwakweli.
peleka utupu wako huko kwani ninini ambacho hukielewi hapo?ungekuwa uko TARIME kwa wanaume tungekutahiri!
 
Jamani kwenye mkoa wetu wa Mara mtu kuwa na majina zaidi ya mawili ni kitu cha kawaida hata mimi nipo kwenye huo mlolongo kwa maana nina majina mawili official na moja la utani ambalo ndilo limenikuza mpaka hapa nilipo.
Kwa bwana Heche kuwa na hayo majina yote ni possible kabisa swali ni kwamba ana yatumiaje? Mimi jina langu la shule ni tofauti kabisa na jina la nyumbani
 
Huyu bundi wa CHADEMA si mchezo....

yan mkuu ni mtihani kweli, majina nayo yamekuwa issue. had yazua mjadala hivyo. hivyo hakuna mambo ya muhimu ya kujadili kuhusu maendeleo ya chama hadi kufikia hatua ya kujua majina ya watu kweli. 2015 kuna kazi kwelikweli
 
Mkuu Osokoni Kuna issue hapa?

Mkuu we kama una Detail za hii kitu mwaga tu humu ndani,wala hkuna haja ya kutegeshea,kama hujajua picha inayoendelea katika hili utaumia sana,na ukiendelea sana utajikuta unakula kitu!!!!!!!
 
Niliposoma tu ile makala ya utetezi ya Bi Juliana Shoza huku nikijua ni msomi wa chuo kikuu nilihisi haraka sana ile kitu ya majina tofauti ya John Heche imepikwa, kama ilikua na ukweli wowote, mwandishi au mtoa shutuma akiwa ni msomi, nilitegemea angeonesha pia wapi huyu bwana ali Cook hayo majina, hadi mwisho wa makala yake sikuona then nikajua aidha hana ushahidi au kafanya makusudi kuposha jamii au alifanya vile ili John Heche mwenyewe aje ajibu na waanze kukosoa kwakusema ni wapi tulipokutumuhu kwamba unatumia jina la mtu? Bahati mbaya mtego wake umeferi vibaya tena, RIP kisiasa bi Juliana.
Ndugu sijakusoma vizuri tatizo lako,Kuna ubaya gan bi Shonza kumtaja ndugu heche kwa jina lake la asili
 
Ndugu wanaJF,


Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.

Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.

Nadhani umtu wake wa karibu sana, ungetusaidia vyeti vyake kuanzia cheti cha ubatizo, mpaka chuo kikuu tuangalie mtiririko wa majina, vinginevyo nawe ni wale wale wanaongea tu bila ushahidi
 
hapa CDM tunakaba mpka penalt so masalia yatafute means nyingine labda nje ya uwanja.
 
Back
Top Bottom