Sijapewa username bado
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,717
- 2,746
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limeeleza kuwa linaendelea kufanya uchunguzi wa kifo cha aliyekuwa msanii maarufu wa vichekesho na mshereheshaji, Emanuel Mathias, maarufu MC Pilipili kilichotokea mkoani Dodoma.
Akizungumza mapema leo Desemba 22,2025 jijini Dodoma, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Gallus Hyera amesema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea na Jeshi la Polisi linakusanya taarifa muhimu ili kubaini chanzo na mazingira ya kifo hicho.
Hyera ameeleza kuwa baada ya uchunguzi kukamilika, watatangaza hadharani matokeo ya uchunguzi huo ili umma upate taarifa sahihi kuhusu tukio hilo.
Aidha, Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu, kuepuka kutoa taarifa zisizo sahihi na kuwataka kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kufanikisha uchunguzi huo.
Chanzo Mwanachi
Akizungumza mapema leo Desemba 22,2025 jijini Dodoma, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Gallus Hyera amesema uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea na Jeshi la Polisi linakusanya taarifa muhimu ili kubaini chanzo na mazingira ya kifo hicho.
Hyera ameeleza kuwa baada ya uchunguzi kukamilika, watatangaza hadharani matokeo ya uchunguzi huo ili umma upate taarifa sahihi kuhusu tukio hilo.
Aidha, Jeshi la Polisi limewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu, kuepuka kutoa taarifa zisizo sahihi na kuwataka kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kufanikisha uchunguzi huo.
Chanzo Mwanachi