Wakati umefika kuangalia uwezo wa jeshi letu la polisi,nafikiri miezi sita wanayokaa chuoni haiwatoshi kabisa. Inashangaza sana,polisi walikuwepo eneo la tukio,tena nasikia walikuwepo wengi,mtu anarusha bomu,wanashindwaje kumkamata? Ingekuwa bomu la kutegwa,tungewaelewa,bomu linarushwa,watu wanamwona mrushaji,wanaanza kumfukuza,polisi wanashindwaje kumpata mhusika? Hakika,ama polisi wetu uwezo wao ni mdogo sana au wanahusika na mlipuko wa bomu hil😵na sasa uzembe wao au uwezo wao mdogo unaanza kuhatarisha maisha ya watu wengine,viongozi wa CCM kama Mwigulu Nchemba,Mwampamba na wengineo maisha yao sasa yako hatarini,chuki waliyonayo watu juu yao ni kubwa mno,ni mbaya mno kwa usalama wao.
Wakati umefiki kwa serikali kufanya uchunguzi wa kina juu ya uwezo wa jeshi la polisi.Maana,matukio yote yenye mwelekeo wa kigaidi wameshindwa kabisa kuyakabili,Matukio ya mauaji ya bomu kanisani Arusha,na yale ya Mwangosi, na yale ya padre Zanzibar,mateso ya Ulimboka,kubenea na Kibanda,n.k hayana majibu.Sasa watu hawana imani tena na polisi wa Tanzania,jambo hili ni la hatari sana,siku itafika watu watakapoamua kuanza kuwavizia polisi njiani na kuwaua,hapo ndipo kutakapokuwepo kilio cha kusaga meno,kinga ni bora kuliko tiba,nashauri polisi wote waende J.K.T. miaka miwili,maana tumeambiwa J.K.T inajenga uzalendo,wakimaliza jeshi waende mafunzo ya polisi kwa miaka isiyopungua mitatu,itakayowajengea ukakamavu na kuwaongezea intrlijensia.TAFAKARI.