Jifungue na ufahamu uchawi na matumizi ya majini kwenye uchawi

jerryempire

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
5,128
8,648
Habari wapendwa
Imenichukua muda mrefu mno kuandika hii mada lakini imenisukuma tu niandike baada ya kuweka namba yangu kwenye thread fulani humu jamii forum

nimepata simu zisizopungua 30 kutoka kwa watu humu,kuhusiana na masuala mbali mbali yanayowakabili,hizo dm's ndo nyingi mno,itoshe kusema mimi siyo mganga wala mchawi sema maswahibu niliyopitia ni mengi.

kiasi cha kunipelekea kujifunza mengi san sababu,nilishakutana na magwiji wakubwa wa masuala hayo na kuyashuhudia mengi mazito mpaka mengine yakasababisha kuniachia makovu na alama za maisha kwa ambao walisomaga thread yangu humu mnaweza kupata picha halisi.

nitakacho andika ni kile ninachokijua kuhusu masuala mazima ya uchawi hasa jinsi gani unaweza kuchezewa/kujikinga nao na kuhusu majini sababu nayajua na nilishawahi kuyaona na yapi niliyoyaona na utajuaje kuwa uko na jini n.k

NB:
KILA UTACHOTAKA KUKIJUA KUHUSU TIPS NTAZOKUWA NAZITOA, TAFADHALI KAMA UTAKUWA NA SWALI AU LOLOTE NIULIZE AU ULIZA HAPA HAPA KWENYE THREAD NTAKUJIBU SITOJIBU DM WALA SIMU YA MTU NA SIHITAJI PESA YA MTU HVYO SITOTOA NO NA HATA UKIIPATA SITOKUSAIDIA KOKOTE ZAID YA KWENYE THREAD HII KWA MANUFAA YA WENGINE.

UFAHAMU UCHAWI

Wengi ukiwauliza uchawi ni nini watakuwa na tafsiri tofauti lakini hauna maana moja ya kuuelezea,

uchawi umebeba maana nzima ya kuumbwa binadamu na ulimwengu kwa ujumla na ndio,lango kuu linalotumika kuwaunganisha binadamu,mungu,majini,na hata malaika iwe kwa uasi na hata kwa uzuri (toba)

unaweza kujiuliza uchawi unahusikaje na kuumbwa kwa binadamu?

vizuri, Kabla ya kuumbwa binadamu waliumbwa malaika na majini ambao walikaa ndani ya dunia hii miaka na miaka kabla ya kuja kuumbwa sisi binadamu

Aliumbwa adamu na kutokana na upweke wake akatolewa eva/hawa kutokana na pande/ubavu wa adamu ili awe faraja na furaha kwa adamu, na hapo ndipo ilipotokea fitina kubwa ambayo ilimgharimu shetani kufukuzwa mbinguni baada ya kumuasi mungu pale alipoambiwa amsujudie adam.

Mungu alimuumba binadamu kisha akasema kuwa amemuumba binadamu kwenye umbile bora akimaanisha ni kiumbe bora kuliko chochote alichowahi kukiumba,hii ndo kauli ambayo huenda ikawa sababu kuu ya kutokea kwa uchawi na maovu mengi duniani twende pole pole utanielewa hapo baadae,

kuna aina kuu nne za uchawi,

1.UCHAWI WA MAJINI,
Huu ndio uchawi mkubwa na mzito kuliko uchawi wa aina yoyote kwani kafara zake huwa ni kubwa mno na ni level nyingine ya uchawi ambao kama ukifanyiwa ni mkubwa hasa wa baharini,sababu huko ndiko kwenye falme nzito za uchawi.

uchawi huu huhusisha,mito,bahari na maziwa,

uchawi wa aina hii mtu huupata kwa kwenda katika falme za hayo maeneo husika na kukubaliana na masharti ya hao viumbe wa sehemu hizo,na mchawi wa aina hii yeye huwa anasafiri/kwenda kuabudj maeneo ambayo ni jirani na maeneo hayo tajwa hapo.

uchawi wa aina hii mtu huweza kudhuriwa kwa mchawi husika kuchanganya vitu vinavyopatikana ndani ya bahari,ziwa,au mito au mtu anayefanyiwa uchawi kupita katika maeneo hayo au kuwa mfanyaji kazi kwenye maeneo hayo.

2. Uchawi wa pili ni wa anga
Huu ni uchawi ambao mtu huweza kuathiriwa kwa kufungwa kupitia upepo,kimbunga,dhoruba,radi,n.k

uchawi wa aina hii hunuwiwa kumfikia mhusika kwa njia hizo mfano mnaweza kuwa mmekaa tu sehemu ikaja radi lakini hyo radi badala ya kuwapiga watu ote ikampasua mmoja tu kati ya watu 20 wa eneo hilo.

3,Uchwi wa pili ni wa ardhini
huu ndo uchawi unaotumika zaidi katika jamii za wachawi wengi kwani huhusisha mizimu ya asili na kila kilichomo aridhini.

uchawi wa aina hii unaweza kumpata mhusika endapo atachukuliwa kitu kimoja wapo kati ya kivuli,kitovu,nyayo nk

4,uchawi wa moto
huu ni uchawi ambao mhusika akifanyiwa huungua au hata kama ikitokea ajali basi lazima ajali hyo ihusishe moto kuwaka au wahusika kuungua moto.
 
Hope kwa uchache ulishapata picha ndogo kuhusu uchawi sasa tuendelee,

NINI KINAFANYA UCHAWI UTOKEE

Hakika ukiona uchawi unavyofanywa unaweza kusema ni mazingaombwe au mambo ya kuigiza live,lakini kiuhalisia uchawi ufanyikapo hutumika nguvu kubwa nyuma ya pazia ili yatokee yanayotokea ambayo kwa macho yetu ya dhambi hatuwezi kuona (macho yetu ya dhambi) hili ntakuelezea vizuri mbeleni.

Ili uchawi uweze kutendeka na kufanya kazi ni lazima atumike jini husika kwenye kulifanikisha hilo,ndo maana huwezi kutenganisha uchawi na majini abadani,

kinachofanyika mchawi husika,hukutana na jini mhusika wa kichawi ambae huingia maagano ya milele na ndo maaagano haya hufanya baadhi ya wachawi kuacha uchawi sababu wanajua mwisho wake ni kifo na hata kama atakufa ndani ya chama chake cha kichawi basi ule uchawi huendelea kwenye uzao wake ote ndo maana wazee wetu zamani walikuwa hawaoani na uzao ambao una mambo ya kichawi au ushirikina.

Agano la kwanza kabisa kuingia kwenye uchawi ni kukana kabisa dini yako na kuabudu majini automatically,na jambo la kwanza ambalo hufanyika ni kukanyaga iwe Quran au biblia kwenye kinyesi(mavi),then kafara nyingine zitafuata kulingana na cheo au grade mchawi anayotaka afikie.

Hivyo basi mtu anaweza kuwa shekhe/mchungaji mkubwa kwenye dini yake lakini upande wa pembeni akawa ni mchawi mkubwa ila nyuma ya pazia akawa alishaasi kwa mungu,na hapa ndipo pabaya zaidi ambako wengine hupewa mpaka nguvu za kufanya miujiza katika dini zao na kupata wafuasi wengi mno na kuaminika kumbe upande wa pili kuna nguvu hutumika hili ntalielezea baadae.

Hivyo basi nadhani ushafahamu kuwa mchawi hawezi kufanya lolote pasipo uwepo wa jini ndo maana mchawi anaweza kwenda sehemu yoyote duniani ndani ya sekunde na akafika, hapo mchawi huyo huongezewa nguvu na kiweza kubebwa na jini huyo na kufikishwa sehemu yoyote kwa maagano yao waliyoyaingia.

Na hapa jini anayafanya haya yote kwa kuhakikisha kuwa anamkomoa mungu kwa kumpotosha huyu binadamu aliyesema yeye ni mbora kuliko kiumbe chochote,na pia nadhani baadae utapata picha kuwa binadamu ananguvu kuliko kiumbe chochote
 
Achana na mawazo ya kipumbavu uchawi haupo.
wewe utakua ni mchawi, wachawi ndio huwa wanatengeneza mazingira watu wasiamini kua uchawi upo na uongo ni kazi zenu.

Ufunuo 21:8

Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na madini ya kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.”

Ufunuo 21:15

Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.

Matendo ya mitume 8:9

Basi mtu mmoja jina lake Simoni alikuwa amefanya uchawi kwa muda mrefu katika mji huo akiwashangaza watu wote wa Samaria. Alijitapa kwamba yeye ni mtu mkuu, 10 nao watu wote wakubwa kwa wadogo wakamsikiliza na kumaka, wakisema “Mtu huyu ndiye uweza wa Mungu ujulikanao kama ‘Uweza Mkuu.’ ” 11 Wakamfuata kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake. 12 Lakini watu walipomwamini Filipo alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake.

"13 Simoni naye akaamini na akabatizwa. Akamfuata Filipo kila mahali, akistaajabishwa na ishara kuu na miujiza aliyoiona."

Hata waislamu uchawi wana utambua na unakatazwa ila wao kuna mstari mwembamba umewatenganisha kati ya dini uganga na uchawi. Wachache sana wanajitenga na uganga na uchawi ila upo na wengi wanautumia.

ukisikia mtu anasema ni uongo ujue huyo ndio mchawi wa kwanza,


"ni sawa mtu ukimwambia huna akili ni vigumu kuthibitisha lakini watu kwa kuona na kufikili huelewa kua huyu hana akili hata kama muhusika anakataa kuwa hana akili " hivyo kuuthibitisha uchawi kwa macho ya kawaida ni kazi kwa sababu umefichwa kama mtu asiye na akili "

Mungu ni mwema na Yesu ananguvu kuliko Miungu yote,Majina yote na anauwezo na nia ya dhati kutuonyesha njia ya uzima .

Amina muamini yeye ,mtafuteni yeye hata kama kila ukitubu na ukamkosea usione aibu bora ufe unamfata fata huwezi jua maana ana huruma na hutizama mioyo yetu.

Muwe na aman kwa Jina na neema za Yesu kristo wa nazareti.
 
Nadhani huko juu nilielezea vizuri/kuhusu sisi wanadamu kuwa tuna macho ya dhambi huenda sikueleweka,

Basi iko hivi binadamu yeyote anapozaliwa hupewa macho ya kuona kila kilichomo ndani ya dunia,kuhisi,kutambua hatari au mtu mbaya au kitu kibaya chochote,na ndo maana kupitia uwezo huo mtoto mchanga aonapo mchawi au jambo baya basi lazima aliyesana na hili hutokea sana pale mtoto anapolia mpaka mwili unapata joto au kutetemeka hapo mzazi jua mwanako anawaona wachawi na wanataka kumfanyia jambo baya.

Dini zetu zinatufundisha mengi lakini mfumo uliotumika ni mfumo wa mafumbo mno hvyo ili kuelewa kilichosemwa ni lazma umpate mchambuzi mzuri/mtafsiri mzuri akutafsirie na ndo maana mfano kwenye Quran unaweza kukuta shekhe anaijua yote lakini kwenye tafsri mtupu kabisa,

Mtoto yoyote azaliwapo,huja na neema na nguvu kubwa,hivyo huwa ni jukumu la wachawi kuhakikisha wanaichukua nguvu hyo ili wakaifanyie mambo yao na ndo maana kwenye dini watu tunaambiwa tuwatoe watoto wetu baada ya siku 40 nje,ma tena tukiwatoa basi tuchinje mbuzi mmoja kwa mwanamke au wawili kwa mtoto wa kiume hapa ni kwa upande wa waislam wakristo sjajua ikoje.

Wengi hawajui kwanini hutakiwa kuyafanya hivyo huenda wakaona ni kama utamaduni tu lakini ina maana kubwa sana,kwani wachawi wa ukoo wako au familia yako,pindi tu mtoto wako anapozaliwa jambo la kwanza kulifanya huwa wanahakikisha kuwa wanapata kitovu cha mtoto wako au kujua kimezikwa wapi.

Ndo maana wazee wetu zamani walihakikisha wanavificha mno vitovu vya watoto zao sehemu ambazo hakuna yeyote anayejua zaidi ya wao wawili (mama na baba) na wengi baada ya kukizika kitovu juu hupanda mti ambao hukaa mda mrefu,mfano mwembe,mbuyu n.k.

Je mzazi utajuaje kuwa kitovu cha mwanao kimebebwa?
jibu ni rahisi ni kwamba pale palipozikwa kitovu chako basi lazima kama kulipandwa mfano mgomba,basi ndani ya week tu lazma mgomba ule uanze kukua na hata kama eneo hilo halikupandwa kitu basi lazma kutoke majani au kipori kikubwa cha mda mfupi tu na kama itatoka ndizi basi hutumika kama chakula kwenye nyumba ambayo mtoto huzaliwa japo hili hufanywa siri kubwa.
 
1.Kwanini majini wanaitika kwa lugha ya kiarabu tuu?

2.Kwanini majini hasa wale mahaba inasemekana wanapotokea kwenye jamii yetu ya watu weusi hutokea kama waarabu?Je kwa jamii zingine wanatokeaje?

3.Kwa yale makafara yanayofanyika kwenye mibuyu ulaya wanafanyaje?

4.Kwanini aina za uchawi unatofautiana kutoka kabila moja mpaka lingine?
 
wewe utakua ni mchawi, wachawi ndio huwa wanatengeneza mazingira watu wasiamini kua uchawi upo na uongo ni kazi zenu.

Ufunuo 21:8

Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na madini ya kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili.”

Ufunuo 21:15

Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji.

Matendo ya mitume 8:9

Basi mtu mmoja jina lake Simoni alikuwa amefanya uchawi kwa muda mrefu katika mji huo akiwashangaza watu wote wa Samaria. Alijitapa kwamba yeye ni mtu mkuu, 10 nao watu wote wakubwa kwa wadogo wakamsikiliza na kumaka, wakisema “Mtu huyu ndiye uweza wa Mungu ujulikanao kama ‘Uweza Mkuu.’ ” 11 Wakamfuata kwa sababu kwa muda mrefu alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake. 12 Lakini watu walipomwamini Filipo alipohubiri habari njema za Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, wakabatizwa wanaume na wanawake.

"13 Simoni naye akaamini na akabatizwa. Akamfuata Filipo kila mahali, akistaajabishwa na ishara kuu na miujiza aliyoiona."

Hata waislamu uchawi wana utambua na unakatazwa ila wao kuna mstari mwembamba umewatenganisha kati ya dini uganga na uchawi. Wachache sana wanajitenga na uganga na uchawi ila upo na wengi wanautumia.

ukisikia mtu anasema ni uongo ujue huyo ndio mchawi wa kwanza,


"ni sawa mtu ukimwambia huna akili ni vigumu kuthibitisha lakini watu kwa kuona na kufikili huelewa kua huyu hana akili hata kama muhusika anakataa kuwa hana akili " hivyo kuuthibitisha uchawi kwa macho ya kawaida ni kazi kwa sababu umefichwa kama mtu asiye na akili "

Mungu ni mwema na Yesu ananguvu kuliko Miungu yote,Majina yote na anauwezo na nia ya dhati kutuonyesha njia ya uzima .

Amina muamini yeye ,mtafuteni yeye hata kama kila ukitubu na ukamkosea usione aibu bora ufe unamfata fata huwezi jua maana ana huruma na hutizama mioyo yetu.

Muwe na aman kwa Jina na neema za Yesu kristo wa nazareti.
Ni kweli umeongea
 
Nadhani huko juu nilielezea vizuri/kuhusu sisi wanadamu kuwa tuna macho ya dhambi huenda sikueleweka,

Basi iko hivi binadamu yeyote anapozaliwa hupewa macho ya kuona kila kilichomo ndani ya dunia,kuhisi,kutambua hatari au mtu mbaya au kitu kibaya chochote,na ndo maana kupitia uwezo huo mtoto mchanga aonapo mchawi au jambo baya basi lazima aliyesana na hili hutokea sana pale mtoto anapolia mpaka mwili unapata joto au kutetemeka hapo mzazi jua mwanako anawaona wachawi na wanataka kumfanyia jambo baya.

Dini zetu zinatufundisha mengi lakini mfumo uliotumika ni mfumo wa mafumbo mno hvyo ili kuelewa kilichosemwa ni lazma umpate mchambuzi mzuri/mtafsiri mzuri akutafsirie na ndo maana mfano kwenye Quran unaweza kukuta shekhe anaijua yote lakini kwenye tafsri mtupu kabisa,

Mtoto yoyote azaliwapo,huja na neema na nguvu kubwa,hivyo huwa ni jukumu la wachawi kuhakikisha wanaichukua nguvu hyo ili wakaifanyie mambo yao na ndo maana kwenye dini watu tunaambiwa tuwatoe watoto wetu baada ya siku 40 nje,ma tena tukiwatoa basi tuchinje mbuzi mmoja kwa mwanamke au wawili kwa mtoto wa kiume hapa ni kwa upande wa waislam wakristo sjajua ikoje.

Wengi hawajui kwanini hutakiwa kuyafanya hivyo huenda wakaona ni kama utamaduni tu lakini ina maana kubwa sana,kwani wachawi wa ukoo wako au familia yako,pindi tu mtoto wako anapozaliwa jambo la kwanza kulifanya huwa wanahakikisha kuwa wanapata kitovu cha mtoto wako au kujua kimezikwa wapi.

Ndo maana wazee wetu zamani walihakikisha wanavificha mno vitovu vya watoto zao sehemu ambazo hakuna yeyote anayejua zaidi ya wao wawili (mama na baba) na wengi baada ya kukizika kitovu juu hupanda mti ambao hukaa mda mrefu,mfano mwembe,mbuyu n.k.

Je mzazi utajuaje kuwa kitovu cha mwanao kimebebwa?
jibu ni rahisi ni kwamba pale palipozikwa kitovu chako basi lazima kama kulipandwa mfano mgomba,basi ndani ya week tu lazma mgomba ule uanze kukua na hata kama eneo hilo halikupandwa kitu basi lazma kutoke majani au kipori kikubwa cha mda mfupi tu na kama itatoka ndizi basi hutumika kama chakula kwenye nyumba ambayo mtoto huzaliwa japo hili hufanywa siri kubwa.
Je, wanaweza kuiba kitovu kilichofichwa ndani ya nyumba?
 
Back
Top Bottom