Mwambomboli
Member
- Dec 25, 2012
- 46
- 7
Fita ni fita mura!Wanareta majungu afasari umewajibu.
Mkuu kuna ubaya mie kuuliza iko swali nataka kujua kama kuna majina ya kikristo.
Ndugu wanaJF,
Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.
Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.
Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.
Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.
Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.
Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.
Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.
Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.
John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.
Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.
Nawatakia jioni njema.
mbona mnajibu vitu vdogo na kuacha mambo makubwa yaliyohojiwa na Shonza?
hebu tupeni ufafanuzi juu ya vifungu alivyolalamikia Shonza kwamba vmekiukwa! hebu tuambieni vigezo vilivyotumika kumwadhibu Shonza na kumuacha Mamuya wakati wote hawakuhudhuria kikao, hebu tuambieni juu ya mshahara wa Heche na kwann kodi ya nyumba yake inatoka kwa katibu mkuu?
hebu tufafanulieni juu ya gari la BAVICHA na dreva wake.
CHHADEMA acheni kujibu hoja nyepesi na zisizohitaji kujibiwa wakat kuna hoja znahtaj majibu yenu na hapo sijawauliza kwann hamjamfukuza Zitto kwa sababu najua Zitto sio BAVICHA!
Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.
.
Unahitaji ufafanuzi gani tena? si ulisha sema Ukuryani majina huwa hata wanawake wanaitwa majina ya Wanaume? kwani kosa liko wapi? na ni kweli kuna wanaume wanaitwa Ghati,Bhoke na kuna wanawake wanaitwa Mwita na lazailaka na haya majina yana maana yake si kwamba wanao wapa hayo majina hawajui maana ya kuwaita hayo majina na kikubwa sana si dhani kama inakuhusu au ndo muendelezo wa Thread? Ufafanuzi ulisha tolewa wewe unataka tena jina la Wegesa, hivi inamuhimu kwa msatakabari wa Nchi? watu tumekaria majungu mwanzo mwisho, ni majungu asubuhi hadi UsikuMkuu Mwita Maranya najua ukuryani kuna majina ya kike na kiume. Pia nafahamu kwamba kuna mazingira fulani unaweza kukuta mtu mwanmume anaitwa jina la kike kama vile Bhoke Munanka (Lazima kuwe na sababu maalum). Hapa naona John anaitwa Wegesa ambalo ni jina la kike. Imekaaje hii?
Yapo tena mengi,kwa mfano nina ndugu yangu anaitwa kokubanza james kiiza lakini baada ya kubatizwa akaitwa Priscillah James Kiiza kwa hiyo hapa jina Priscillah ni la kikristu je una la ziada dada?
Ndugu wanaJF,
Nimelazimika kuanzisha thread hii kwa lengo moja tu la kutoa ufafanuzi juu ya upotoshwaji wa jina la mwenyekiti wa baraza la vijana Chadema unaofanywa na kundi la masalia kwa sababu maalum.
Mwishoni mwa mwaka jana TUNTEMEKE aliwahi kuibuka na madai kama haya kwamba John Heche anatumia cheti cha ndugu yake, na kwamba hakuwahi kusoma chuo kikuu cha mtakatifu augustino (SAUT) cha mwanza. Leo tena katika thread iliyoanzishwa na mwanamasalia aliyetimuliwa Chadema bi. Juliana Shonza amejitahidi sana kutumia jina la Wegesa Charles Suguta ama Wegesa Suguta.
Bila shaka ameamua kufanya hivyo kama muendelezo wa tuhuma walizozianzisha kundi la masalia kwa kutumia ID yao ya kundi ya Tuntemeke kama nilivyoeleza hapo mwanzo. Hili kundi la PM7 linataka kumuonyesha John Heche kwamba naye amegushi jina kama walivyo baadhi ya viongozi wakubwa huko ccm (wafadhili wao). Mathalani imetajwa mara kadhaa kwamba miongoni mwa watu wanaotumia majina ya kugushi huko ccm ni pamoja na Naibu katibu mkuu bara Bw. Mwigulu Nchemba (Lameck Madelu?) na Dr. HKigwangalla (Saidi Bagaile?) ambao wanadaiwa kutumia majina ya bandia.
Sasa nirudi kwenye hoja ya msingi. Kawaida sisi wakurya hata kama umezaliwa mjini ama katika mazingira ya mbali na nyumbani/kijijini lazima unapewa jina la kikurya, kwahiyo kwa wakurya wengi wanakuwa na majina mawili ama matatu lakini yote yakiwa ya mtu mmoja.
Kwa mfano mwalimu Nyerere, majina yake ni Julius Kambarage Nyerere(Julius jina la kikristo). Kuna mwanae Charles Makongoro Nyerere (Charles jina la kikristo), kuna Dr. James Mnanka Wanyancha-mwenyekiti wa Road Fund (James jina la kikristo), Marehemu Jenerali Ernest Mwita Kyaro (Ernest jina la kikristo), Jenerali mstaafu George Marwa Waitara (George jina la kikristo. Nadhani kwa kutaja hao wachache mnaweza kuona scenario ya majina ya kikurya, naamini kuna makabila mengine yenye utamaduni kama wa kwetu.
Sasa nije kwa John Heche Suguta:
Jina lake la kikurya ni Wegesa na baba yake mzazi anaitwa Heche Suguta. Wegesa Heche Suguta jina lake la kikristo ni John, ndipo sasa unapata John Heche Suguta. Jina la kikristo la baba yake John Heche (Heche Suguta) ni Charles, ndipo sasa unapata Charles Heche Suguta.
Katika vyeti vyake vya shule John Heche anatumia jina la Wegesa Charles Suguta (Wegesa Suguta). Aliandikishwa shule kwa jina la Kikurya na akaendelea kulitumia katika harakati zake zote za kishule. Ndugu zake na John Heche ni pamoja na Bw.Manchare Heche Suguta (Mwanasheria NEMC), Chacha Heche Suguta (M/Kiti Bavicha Tarime) na Mome Heche Suguta (Tarime) kwa kutaja wachache ambao angalau wanafahamika na watu wengi.
Nimalizie kwa kuwajulisha masalia kwamba kama mnadhani mnaweza kumchafua Bw. John Heche kwa staili ya majina basi nawashauri msahau kwakuwa watu wote waliokua nae toka utotoni Tarime, shuleni alikosoma sekondari ya Bulima (O level), Musoma Alliance (A level), Bunda TTC na hatimaye SAUT Mwanza wanamfahamu sana John Heche kwa majina yote mawili.
John Heche aligombea na kushinda kiti cha udiwani Tarime mjini mwaka 2008 katika uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Chacha Wangwe, kwa kumshinda mbabe wa Tarime Bw. Peter Zakaria. Wakati huo alikuwa mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu augustino (SAUT) Mwanza. Kama angelikuwa anatumia majina ya bandia ama majina ya mtu mwingine bila shaka hilo lisingejificha wakati wa kampeni za uchaguzi.
Baada ya kusema hayo nadhani nime-clear doubts zilizokuwa zimeanza kujitokeza kwa baadhi ya watu hapa JF.
Nawatakia jioni njema.
Mtoa mada ameelezea majina ya kikuria kirahisi rahisi mno na maelezo hayo hayawezi kusimama mbale ya sheria.Kisheria mtu anakuwa na majina matatu ambayo hayatambui dini ya mtu bali majina hayo.Sasa mheshimiwa Mwita Maranya katoa ufafanuzi wa jinsi Wakuria wanvyokuwa na parallel names ambazo kisheria ni aliases.Kwa hiyo tuhuma zilizopo haziwezi kuelezwa kirahisi hivyo.
Mkuu Mwita Maranya najua ukuryani kuna majina ya kike na kiume. Pia nafahamu kwamba kuna mazingira fulani unaweza kukuta mtu mwanmume anaitwa jina la kike kama vile Bhoke Munanka (Lazima kuwe na sababu maalum). Hapa naona John anaitwa Wegesa ambalo ni jina la kike. Imekaaje hii?
Kweli siku yako haijafika. Hujui asili na utaratibu wa majina ya kikurya usipotoshe bora uulize usaidiwe.
Kuna wanawake wanaitwa Marwa, Chacha ama Mwita ambayo ni majina ya asili ya kiume na kuna wanaume wanaitwa Bhoke, Ghati ama Rhobi ambayo ni majina ya asili ya kike.
Kuna majina kama Wegesa, Matinde, Nyamhanga, Nyangi, Mogesi n.k ambayo yanatumika na jinsia zote kutokana na sababu maalum wazazi wanaamua kumpa mtoto jina fulani.
Mathalani bibi yake na baba yangu anaitwa Mogesi lakini sasahivi familia yetu inawapa jina hilo watoto wa kiume kutokana na familia kuamua hivyo kama kumuenzi.
Unahitaji ufafanuzi gani tena? si ulisha sema Ukuryani majina huwa hata wanawake wanaitwa majina ya Wanaume? kwani kosa liko wapi? na ni kweli kuna wanaume wanaitwa Ghati,Bhoke na kuna wanawake wanaitwa Mwita na lazailaka na haya majina yana maana yake si kwamba wanao wapa hayo majina hawajui maana ya kuwaita hayo majina na kikubwa sana si dhani kama inakuhusu au ndo muendelezo wa Thread? Ufafanuzi ulisha tolewa wewe unataka tena jina la Wegesa, hivi inamuhimu kwa msatakabari wa Nchi? watu tumekaria majungu mwanzo mwisho, ni majungu asubuhi hadi Usiku
Mkuu kuna ubaya mie kuuliza iko swali nataka kujua kama kuna majina ya kikristo.
Hawa jamaa ni ndugu john pamoja na wegesa. Nakumbuka nilisoma nao bulima sec iliyopo magu na walikuwa wamenitangulia mwaka mmoja