Mkuu
Kwenye post yako umezingatia vigezo gani kuwapambanisha chadema na waislamu.
Waislamu ni waumini wa dini ya kiislam wakimfuata Mtume mohamad (SAW)
Chadema ni chama cha kisiasa chenye lengo la kushika dola kwa maana ya kuwasimamia na kuwaongoza watanzania
wote (waislam, wakristu, wahindu na wote wasioamini na kuamini) katika kujitawala na kujiletea maendeleo kwa misingi
ya usawa kama ilivyo ndani ya sheria mama KATIBA.
Hivyo chadema ni chama cha kisiasa na si kiimani ndiyo maana kuna Prof Safari, zito na wengineo ambao ni waislamu je hawa nao wanafanya fujo au sio waislamu hao ni chadema?