kelphin
JF-Expert Member
- Dec 24, 2019
- 9,111
- 14,481
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo
Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.
Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.
Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno
Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system
Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol
Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni