UDA yauzwa kwa bei chee, Ofisi zake Zavamiwa

Kwa vile kuna mpango wa DART ambao unahusiana na usafiri wa Jiji la Dar - kazi iliyokuwa imefanywa kisheria na UDA - kwanini UDA haikubadilisha na kuwa hiyo mamlaka mpya ya DART - ikiwa na facilities na mara nyingine ambazo zingeweza kuwa sehemu ya mtaji wake? Kulikuwa na tatizo gani la kuzuia UDA isiwe DART?

Kwa kweli hata mimi nimeshindwa kuelewa. Decisions nyingine huwa zinafanywa mpaka unashindwa kuelewa why they reached such a decision. Mwaka jana waziri Mkuu Pinda, kwa Niaba ya Rais Jakaya Kikwete, akizundua mradi wa mabasi matano yenye dhamani ya sh 500 million ya kubeba wanafunzi yaliyotolewa na CRDB kwa UDA alilitaka shirika la UDA kuwa macho ili lsije likafia mikononi mwao. Kuna mdau alighusia humu JF mwaka jana kuwa kabla ya kutoa huu msaada, UDA waliomba mkopo wa kununua mabasi CRDB wakatoswa. UDA bado ni shirika zuri na kilichotakiwa kufanywa na serikali ni kulifufua hili shirika na kulitumia katika mradi mzima kuboresha usafiri Dar Es Salaam. Badala yake tunaona yale yale ya KAMATA. Kukiwa na shirika moja tu lenye uhakika kusafirisha watu kwenda waendako sijui kama watu wataamua wapande magari yao kwa kila siku.
 
Dah kweli Nchi haina utawala wa sheri, mpaka mtu binafsi anaenda kuvunja ofisi za shirika la UMMA, hachukuliwi hatua tu, jamani sijaona nchi yenye kunuka rushwa kama hii

Mamamuzi magumu, maamuzi magumu, maamuzi magumu!!! Ni nani kati ya Mwekezaji, Meneja wa Uda, Polisi na Wizara hawezi kuchukua maamuzi magumu? Mwekezaji kavunja ofisi-kachukua maamuzi magumu. Meneja wa Uda kaenda polisi - kachukua mmamuzi magumu. Polisi imemweleza meneja akajadiliane na mwekezaji na wahusishe mamlaka / wizara husika -polisi imechukua maamuzi magumu. Naibu Waziri kaulizwa kulikoni iofisi ya umma kuvunjwa na mwekezaji, kasema yuko jimboni kwake hajui kinachoendelea huko UDA - kachukua maamuzi magumu!!! Mmmmmm, kukosa kuchukua maamuzi magumu wakati muafaka na kwa umakini kunai-cost sana nchi yetu!!!
 
tatizo decision maker karibu wote wanamiliki daladala. kama kuna taasisi inaweza kusimamia haya mawazo mazuri yanayotolewa kwenye hii post tunaomba ijitokeze kuishindikiza serikali nasi tutakuwa nao bega kwa bega. Yaani nimeipenda sana hii post kiasi kwamba natami ningekuwa mimi ndiye muamuzi mkuu. msongamano mjini ungeisha fasta
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Natamani niwaajue think tankers wetu ili nijue Mungu aliwapa akili zao wazitumie wapi?Atuwezi wote kukaa kama Taifa ili tufikilie tutaliendashaji shirika letu kama ilo UDA,ila kupitia wachache wetu wanabeba dhamana ya kuamua hatima ya shughuri za umma kwa faida yetu sote.

Nahoji maamuzi haya ya kila kitu kubinafsiha jamani hatuna tunaloweza jamani,tukalifanya nasi tukawa na vyetu kwa faida yetu.Jamani hivi Serikali inawezaje kuwa na dhamila za kuhitimisha kitu ambacho kwa macho ya kawaida uwepo wake ni ndani ya uwezo wa Serikali ni tija zaidi kwa Umma kuliko kukabidhiwa kwa sekta binafsi.

Kwanini tusipime faida ya kuwepo mikononi mwa Serikali ni bora zaidi kuliko uwepo wake mikononi mwa mtu binafsi.THINK TANKERS wa sasa watoto wenu huko mbele ya safari watauliza hata mifupa yenu kuwa mlikuwa na matatizo gani kufikia maamuzi haya leo mnayoyafanya leo hii,kwa kuwa gharama zake zitalipiwa na watoto wenu hao.

Watakapokuwa wanaambiwa kulipa gharama hizo wataomba kujua uwezo wenu wa maamuzi wakati ule ulikuwa na walakini na hatimae mtakuwa mmewapa matatizo vizazi vyenu,kutiliwa shaka nafasi yao kupewa haki yao wao pia kuthibisha kama wanaweza kuongoza wenzao [Like Son Like Father or Like Daughter Like Mom].Hivyo mtakua mmeua kizazi chenu na watawachukia daima.Kwanini mnaliamulia Taifa kwa kuangalia leo tu jamani.
 
Kufika 2015 Tz itawaka moto. Miaka ya yuma waliuza hivi hivi mashirika kama UDA na hakuna aliyewahoji. Wamejisahau, wanaendelea. Watu wakihoji wanaitwa wapinzani
 
Fools leading us to fall in everything, na mbaya zaidi na zaidi, ufisadi unafanyika saaana wakati wa kuuza governmental sectors to private firms, here is where wizi mkubwa unafanyika, unakumbuka ubinafsishaji wa mashirika ya umma, banks, etc na ukisikia Ubia/ eti govern 51% na mwekezaji 49% tumeliwa, ni mazing'aombwe tu, hizi kampuni za madini kibao uliza mbunge hata mmoja tena jimbo wanalochimbia hata serikali inapata % ngapi is unknown, eg Kule selous juzi kati Maige (laziest of all ministers, na sijui if he knows himself first, wanyama hai wamepelekwa nje usiku Maige hajafukuzwa kazi)kasema imemegwa 34,000 km kwa ujimbaji wa uranium of which mapato kwa mwaka estimated to be $200mil serikali itapata only, only, onlyyyyyy, onlyyyyyyy $8mil kwa mwaka aibu gani hiiii, nani hajui madhara makubwa ya uranium, jamani uranium leakage is worst ever, it affects kizazi na kizazi genetically, waziri anatamka akikenua meno eti mapato yataongezeka, punguani kweli, sasa UDA ni mwendelezo wa Ufisadi, imagine mtu binafsi anavunja ofisi ya serikali then wapo kimya na polisi/ mkuu wa temeke anasema wamalizane wenyewe huko, what, what give me a break, shame...!!!!
 
Mr Mak,, hata wewe hii leo imekugusa, umeona mafinyufinyu ya utawala uliopo sasa. nzuri sana! ukweli inauma sana, unapokuja kusoma majibu aliyotoa kiongozi wa Wizara "nipo jimboni kwangu", majibu ya kamanda wa polisi "kapatananeni" unakanganyikiwa kabisa. pale kuna crime tayari (uvunjaji),, wanapatana nn sasa?
 
Maslahi binafsi yakiwa mbele hakuna tutakalofanya likaenda mbele ......hivi ile hoja ya Kikwete kupeleka muswada bungeni kutenganisha siasa na biashara iliishia wapi? au Ma-lobbyists walimzidi kete? Manake naona mambo mengi nchi hii inaumia kwa sababu ya maslahi ya kibiashara ya watu walio madarakani na nje kuangalia kwanza biashara zao na wakikumbuka ndio wananchi na nchi baadaye.
 
Ngoja tutengeneze vi- oligarchs vyetu hapa. Sijui tunasubiri nini kubinafsisha MAGEREZA ili kauli na utabiri wa Mwalimu utimie.
 
Inasemekana kuwa Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA) lenye assets zenye dhamani ya sh12 billion limeuzwa kwa kampuni ya Simon Group Ltd kwa sh 285 million. Wapo wengine wanasema kuwa ni asilimia 51 tuu ya share za UDA zimeuzwa kwa sh12 billion. UDA ilifanyiwa valuation mwaka 2009 ambapo ilikutwa ikiwa na assets zenye dhamani ya mabilioni ya shilingi. Kwa mujibu wa mkataba, Simon Group Ltd ilitakiwa kulipa malipo ya awali ya asilimia 25 ya shares ndani ya siku 14 baada ya kusaini mkataba, malipo ya asilimia nyingine 25 ya shares ndani ya siku 120 baada malipo ya kwanza, na asilimia 10 kila mwezi mpaka malipo yote yakamilike.

Hata hivyo, mpaka February 25, 2011, Simon Group Ltd imenunua asilimia 12 tuu ya shares kwa sh285 million na haijalipa malipo mengine yaliyobakia. Ukiangalia hapo tayari imeshavunja mkataba kuhusiana na malipo. Cha kushangaza kuna taarifa kuwa mnamo tarehe 21 mwezi ulipita, majira ya jioni, Simon Group Limited walivunja ofisi ya Meneja Mkuu wa UDA zilizopo makao makuu ya UDA Kurasini na kuchukua ofisi.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya UDA, Iddi Simba, amekubali kuwa kweli ofisi za UDA zimevamiwa na mwekezaji wa ndani lakini suala zima linashughulikiwa na CHC. Kuna taarifa ambazo hazijadhibitishwa kuwa serikali imesimamisha mauzo ya hizo asilimia 51 ya shares za UDA kwa sababu mauzo hayakufuata taratibu zinazotakiwa.

Manager wa wa UDA, Victor Milanzi, ameripoti suala husika polisi. ACP wa polisi Temeke amesema kuna "contractual misunderstanding" kati ya UDA na hiyo kampuni na ameshauri pande zote zikae chini ili watatue tatizo kabla ya kuchukua hatua za kisheria. Pia amesema ameshauri pande zote mbili watatue tatizo lao kupitia wizara na mamlaka husika. Kaimu Waziri wa Usafirishaji, Dr Athumani Mfutakamba, amesema hana taarifa na uvamizi huo kwa vile kwa sasa yupo jimboni kwake.

Waosha vinywa wa chama tawala watakwambia wameamua kubinafsisha ili lifanye kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora.
 
UDA ilitokana na kubinafisishwa kampuni binafsi ya Dar es Salaam Motor Transport (DMT) na kuzaa UDA na KAMATA. Kampuni ya DMT ilikuwepo tangu enzi hizo za mkoloni halafu ikabinafishwa na utawala wa Mwalimu Nyerere.
Ikataifishwa Mama Mdogo.Sasa ndio imebinafsishwa tena.
 
Sauti zetu wananchi wala hazisikiki huu ndio ukweli kwani sasa ni upupu juu ya upupu kuna nakala moja Prof Shivji aliandika akielelezea jiinsi vile wale walionacho especially viongozi wa serikalini ambavyo sasa haelewi kuwa kuna wananchi wana shida na si kwa makusudi bali ni level ya ufisi waliyofikia ndio inawafanya hivi inawablind completely i think we shud sit down and devise a strategy which will allow us the Government ( Gov is the People) "its ironic in our tz context" to be heard by the one we have employed to work for us (The Gov in our Tz Context)
 
kuvunja ofisi hata kama UDA na Simon Group wana mkataba tayari ni uhalifu na hawataweza kukaa pamoja wakapatana nilifikiri polisi wangefanya kazi yao ya kumkamata kwa kosa la kuvunja ofisi mambo ya mkataba hayahusiani na polisi.
 
Iwapo hiyo DART itakuwa shirika la umma, basi fate yake haitatofautiana na ya UDA.
 
Dah kweli Nchi haina utawala wa sheri, mpaka mtu binafsi anaenda kuvunja ofisi za shirika la UMMA, hachukuliwi hatua tu, jamani sijaona nchi yenye kunuka rushwa kama hii

Ukiona hivyo ujue kuna mtu anawapa Kiburi (Unajua miradi hii ni ya wakubwa sasa wanatumia makampuni ama watu wengine tu kukwapua mali za umma)
 
Dah kweli Nchi haina utawala wa sheri, mpaka mtu binafsi anaenda kuvunja ofisi za shirika la UMMA, hachukuliwi hatua tu, jamani sijaona nchi yenye kunuka rushwa kama hii
sheria zinatumika kudhibiti upinzani na kuiba maiti mochwari.tutafika tu msijali chamsingi tumeshaiona njia ya kupita.kaza moyo kujua mambo kunaumiza moyo sana hasa unapofanyiwa mambo ya kijinga na serikali ya mambumbumbu kama hii.
 
Huko kwenye Mawizara kuna mtu mwenye akili kweli au wote mapunguani tu?

Dr Gaijin(wastahili)

Mawizarani wapo watu wenye akili tena saana, wengine ni wachapa kazi kweli. Tatizo nipale unakuta file lina kimemo juu,pia maslahi ya wazee, hali kama hii, watu wanavaa miwani ya mbao na kuharakisha mwanaharamu apite salama

Nikupe mfano mzuri, kuna wizara moja nyeti tu, kuna mama moja ni mkuu wa kitengo( elimu yake ni kichekesho) hata mtoto wa kidato cha sita anaweza challenge reason capacity yake. Huyu mama ananguvu kuliko katibu mkuu wa wizara, na hata waziri mwenyewe. Kisheria anatakiwa areport kwa katibu mkuu lakini yeye anareport Magogoni moja kwa moja. ma dr, wasomi waliopo hapo wizarani utawalaumu kwa maamuzi yasiyokuwa na tija kwa taifa yanayotendwa na wizara?

Inaiskitisha lakini ndo hali ilivyo
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom