Kwahiyo hapa umekubali kwamba kuzaliana sio chanzo cha uhai kama ulivyodai, bali ni muendelezo tu?
Kuzaliana huko hakuwezi kutokea pasipo viumbe walio hai.
Kuzaliana ndio chanzo cha uhai.
Uhai hauwezi kufanyika kama hakuna viumbe hai.
Unasema kuzaliana ni chanzo cha uhai cha kiumbe kipya,...Je hicho kiumbe cha zamani (kabla mfumo wa kuzaliana haujaanza) kilipatia wapi uhai?
Ndio maana nilikwambia process ya kuzaliana ni
Endless. Haina mwanzo wala mwisho.
Ukianza kuweka ulazima wa kwamba process ya kuzaliana ina mwanzo. Hata huo mwanzo wa process ya kuzaliana lazima uwe na mwanzo wake mwingine.
Na kama ulazima huo haupo, Hata huo mfumo wa kuzaliana hauna na Hauhitaji mwanzo.
Maelezo yako bado yanathibitisha kwamba kuzaliana ni muendelezo tu wa uhai na sio chanzo cha uhai..
Nilikwambia hivi, kuzaliana ni mwanzo wa uhai wa kiumbe kipya kutoka kwa viumbe wa zamani wa jamii hiyohiyo ambao tayari wana exist.
......hii concept unaweza ukaifananisha na "Original & Copies" au "Production & Reproduction" nadhani ukielewa hizo terms mbili ndiyo utajua tofauti kati ya mwanzo wa uhai wa aina fulani ya kiumbe na muendelezo wa kizazi cha kiumbe husika.
Kama hakuna viumbe hai wa kuzaliana kuleta uhai, utapata wapi huo uhai?
Hapa ndiyo umezidi kujichanganya,..yaani unasema Kuzaliana ndio kulianza kwanza.? haiingii akilini kabisa logically & Biologically ili kuzaliana kuwepo utahitaji viumbe ambao ni HAI,..kukishakua na viumbe hai kuzaliana ndiyo kunafuata sasa,......
Ndio maana nilikwambia kuzaliana ndio mwanzo wa kiumbe kipya husika(kimoja) kutoka kwa viumbe wa zamani wa jamii hiyohiyo waliozaliana.
Na process ya kuzaliana ni endless.
Hivyo kauli yako kwamba kuzaliana ndiyo kulianza haipo sahihi.
Sasa kama kuzaliana hakukuanza, Thibitisha basi kilicho anzisha uhai pasipo kuhusisha viumbe waliozaliana.
Yes, Uhai unaendelezwa kwa kuzaliana,....je chanzo cha uhai ni nini?..............Maana kimsingi hata wewe umekubali kwamba kuzaliana kunaendeleza tu uhai lakini si chanzo cha uhai,..
Chanzo cha uhai ni viumbe hai.
Ambao walikuwepo, wapo na wataendelea kuwepo.
NB; Kama ukiwa muelewa utaona wazi kwamba kwanza inabidi kuwe na viumbe hai kisha kuzaliana kufuate,..sasa hoja ya msingi ni kwamba kabla ya kuzaliana kuanza, hao viumbe hai wa mwanzo "yaani original creatures walitokea wapi au vipi, before sisi copies tunaotokana na kuzaliana???
Hakuna ulazima wa kwamba viumbe hai(original creatures) vina mwanzo.
Kama ulazima huo upo, hata huo mwanzo wa original creatures, lazima uwe na mwanzo wake mwingine.
Pasiwepo kiumbe chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo mwanzo.
Na kama ulazima huo haupo, Hata original creatures hawana mwanzo.