Ni nani anamiliki SMG Tanzania?
Swali zuri sana. Mostly SMG zinamilikiwa na vyombo vya usalama, hususan polisi.
I said mostly, maana yake si ajabu kukuta mtu binafsi anayo.
Na pia tunajua kwamba jeshi letu la polisi alosto, askari polisi hao hao wengine wanabadili nguo za kipolisi na kuingia kazini kama majambazi na SMG za serikali.
Au kuzikodisha kwa majambazi.
Hivyo basi, ingawa inawezekana kabisa kwamba hii ni kazi ya vyombo vyetu vya usalama, mtu atakayefikiria kidogo tu ataona kuwa, kama kulikuwa na watu wengine, tofauti na vyombo vya usalama, waliotaka hili lionekane kama limefanywa na vyombo vya usalama, wangejua kwamba kutakuwa na forensic investigation. Na walijua kwamba kutumia bunduki kama zinazotumiwa na vyombo vya usalama kungeleta picha kwamba hili limefanywa na vyombo vya usalama, huku wao waliofanya hili kikweli wakiachwa bila uchunguzi.
Sisemi hilo ndilo lililotokea, naonesha tu kwamba hii habari ya kurukia kusema kwamba hili limefanywa na vyombo vya usalama kwa sababu ya risasi za SMG, ingawa inaweza kuwa kweli, inaweza pia kuwa a planted decoy to disguise the real source.
Uchunguzi zaidi utakaoweza ku corroborate mambo mengi zaidi yanayoonyesha kitu kimoja unahitajika.