Lakasa chika7
JF-Expert Member
- Jan 7, 2017
- 454
- 1,261
- Thread starter
- #21
Baadhi wanasema kuna majini wazuri na majini wabaya, wazuri hua wanasali na kumuomba mungu na wabaya hadi ma atheist wapo
Wapo wanaodai kua kuna elimu juu ya utengenezaji wa hivyo viumbe.
Kuna siku nilisikia redioni mkufunzi akitoa somo namna ya kuita jini kwa kutamka maneno fulani hivi ya kiarabu.
Yale maneno niliyanukuu vyema nikawa naya practice maana mdau alisema unatakiwa uende njia panda usiku wa maneno kisha utamke hayo maneno
Nikiwa na tumaini kua leo ndio siku ambayo najithibitishia kua majini yapo, nikafika njia panda nikaanza kuyatamka hayo maneno kwa kuyarudia rudia zaidi ya mara 100 lakini hakukua na respond yeyote kutoka third party system
Wakati nikiendelea kutamka yale maneno nilishtukizwa na roba flani matata upande wa nyuma, mwanzo nilidhani ni ujio wa jini kumbe ni kibaka wa mtaa na alikua anapiga patrol
Aisee nilimlaumu sana yule jamaa wa redioni
No prove.. Wewe ulikuwa na nyegekuna DADA moja nilikutana nae bar flani hiv hapa mjini..nikamuita tujuike pamoja...duh akaanza kusema ana njaa nimpe 10000 ya chakula,mara aseme mama ake ni mgonjwa anahitaji 100000 ya operation,...sijakaa vizuri ktkt ya maongezi mara anasema tena nimpe 35000 anataka kwenda saloon kesho ..eh hata sijamjibu kitu akapita machinga kabeba viatu flan vya kimasai hivi...akaniambia tena Baby ninulie hiki tsh 30000 tu...
Dah Nilivoondoka ondoka pale hata sielewi nilijikuta tu nimefika home..
MAJINI yapo jamani WANAUME wenzangu