Sawa,..kwa mantiki hiyo tunakubaliana kwamba kuzaliana ni mfumo ambao hauendelei tu wenyewe to infinity bali kuna muda inabidi uwe controlled, ili kuhakikisha viumbe havitoweki duniani?
Hapana haiko hivyo.
Mfumo wa kuzaliana unaendelea tu wenyewe to infinity na hauhitaji kuwa controlled na yeyote yule.
kwa sababu mfumo huu wa kuzaliana unaji control wenyewe automatically.
Ndio maana wanyama,ndege,samaki na viumbe wengine wote wanazaliana tu wenyewe kila kukicha pasipo kuwa controlled na yeyote yule.
Viumbe kutoweka duniani na mfumo huu wa kuzaliana kukoma, Labda litokee tukio ambalo litawa angamiza viumbe wote wakaisha wote kabisa, Pasipo hata kiumbe mmoja kubakia.
Hapa ndipo unaweza kusema kwamba mfumo wa kuzaliana umefika mwisho kabisa.
Lakini kama viumbe bado vipo, mfumo wa kuzaliana utaendelea wenyewe, automatically.
Na, Je tunakubaliana kwamba kwenye hoja hii umekiri mwenyewe kwamba kuzaliana sio chanzo cha uhai na maisha ya viumbe hai hapa duniani?......
Kuzaliana ndio chanzo cha uhai kwa kiumbe husika.
Ambapo kiumbe hicho husika hupata uhai kutoka kwa viumbe wa jamii yake.
Kwani wewe kabla hujazaliwa ulikuwa na uhai?
Uhai si umeupata baada ya wazazi wako kukuzaa wewe?
Au ulikuwa na uhai kabla ya wazazi wako kukuzaa?
Maana umeonyesha kwamba viumbe wakifa wote hawatoweza kuwepo tena duniani kwasababu hata kuzaliana hakutokuepo......
Ndio viumbe wakifa wote na mfumo huu wa kuzaliana utakufa na hautakuwepo tena.
kwa sababu viumbe hawatakuwepo tena.
Viumbe wapo na mfumo wa kuzaliana upo.
Pia viumbe vikiendelea kuwepo na mfumo wa kuzaliana utaendelea kuwepo.
Viumbe vyote vikitoweka kabisa na mfumo wa kuzaliana utatoweka, hautakuwepo tena.
Sasa kama kuzaliana sio chanzo cha uhai wa Viumbe hai....Je, uhai wa viumbe hai ulitoka wapi?
Kuzaliana ndio chanzo cha uhai ambao upo milele.
Na mfumo huu wa kuzaliana umetoka kwa viumbe ambao walikuwepo, wapo na wataendelea kuwepo milele.
Maana tumeona kwamba no uhai no kuzaliana,....tujiulize sasa nini kilifanya mpaka viumbe vikapata uhai na kufanya mfumo wa kuzaliana kwa viumbe hai ukawepo.
Uhai upo milele, kuzaliwa ndio mwanzo wa Uhai wa kiumbe husika.
Uhai una mwisho kwa kiumbe husika ambao ni Kifo.
Ndio maana kila kiumbe hupata uhai kwa wakati wake, Na kifo kwa wakati wake.
Wewe hukuwa na uhai, ila ulipata uhai baada ya kuzaliwa.
Na hata vitukuu vyako kwa sasa havina uhai ila vitakuja kupata uhai kwa kuzaliwa.
Hivyo uhai mwanzo wake ni kuzaliana kwa viumbe husika, kuleta kiumbe kingine kipya.
Viumbe vina mwanzo ambao ndio uhai unaotokana na kuzaliana, Na mwisho ni kifo.