Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.

Yeah, kuhani nadhani umemaliza mjadala huu.
Mod tafadhali peleka hii thread kule inapotakiwa
 


RAIS WA KWANZA KUHUTUBIA AU KWA KISWAHILI ALIKUWA JOACHIM CHISANO..alipokuwa rais wa mozambique....kikwete has just follow steps za wengine wanaaooongea kiswahili pale...hakuna la ajabu hapo!!!

kama ni nabii basi ni KIBWETERE!!!
 
Hizi ni chuki za muendelezo sijui kwa vile jaji kiongozi Jundu kachaguliwa?jana Rais Kikwete kamchagua Jaji mkristu Catherine hadi sasa sijaona shutuma za udini.

pia amewachagua Jaji mstaafu Samatta kuwa mkuu wa chuo cha Mzumbe, na balozi mstafuu mkristu kuwa mwenyekiti wa SUA.David Mattaka na ngereja sio waislam.

hakuna maoni ya kusema kuna udini ila kwa hili la Fakihi Jundu limekuwa gumzo la mji.
naomba kuuliza hivi karibuni JK kachagua makatibu wakuu na makatibu wakuu wasaidizi kina Kamuhanda wamefanywa kuwa manaibu katibu wakuu wa wizara ya mambo ya nje. wote waliochaguliwa ni wakristu.

wakuu wa wilaya waliochaguliwa na Kikwete asilimia 80% ni wakristu jaribuni kufanya utafiti, mawaziri bado wengi ni wakristu,waziri mkuu Pinda alipokuwa waziri wa Tamisemi watendaji wake zaidi ya 140 aliowachagua ni wakristu kwa asilimia 90.

Mimi naomba tutizame teuzi za JK kuanzia mawaziri,makatibu wakuu, wakuu wa mikoa tuone dini gani wengi, tukijua hilo ndio tulaumu kama mdini au laa.

michango kama hii nia yake kumvunja nguvu JK na kujaribu kumtisha kuwa wenye nchi ni dini fulani Tanzania, very unfortunate hao wanaolilia kuwa watawala kwenye mapambano ya uhuru hawakuwa na mchango mkubwa kama walivyofanya waislam kwa kujitolea kila walichonacho.

Nauliza swali kama Marehemu Ramadhani Kihiyo alivuliwa ubunge kwa kuwa na cheti tu kilichodaiwa kuwa ni feki, vipi Nchimbi,Kamala, Mary Nagu, Mahanga, Chegeni, Lukuvi, Diallo,Mathayo David ambao imethibitika wana PhD feki na digrii wanaendelea kushika nyadhifa hizo? kama wangekuwa waislam tungelala?ikiwa Kihiyo alikuwa na certificate tu dunia nzima iliambiwa,hawa wateule kwa vile ni watu wa kanisa wanamezewa.
 
Kuhani,
You'd make a damn good defense lawyer. I can imagine the prosecutors making sure they got their facts right when it is known the Honorable Kuhani is the defense lawyer in this case.
 
Tatizo la kuchagua kiongozi asiye na mwelekeo, uelewa , wala kujua nini la kufanya hata katika maisha yake mwenyewe ni hili tulionalo kwa rais kikwete.

...mpaka kufikia u-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaonyesha anajua nini anachokifanya kwenye maisha yake.

Ndugu huyu anaonyesha udini bila soni, mbaguzi , mkumbatia wezi, hana maadili (hata ya ndoa tu) na zaidi hana uwezo wa kuongoza.

...ni mfumo tu wa uongozi kuzingatia na utawala wa kisheria, unless uchambue hapa kwa kina udini wake, ubaguzi wake, na ubovu wa uongozi wake kutokana na mifumo unayoielewa ya uongozi.

Ndiyo maana amekuwa akijaza waislamu kwenye uteuzi wa nafasi zote muhimu.

...sijui hapa unatafuta supporters au sympathizers? i cannot comment further.


...kwakuwa kachaguliwa kidemokrasia, na mwaka 2010 mwendo mdundo...

Ngeleja anataka kuiba palepale ambapo lowassa na karamagi wameiba na bila aibu anatuona wajinga. Rais naye anaangalia.

...Ngeleja anatakaje kuiba?

Ingekuwa mtu anamwibia kimada kweli angekaa kimya hivi nchi akibakwa? Anakaa kimya kwa vile yeye haelewi. Anafikiri yeye ni mcheza filamu wakati yeye ni rais. Mungu wangu!!!!

...ushamhukumu hapo haelewi, starring hauwawi ndugu yangu...

Na zitto kabwe amekuwa mpumbavu. Kisha lipiwa yule!

...unamuonea, kama una ushahidi amekuwa mpumbavu na kisha lipiwa, leta hapa jamvini!

Ni kwavile watanzania wajinga mno

...Loh! hilo la kutuhukumu Watanzania ni wajinga, hapana mimi sikubaliani nalo. Umetumia kigezo gani?

...mimi nakataa kwasababu; alishinda kwa 80% ya kura 11.3 million zilizopigwa, wakati idadi ya Watanzania ni zaidi ya millioni 36. Nami ni mmoja katika hao ambao hawakumpigia kura...
 
Kuhani,
You'd make a damn good defense lawyer. I can imagine the prosecutors making sure they got their facts right when it is known the Honorable Kuhani is the defense lawyer in this case.

"You would make..."? How do you know I haven't made? Measure your statements!

Jasusi, tukiacha utani, mimi mwenyewe sio Muislam wala Mkristo, in fact sijui, sidhani, kama kuna Mungu!

Ila naona Wakristo mme panick kuona Kikwete anachagua Waislam katika rate ambayo labda ni ya kasi kupita mlivyozoea. Lakini Jajusi, unless imefikia mahala Wakristo sasa wamekuwa underrepresented hamuwezi mkaanza kulalamika. Mtakuwa mnamuonea Kikwete.

Halafu inawezekana Kikwete, maskini ya Mungu, alipanga kwamba moja ya mission yake atakapokuwa Rais ni kusawazisha hiyo imbalance iliyokuwepo, kwa maana kwamba aliona Marais wa nyuma yake hawakutilia mkazo hilo swala, au labda kwa kweli kulikuwa hakuna Waislam wengi sana waliokuwa na sifa kutokana na sababu za kihistoria. Kwa hiyo mimi nadhani Jasusi, Wakristo mmekuwa na undue trepidation hapo.

After all, listen to this, Jasusi, inawezekana Kikwete is doing us all a favor. Na hili nitalisema bila kuogopa: Labda Kikwete anajua, na mimi ndivyo ninavyo amini, kwamba ndugu zake Waislam wanaweza kuwa wepesi kulipuka kudai haki zao wakihisi wanaonewa (angalia hata Mufti Mkuu ilibidi awasihi Waislamu wenzake wakati wa ujio wa Bush kwamba wasilete mushkeli kwa mgeni). Kwa hiyo Kikwete anataka kuondoa mzizi wa fitina kutuepushia wote majanga. Ni sawa na Marekani sasa hivi ni vigumu sana kwa weusi kusema wanaonewa, wanaishi kwenye ma ghetto, well ma mayor wote kwenye miji ya ma ghetto weusi! Sasa who is responsible for you not building better communities? Na sasa Rais wao Mweusi, Wazungu wajanja, wametukata ngebe.

Halafu Jasusi, lingine ambalo namsifu Kikwete, in fact hapa kamzidi hata Nyerere, ni kwamba yeye haogopi kuweka watu wa mbali sehemu nyeti.

Nyerere alikuwa sehemu nyeti amezungukwa na ma cousins, kina Butiku, Musuguri, Bhoke Munanka, Charles Nyirabu, Joseph Nyerere, Joseph Warioba, Adam Marwa, to say nothing of mafisadi wa kwao ambao hawakufungwa, wale wa GAPEX etc etc. Na kabla hajakimbia, Nyerere akamsimika Warioba, akam ram Warioba down Mwinyi's throat! Kikwete kaweka kina Philemon Luhanjo pale Ikulu, Mwamunyange jeshini, Pinda, Jaji Mkuu Augustino Ramadhani (Mkristo) etc. etc. total strangers kwa standard za Marais wa Kiafrika katika watu wa karibu. Mimi kwa kweli, Jasusi, simlaumu sana Kikwete kujali ku address hizi historical imbalances za udini.
 
Kihiyo hakuvuliwa ubunge kwa sababu ya Uislamu wake, bali alifoji cheti cha taaluma. Ni kosa la jinai na alistahili aende jela.
Hao wote uliowataja wana Ph.D feki, sio kwa forgery bali vyo waliposoma, havitambuliki. Hivyo hawajafoji vyeti, bali wana vyeti halali ila havitambuliki. Kutokuwa na Ph.D sio sifa ya uongozi.

Kujiita Dr. Kwa Tanzania sio kosa la jinai, tuna Prof. Maji Marefu, Prof. Matikisa, Prof. Singili. Tuna ma Dr. Kibao,
Dr. Kifimbo, Dr. Isaack Ndodi, Dr. Hawa Nyamichwo, Dr. Tamba na kuendelea.

Hoja ya uswahiba na udini, haina nguvu, issue ni Wakristu walishika nafasi muhimu kwa muda mrefu, akitoka Mkristu akaingia Muislamu basi ndio inakuwa nongwa.Wakristu wakiendelea kupewa ulaji hilo halionekani.

Kwa mijibu wa katiba ya nchi, madaraka ya rais kuteua ni exclusiwe at his pleasure hata akiamua kuteua waliokuwa
Vimada wake, marafiki zake, wanamsondo, wazee wa Saigoni na kuendelea, bado hakuna kosa lolote.

Issue jee hao walioteuliwa wote wana uwezo wa nafasi walizoteuliwa nazo, hili ni udhaifu wa mtu na mtu.
 
Miye haya ya uislamu na ukristo naona yanatubagua tu Watanzania. Mimi nataka viongozi ambao ni wachapa kazi na ambao siku zote wataweka mbele maslahi ya Watanzania badala ya wao wenyewe, siyo woga watakuwa tayari kupambana na mafisadi bila woga wala kificho. Hawa ndiyo viongozi ninaowataka katika Tanzania yetu. Kiongozi akivurunda sitaogopa kusema kwamba amevurunda bila kujali dini yake. Tusipoangalia Waislamu wataanza kusema hao wanamkosoa Kikwete kila kukicha ni Wakristo maana wanataka kumuingiza Mkristo mwenzao, kitu ambacho hakina ukweli wowote.
 
Pasco.
Nchimbi lini alikwenda kusoma?Mrema alikwenda lini kusoma? Nagu lini alikwenda kusoma? hakuna chuo kikuu UK alichosoma Kamalla na Nchimbi ni utapeli. kama wanajua shahada walizonazo si sahihi kwanini waendelee kuzitumia?ni kosa la jinai kuwakilisha shahada za uongo.kama wao ni wakweli waseme hadharani kuwa walidanganywa.

Kuhani.
Umesahau nyerere aliweka ndugu zake kama Msuguri MKUU wa jeshi,Charles Nyirabu kuwa gavana wa benki kuu wakiwa jamaa zake.kwa safu ya watendaji wa kikwete uliyoweka kama kina LUHANJO,PINDA,MEMBE,ETC ni dhahiri si mdini ila Mkapa ndio mdini alikuwa na wasaidizi wa karibu wa kikristu kama Sumaye,Malecela,Mangula,Apson,Maokola majogo na wizara zote nyeti kuwapa wakristu kama kina Mramba na Yona licha ya utendaji wao mbovu.

Nimewahi kusoma mahala sijui hapa JF au Blog nyingine kuwa watendaji wa kiislam ni waadilifu mfano DR.Shein,Marehemu DR.Omar Juma,DR.Salim Ahmed Salim,Mzee Kawawa.kulinganisha na watendaji wa kikristu kama Lowassa,SUMAYE,Mkapa,Yona etc.
 
Hapa wandugu tutofautishe hoja mbili! Moja ya Uswahiba na ingine ya Udini!

1. Kwa udini ni ukweli kuwa JK ameongeza kasi ktk uteuzi wa waislam ngazi za juu..hata hivyo bado kwa Tz itachukua mda mrefu to address such historical imbalances: yaani kuna sehemu za elimu ya juu au utafiti Tz over 80% wa wafanyakazi ni Wakristo yet statistics zinaonyesha makundi haya hayapishani sana kwa idadi! Kama ni watz wanaqualify hata kama mimi ningekuwa JK ningechukua affirmative action kuwapa nafasi pia waislamu..kwa kuwa wapo wanaqualify kwa sasa!

2. Uswahiba. Hili kweli limekuwa taabu. na wengi kwa kutumia influence huenda kumlilia ili wapate nafasi za watu wao kuajiriwa. Hebu angalia Mtoto wa Mongela kuwa DC Kigoma...je huyu mtoto alikuwa na uzoefu gani? Haya yote yanatokea baada ya mke wa huyu mtoto kuchukuliwa na waziri wa JK..Karamagi! Ndo maana kuna haja ya kuangalia jinsi ya kuzuia malobists kuinfuence maamuzi yake kama alivyosema Obama na uraisi wake ktk White House! Watu wanaomlilia shida ili kupewa favour ni wengi mno! Na huu ni aina ya uswahiba ambao wengi wanaupiga vita!

3. Kuna haja kuwa na Vetting ili kuchekecha viongozi wabovu wanoteuliwa kabla ya kuapishwa! Tungekuwa na Vetting system nzuri ya Kamati ya Bunge Mattaka asingepita MD ATCL!

Sasa kwa vile hatuna Vetting..ndo maana saa ingine huweza kuteua hata maswahiba wake tu wasio na uwezo au wenye rekodi mbaya!
 
hii mijadala ya dini na ukabila haitatusaidia ndugu zangu.tukiiendekeza haitatupeleka popote zaidi ya kutufarakanisha kama taifa na mwisho wa siku hao mnaowatetea wataendelea kula kuku na hata kutokomea nje ya nchi mambo yatakapokuwa siyo mazuri na kuwaacha wenzangu na mimi wasioweza hata kumudu milo mitatu kwa siku wakichinjana.
tukumbuke kuwa siku zote mambo ya imani yana nguvu sana.mtu hata kama haendi kanisani/msikitini lakini ukitaja imani yake ndivyo sivyo hamuwezi kuelewana.ndiyo mana mijadala yote ya hawa viongozi wetu ikishajikita kwenye dini basi wengi watachagua sides kulingana na imani zao.
nadhani tulilie teuzi za watu wenye sifa wawe waislam,wakristu ama wapagani.hii ndiyo iwe hoja na si dini wala kabila.
 
Kuhani,
Asalaam aleikum, Bwana asifiwe...Umemaliza!

Aleikum Salam Warahmatullah Taala Wabarakatuh. Alhamdulillah Rabil Allamin, Wasallatu Wasalam Ala Sayidina Muhammad, Salallahu Alaihi Wasalam.

Na mtu wa kwao, nabii wao mwenyewe, amesema: Watanzania ni waongo siku zote, hayawani wabaya, walafi, wavivu. Ushuhuda huu ni wa kweli. Kwa sababu hiyo wakemee kwa ukali ili wapate kuwa wazima katika imani, wasisikilize hadithi za Kifisadi. Waraka wa Paulo Mtume kwa Tito 1:12-14, adapted.
 

Hizi shughuli kumbe unaziweza unaweza kuchagua kokote kule na ukafit bila matatizo yoyote.
 
Waafrika na hasa watz na starehe hapo hatutoki ila kwa namna yoyote visababu havikosi.
Tutaishia huko huko enzi za mababu kila msimu na party. Mtoto kabarehe party, kaenda jando party.
Haya ganesh endeleeni na party zenu tuone kama nchi mtaitoa.
Wenzenu wanatafuta namna ya kupunguza kodi kwa mwananchi nyie mnatafuta namna ya kumkamua zaidi mwananchi. Haya!
 
Nimewahi kusoma mahala sijui hapa JF au Blog nyingine kuwa watendaji wa kiislam ni waadilifu mfano DR.Shein,Marehemu DR.Omar Juma,DR.Salim Ahmed Salim,Mzee Kawawa.kulinganisha na watendaji wa kikristu kama Lowassa,SUMAYE,Mkapa,Yona etc.

Ukiwa biased kaaazi kweli kweli. Pole sana ndg, wewe ni mdini na posts zako zinachekesha ila hujui tu.

Kwenye hiyo list ya wasilamu waadilifu mbona hujamalizia first XI kwa kuwaweka Nazir Mustafa Karamagi, Msabaha, Rostam Azziz na wengieneo?
 
Ndugu yangu Kandambili, hao unaowasema wamepata vyeti vyao toka On-line Courses ambazo hazitambuliwi. Misingi ya teuzi zao sio hizo, Ph.D zao. Bado wangeula tuu hata bila ya hizo shule famba zao. Siungi mkono jambo hilo lakini tofautisha na kufoji. Wewe unaweza anzisha Chuo Kikuu cha Kandambili on line, na ukatoa Ph.D zako kwa wiki moja mtu anapata. Watu wakaomba pesa wakalipa na wewe ukawapa hizo Ph.Ds jee wamefoji?. Kupata degree ni issue nyingine na kutambuliwa ni issue nyingine. By the way, what has this have to do with udini?
Au kwa vile hao wenye Ph.D fake wote ni Wakristo?.
It has nothing to do with dini, hizo ni individual issues.
 
Kama wote ni wakristo, au kama wote ni waislamu au wenye dini ya kisanii kama ya Mzee Kingunge, haisaidii kitu. Kazi yao sio kueneza dini, ni kuongoza nchi. Kama wote ni wasialmu na wanaweza kuzuia mauaji ya Albino, kuwaadhibu wezi wa EPA na Richmond kuna ubaya gani? Kama ni wakristo wote na wanaweza kuondoa matatizo ya wananchi kuna ubaya gani?
 
CCM msikimbie kwa kuleta visingizio vya udini hapa JF ,najua mmebanwa kila kona na mnazidi kupelekwa pembeni na kuwekwa kwenye kona ili msulubiwe ,hivyo hizi danadana za kuleta hapa Jf ili watu wacheze na kupiga danadana hilo ,naamini haliwezi kupewa nafasi kabisa ,na wale watu ambao wapo mstari wa mbele wasikubali kuingia katika mtego huo unaonyemeleshwa hapa JF ,kama mnavyojua JF ni kiungo muhimu katika siasa za ndani za Tanzania ,hususani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, mbinu iliyopo hapa ni kuwapindisha wananchi wazidi kuelekekea na kutumbukia katika shimo la maafa ya CCM , hizi ni mbinu ambazo zinataka kuwapindisha wananchi ,ukiangalia hoja ya udini haina nguvu kwani karibuni wabunge wote wa Tanganyika ni wakiristo halikadhalika Mawaziri ,sasa mkitaka kujua wanaoharibu nchi na kuwapa nguvu wale walioko juu ni wabunge ,wawe waisilamu au wa kiristo au wasio fungamana na upoande mwengine ,ni wabunge tu kwani wao ndio wanaokubali au kukataa muswaada na kitu chochote kile kinachopita kutumika na serikali iwe sheria au manunuzi ya juu yanayohusisha matumizi makubwa ya fedha ambayo hupatikana katika bajeti.

Muhimu ni kubadilisha nguvu za wabunge hapo Bungeni ,ni lazima nguvu za CCM zikatwe miguu na mikono wabakishiwe mkia tu ,Hata nguvu ya Raisi ipo kwenye ubunge ,leo kama Kikwete asingekuwa na wabunge wengi pale bungeni angelikuwa matatani ,lakini anachoringia ni wingi wa wabunge wa Chama chake ,ndio inakuwa hata hana wasi wasi.

CCM ivunjwe nguvu kwa kuwapunguza wabunge na ikiwezekana asilimia 75 ya viti vya ubunge vichukuliwe na upinzani ,je wapinzani wataweza kupata asilimia hiyo? Kivipi ?

Inawezekana kabisa mbona Pemba waliweza ,Pemba walichukua asilimia mia moja ya viti vya ubunge ,hivyo uwezo upo kabisa nao ni kupambana na CCM kwa kila Pembe na kutokubali kwa wananchi kuondoka sehemu zao za kura ,vilevile kupata watu ambao ni wasimamizi wa ndani wa Uchaguzi wasiokubali kudanganywa ,ndipo tukasema tume huru ni kitu cha lazima kabla ya Uchaguzi.

haya mambo ya udini ukabila hayana msingi kabisa wala hayahusiani na mfumo wa vyama vingi,huo ni mfumo wa chama kimoja tu katika kuongoza serikali,kwa ufupi kama mnasema CCM ina udini basi dawa ya kuondoa ni kuwaweka kando.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…