UHURU JR
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 17,375
- 8,666
Nimesema toka mwanzo kwamba bado hatujajua roho ni nini, sasa labda useme kuwa ukiwa hujui kitu ni nini basi hufanya hicho kitu hakipo.Sijauliza roho inahusishwa na nini, nimeuliza roho ni nini.
Kama ni habari ya kuhusishwa tu, Willy Gamba anahusishwa na majasusi wa Tanzania, katika riwaya za Aristablus Elvis Musiba, lakini hilo halimaanishi Willy Gamba ni jasusi wa Tanzania aliyepo kiuhalisia nje ya hizo riwaya.
Sasa na wewe unahakikishaje roho ipo kweli na si sehemu ya hadithi tu kama Willy Gamba?
Sijajua habari za hadithi zimeingiaje hapa! kuna baadhi ya maradhi ambayo bado hayaja julikana hasa husababishwa na nini ila vipo vitu ambavyovinahusishwa kusababisha hayo maradhi. Sasa kwenye roho hatujui hasa roho ni nini ndio maana nikatumia neno kuhusishwa na uhai.