Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
1) Mwanakijiji naona hapa unataka kulazimishia jambo. Ningekuona analytical zaidi kama jitihada uliyofanya kucalculate hii asili hivyo ungefanya hivyo hivyo kujua asilimia ngapi ya wanachama wa CCM ni waislamu na ni asilimia ngapi ni wakristu. Ili hii proportionality principle yako iwe valid ni lazima ufanye hivyo. Nachojua kwa hesabu ya watu Tanzania waislamu wanazidi wakristu.

UFAFANUZI:

- Assume asilimia 70 ya wana CCM ni waislamu na asilimia 30 ni wakristu. Utafanya pia representation 50/50?

- Na kama asilimia 90 ni wakristu na asilimia 10 ni waislamu utafanya pia 50/50

So ili nikuamini nashauri utujulishe hili.

2) Mwanakijiji unaasume kwamba iwa CCM wanawakilisha maslahi ya dini. Hawa sio viongozi wa dini. Waislamu na wakristu si lazima wapingane kwenye sera hata kama zinahusu dini. Nakumbuka Mrema ni mkristu lakini anasaport anasupport Mahakama ya Kadhi.

3) Huwezi kujua wakristu na waislamu kwa kuangalia majina. Kuna wengine wana majina ya kiislamu lkn hawajui msikiti uko wapi, wengine majina ya kikristu lkn hawajui kanisa liko wapi. Wengine wanahudhuria matukio ya kidini km social ocassion tu na sio religious. Sasa unaweza kutuambia ni wangapi kati ya hao uliotaja ni practioners wa dini zao?

Makamba anaswali kweli? Chenge je? Ebu ndugu zetu waislam na wakristo tufahamisheni hili, nina wasiwasi. Au ni wahumini wa ile dini ya "VIJIUNGA"
 
CUF ni chama cha kidini ya kiislam, CCM chama cha dini ya kiislam, chadema chama cha kikabila, NCCR mageuzi cha kikristo, DP cha kikristo, UDP cha kisukuma??!! CHAUSTA cha kipentecoste??? chagueni mnataka chama gani? cha mafisadi? cha kikabila au cha kidini?


Mama mbona haujaspecify kabila hapa kama ilivyokuwa "UDP cha wasukuma".
 
Hivi JF ni branch ya Chadema? mtu kwao, mpaka kieleweke, slaa, zitto wazito wa chadema? haya kitila, mwanakijiji, mgaya et al washabiki, wapenzi, wakereketwa wa chadema? just curious.
 
kama yafuatayo hapa chini wewe huoni kama ni kucriticize basi wewe una lako jambo:

CCM,CHADEMA,CUF,NCCR na UDP
Hakuna chama kinachofuata DINI yoyote ya Kiislam wala Kikiristu maana hawafuati maadili ya dini hizo,humo CCM kuna mafisadi hakuna dini humo,CHADEMA wafisadi wamo na wabaguzi wa ukabila pia wamo na vyama vingine vivyohivyo.

Hata hivyo Nakubaliana na nashauri huo uwiano inabidi wauungalie CCM maana Adui usimpe chansi ama upenyo.Mimi sikatai wala kukubali .Hii ni hoja mhimu yakuangaliwa kwa wana CCM.CCM mmesikia hilo.
 
Mama mbona haujaspecify kabila hapa kama ilivyokuwa "UDP cha wasukuma".

okay, chadema chama cha wachaga, tlp chama cha wachaga; ai wachaga kwa siasa, karibu watachukua "nji", keleuwiiiii, ruwa mangi na m.....
 
Mimi sitaki kushabikia suala la udini ikiwa ni CCM au chama chochote – our focus should be to look at the development of the country!

Suala la uwingi wa waislamu ulikinganisha na wakristo haimaanishi kuwa wakristo wanaburuzwa kwenye decision za CCM.

Tukiangalia kuwa Nyerere alikuwa mkristo lakini ndiye aliyekuwa decision maker wa CCM pamija na kuwa waislamu walikuwa ni wengi.

I suggest hilo suala la udini lipelekwe kwenye forum ya dini, so that we do not get distracted from our main focus – I cant believe that MKJJ can raise such an issue, as I have great respect for him!
 
Mama mbona haujaspecify kabila hapa kama ilivyokuwa "UDP cha wasukuma".

Anachofanya mama hapa ni kusema yaliyosemwa na wengine (sio mama) kuwa chadema ni chama cha kikabila. Inawezekana mama halijui hilo kabila ila wewe unaweza kuwa unalijua na ukalitaja hapa kwa msaada wa wanajamvi wote.

Kanuni ile ile inayotumika kuviita hivi vyama vingine kuwa ni vya kikabila au kidini ndio hiyo hiyo inatumika kukiita ccm kama chama cha kidini.
 
Nyerere alisema CCM haina dini, katiba ya CCM inasema hivyo pia, tukumbuke majina sio kipimo cha uumini, factors nyingi kama wakati, muundo wa hio kamati kuu,sifa na geographical areas wanapotoka wajumbe ndio imesababisha kupelekea percent kubwa ya wajumbe kuwa waislam, CCM na vyama vyote vengine wana vigezo vyao ambapo hawaangalii dini bali uwezo na sifa za wawakilishi, Nchi ya Tanzania ina mchanganyiko wa dini kuu mbili Uislamu na Ukiristo na kama ccm kweli ina Udini hebu tuangalie tokea imeanzishwa na hao wajumbe wa ngazi za juu tokea inaanzishwa walikua ni waislamu? Hivi imejenga misikiti mingapi au makanisa mangapi? hiki ni chama cha siasa sio Dini! Tuachane na mawazo finyu jamani ili tuendelee, Tuangalie nchi za wenzetu hivi vyama vya siasa mfano democrat,Republican(USA) Labour/Conservative(UK) Kanu(kenya) ni vya kikristo kwa vile asilimia kubwa ya viongozi wao ni waumini wa kikristo? Au kule Somalia, Egypt nk unategemea vyama vyao vya siasa viwe na wakristo asilimia sawa na waislam? Iyo Wangwe's Doctrine yako haifai ktk kuleta maendeleo ya nchi yetu, cha kuangalia ni uwezo na sifa za viongozi sio dini au kabila zao. Ni hayo tu.
 
kama yafuatayo hapa chini wewe huoni kama ni kucriticize basi wewe una lako jambo:

Nakubaliana na wewe..Ila swali la msingi kutoka kwa Kubwa jinga lilikuwa ni lini alianza ku criticize?
Navyojuwa ni kelele za WANGWE HIZO!
Maana hiyo makala hapo juu ya MKJJ ni ya jana kama sikosei!
Sasa hayo matatizo kayajuwa jana?
 
Hivi JF ni branch ya Chadema? mtu kwao, mpaka kieleweke, slaa, zitto wazito wa chadema? haya kitila, mwanakijiji, mgaya et al washabiki, wapenzi, wakereketwa wa chadema? just curious.

Mama,

Hapa pia kuna Mtu wa Pwani, kada mpinzani, Kubwajinga, zemarcopolo, kibunango, masatu, FMES, na wengine wengi tu ambao ni wanaccm. Itakuwa ni makosa kutumia majina machache ya wanaofikiriwa kuwa upinzani kusema kuwa JF ni branch ya Chadema bila kujali kuwa kuna wanaJF humu ambao ni wana ccm.

JF haina chama ila wanachama wa JF wapo wenye vyama na wapo wengi ambao hawana vyama vyovyote vile.
 
Mi sioni sababu ya watanzania kuanza kuangalia masuala ya dini sijui kabila, wote ni watanzania tunaopinga au kukubali ufisadi fullstop.
Haya mambo ya dini tuna uhakika nayo? kama ni kwa kuangalia majina then we/you are totally wrong, kuna kina Mohamed, Juma ,Omari kibao makanisani, na nimewaona kina Peter, John misikitini. Unless umemuuliza mhusika na akakutajia dini yake then utakuwa na uhakika yeye ni dini gani ila kwa majina, tusiendelee kufanya assumptions zisizo na maana.
Na kwenye makabila kuna baadhi yetu hatujali mtu ametokea wapi ili mradi anafanya kazi vile inavyotakiwa, hapa sitaongelea sana sababu tuko tofauti na tunachukulia hili swala kwa uzito tofauti.
Habari ndio hiyo...............!
 
na budhha na bohora wataunda vyao, si ulisikia maaskofu wanataka representation bungeni? Mashihidi wa yehova na SDA nao hawatakubali! na wahadzabe nao watataka mwakilishi. Hivi kuna mbunge anayewakilisha watoto? maana hili ni kundi maalum na liko underrepresented, wanangu mpo???

Na waislamu nao wanataka kujiwatala kwa sheria zao wao ndani ya nchi yenye mfumo thabiti wa sheria isiyofungamana na dini yoyote....all these put together you just get the MOST POISONOUS COCKTAIL you never had!
 
Friends... I am making a very serious point here... na sijasema mimi naamini nini.. nimehoji tu? Ukiacha jazba na emotions na kurudi na kusoma pole pole nilichoandika you might get what I'm trying to say. Ila kama hutaweza kukipata nikipata nafasi nitakifafanua. Nachagua maneno yangu vizuri na hata kichwa cha habari kiko kwa makusudi.
 
Mama,

Hapa pia kuna Mtu wa Pwani, kada mpinzani, Kubwajinga, zemarcopolo, kibunango, masatu, FMES, na wengine wengi tu ambao ni wanaccm. Itakuwa ni makosa kutumia majina machache ya wanaofikiriwa kuwa upinzani kusema kuwa JF ni branch ya Chadema bila kujali kuwa kuna wanaJF humu ambao ni wana ccm.

JF haina chama ila wanachama wa JF wapo wenye vyama na wapo wengi ambao hawana vyama vyovyote vile.

hapa wanaodominate hii terittory ni hao chadema, na hao uliwataja wakiwa humu wanaitwa wapinzani vidume??!! tena umemsahau masaka, kijana yule sijui anavuta nini, tena saa ingine sio kuvuta...waweza fikiri kapuliziwa. Katika sentensi zake inayonifurahisha ni ile ya kidumu chama cha mapinduzi, kwi kwi kwi kwiii, tena ukiisema hiyo kwa tone ya karume, mie mbavu sina hahahahaaaaa
 
mi Sioni Sababu Ya Watanzania Kuanza Kuangalia Masuala Ya Dini Sijui Kabila, Wote Ni Watanzania Tunaopinga Au Kukubali Ufisadi Fullstop.
Haya Mambo Ya Dini Tuna Uhakika Nayo? Kama Ni Kwa Kuangalia Majina Then We/you Are Totally Wrong, Kuna Kina Mohamed, Juma ,omari Kibao Makanisani, Na Nimewaona Kina Peter, John Misikitini. Unless Umemuuliza Mhusika Na Akakutajia Dini Yake Then Utakuwa Na Uhakika Yeye Ni Dini Gani Ila Kwa Majina, Tusiendelee Kufanya Assumptions Zisizo Na Maana.
Na Kwenye Makabila Kuna Baadhi Yetu Hatujali Mtu Ametokea Wapi Ili Mradi Anafanya Kazi Vile Inavyotakiwa, Hapa Sitaongelea Sana Sababu Tuko Tofauti Na Tunachukulia Hili Swala Kwa Uzito Tofauti.
Habari Ndio Hiyo...............!

Nakubaliana Na Wewe...watanzania Waelewe Hili....kuna Dini Mbili Tu...at Least Kwa Sasa Taifa Letu Lina Dini Mbili...Nazo ni..

1)Dini Ya Wazalendo

2)Dini Ya Mafisadi.

Nb:kazi Yetu Hapa Jf Ni Kuwaambia Wananchi kuwa Nani Yuko Dini Gani Kati Ya Hizo Dini Mbili Hapo Juu Kabla Hamjapiga Kura!
 
Na waislamu nao wanataka kujiwatala kwa sheria zao wao ndani ya nchi yenye mfumo thabiti wa sheria isiyofungamana na dini yoyote....all these put together you just get the MOST POISONOUS COCKTAIL you never had!

patakuwa hapatoshi, Mungu epushia mbali kabisa tena katikati ya bahari. Ndio maana hizi mambo za udini zinakuwa hatari sana.
 
Huyu bwana Mwanakijiji anataka kuturudisha kwenye enzi za zama za mawe!!!!!. Kesho utatuambia hata Taifa stars imejaa udini.....

Umefumbwa fumbo.

Mwanakijiji anatumia lugha ya tasnifa.

Anataka kujenga hoja-kejeli kwamba kama Chadema kuna ukabila kwa sababu Chacha Wangwe kasema kuna Wachaga/Wapare watano kati ya sita basi hata CCM kuna udini kwa sababu wajumbe 25 kati ya 38 ni wa dini moja.

Tatizo la hoja-kejeli yake ni kwamba ame distort hoja ya Wangwe, kaitengeneza upya, halafu akaipa jina, Wangwe's Doctrine.

Wangwe hakusema anataka wajumbe wagawanywe sawa kwa sawa. 6 gawanya kwa 26 haigawanyiki. Wangwe kauliza itakuwaje Watu 5 kati ya 6 watoke eneo moja.

Wangwe na wenzake hawakuwa na mikoa miwili tu ya kugawanya nafasi kama dini zilivyo, bali 26. Walikuwa na uwezo mkubwa wa kuzigawa.

Wangwe hakutumia kigezo hicho kimoja tu cha 5 baina ya 6, ila ni shutuma ambayo haikuanza na uchaguzi wa Wabunge wa 2005, na pia amedai hata madereva na wafagiaji CHADEMA ni wa eneo moja.

Mwanakijiji ame distort alichosema Wangwe.
 
Mama,

Hapa pia kuna Mtu wa Pwani, kada mpinzani, Kubwajinga, zemarcopolo, kibunango, masatu, FMES, na wengine wengi tu ambao ni wanaccm. Itakuwa ni makosa kutumia majina machache ya wanaofikiriwa kuwa upinzani kusema kuwa JF ni branch ya Chadema bila kujali kuwa kuna wanaJF humu ambao ni wana ccm.

JF haina chama ila wanachama wa JF wapo wenye vyama na wapo wengi ambao hawana vyama vyovyote vile.

Mgaya,
Kwa vile tunapinga vituko vya CHADEMA haina maana kuwa sisi ni CCM, ingawa wapo walio-declare kuwa CCM. Wengine tunachotaka tu ni kila atakayeshika madaraka ya nchi yetu awe vile tunavyotaka sisi, mzalendo, asiye mkabila wala mdini period. Hayo ya JF kuwa ext. ya Chadema nafikiri ni suala zuri kujadili likipewa thread yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom