Uchambuzi wa nyota kila siku

Uchambuzi wa nyota kila siku

Utukufu wa sayari (ash-sharaf) unahusiana na:

Siku maalum ambayo sayari fulani inakuwa kwenye hali ya nguvu ya juu (exalted) inapopita kwenye nyota (buruj) fulani. Hii siyo tu kwa tarehe ya mwezi bali ni kwa daraja (degree) ya nyota hiyo katika anga la falaki.

Kwa mfano:

Zohali (Saturn) inakuwa kwenye utukufu (ash-sharaf) wake ikiwa kwenye daraja ya 21 ya nyota ya Mizani (Libra).

Mushtara (Jupiter) kwenye daraja ya 15 ya nyota ya Kaa (Cancer), nk.

Hivyo: Utukufu si lazima uwe tarehe hiyo hiyo kila mwaka kwenye kalenda yetu ya kawaida (Gregorian au Hijria). Kwa nini?

Sababu Kuu ni Kwamba:

1. Sayari huzunguka katika mizunguko yao ya kipekee (orbits) — kila moja ina kasi yake tofauti.


2. Kila mwaka, muda ambao sayari fulani inafika kwenye daraja ya utukufu unaweza kutofautiana, kwa sababu ya:

Mizunguko yao ni ya miaka, si miezi.

Kwa mfano, Saturn (Zohali) huchukua miaka 29-30 kuzunguka jua mara moja – hivyo haiwezi kufika kila mwaka kwenye 21° ya Libra.

Jupiter (Mushtara) ni kama miaka 12.

Zuhura (Venus) ni karibu miaka 8 kwa mizunguko kamili, nk.

Kwa hiyo

SI LAZIMA kila mwaka sayari husika ifike kwenye daraja ya utukufu wake. Kuna miaka inapita bila kufika hapo. Kuna mwaka mmoja inaweza kufika kwa mwezi huu, mwaka mwingine mwezi mwingine, au hata ikose kabisa mwaka mzima.


Mfano Halisi:

Mwaka huu 2025, unaweza kuona Jupiter haijafika kwenye daraja ya 15 ya Cancer – hivyo haipo kwenye utukufu wake mwaka huu. Lakini inaweza kufika mwaka 2027.

Wakati huo huo, Zohali inaweza kuwa karibu na 21° ya Libra, na hivyo utukufu wake unaweza kuwa halisi mwaka huu.

Kuhusu Tarehe za Kalenda

Tarehe kama “15 ya Cancer” au “21 ya Libra” si lazima zilingane na siku ile ile ya kalenda kila mwaka, kwa sababu:

Nyota (buruj) za falaki zinaanzia tarehe tofauti kila mwaka.

Tuna kalenda tofauti: ya Kiarabu (Hijri), ya Miladia (Gregorian), na kalenda ya falaki ya nyota.
Hivyo basi Utukufu wa sayari si wa kila mwaka kwa kila nyota.

Inategemea sayari yenyewe imefika kwenye daraja gani.

Tarehe uliyoandika ni ya kudumu kama “daraja ya utukufu”, lakini sio lazima kila mwaka tarehe hizo zilingane kwa kalenda wala zifikiwe na sayari husika.

Ili kujua kama sayari imefika kwenye utukufu wake mwaka huu, inabidi kuangalia ramani ya nyota (ephemeris) ya mwaka husika.
 
"Emphemeris ya mwaka husika"
asante sana ndugu.
kuna vitu ving umenifungua macho.
1.kwenye kitabu hcho niliona kila sayari na siku inazotumia kwenye mzunguko

2.pia naomba nijue nitapateje hiyo emphemisis ya mwaka.?
 
Hivyo basi Utukufu wa sayari si wa kila mwaka kwa kila nyota.

Inategemea sayari yenyewe imefika kwenye daraja gani.

Tarehe uliyoandika ni ya kudumu kama “daraja ya utukufu”, lakini sio lazima kila mwaka tarehe hizo zilingane kwa kalenda wala zifikiwe na sayari husika.

Ili kujua kama sayari imefika kwenye utukufu wake mwaka huu, inabidi kuangalia ramani ya nyota (ephemeris) ya mwaka husika.
Bro historia yangu naielezea kifupi, miaka mitano iliyopita nilikua na jamaa yangu kipindi hicho nasoma yeye yupo kitaa akanishawishi twende Kwa mganga kupata dawa ya mvuto Kwa madem, Cha ajabu yeye hakutumia hiyo dawa ila mimi niliimaliza yote( ya kuchoma na ya kuongea) , na tangu kipindi hicho nimekua mtu wa nuksi kila mara na mabalaa na nimekua nikitokewa na majinamizi mara kwa mara hasahasa kipindi kile nimetoka Kwa mganga, namba unisaidie tatizo linaweza ikawa ni nini
 
Bro historia yangu naielezea kifupi, miaka mitano iliyopita nilikua na jamaa yangu kipindi hicho nasoma yeye yupo kitaa akanishawishi twende Kwa mganga kupata dawa ya mvuto Kwa madem, Cha ajabu yeye hakutumia hiyo dawa ila mimi niliimaliza yote( ya kuchoma na ya kuongea) , na tangu kipindi hicho nimekua mtu wa nuksi kila mara na mabalaa na nimekua nikitokewa na majinamizi mara kwa mara hasahasa kipindi kile nimetoka Kwa mganga, namba unisaidie tatizo linaweza ikawa ni nini
Pole mkuu ulikutana na mganga ambae sio mzuri
 
"Emphemeris ya mwaka husika"
asante sana ndugu.
kuna vitu ving umenifungua macho.
1.kwenye kitabu hcho niliona kila sayari na siku inazotumia kwenye mzunguko

2.pia naomba nijue nitapateje hiyo emphemisis ya mwaka.?
Naam mkuu elim ya nyota n Pana sana mkuu kalibu darasani kama utaitaj utaenda kujifunza mengi zaid ya aya Niliyo kuchambulia apa
 
UNAIJUA NYOTA INAYOKUSAIDIA KIFEDHA?

Fuatana nami:::::::

(DOGOLI (Dr)


Kwenye masuala ya kifedha, hakuna mtu anayeweza akafanikiwa bila kuhitaji mtu wa kushirikiana naye.

Kiroho, kila mtu ana mshirika wake katika kila jambo ikiwemo masuala ya kifedha.

Usipoijua hii siri unaweza kujikuta unamshirikisha mtu kwenye biashara zako au mambo ya kifedha, badala ya kupiga hatua kwenda mbele unarudi nyuma kumbe tatizo ni huyo mtu uliyemshirikisha kwenye masuala yako ya kipesa!

Kuna Nyota ambayo haiendani kabisa na aina fulani ya biashara. Kwa mfano wewe nyota yako ni Aries na unafanya biashara ya kuuza vifaa vya umeme, gesi, mafuta nk, alafu ukamwajiri mtu au ukaingia kwenye business partnership na mtu wa nyota ya Samaki; uwe na uhakika kwamba hiyo biashara itakufa kwa sababu hawa watu hawana ushirikiano kabisa kiroho katika mambo ya fedha.

Aries (nyota ya Punda) anatakiwa aajiri mtu wa Nyota ya Taurus (Ng'ombe) kwa sababu wanaelewana sana na wana compatibility kubwa kwenye mambo ya fedha.

Gemini (nyota ya Mapacha) anatakiwa ashirikiane na Cancer (Nyota ya Kaa) kwenye mambo yahusuyo hela.

Cancer amshirikishe Leo (Simba)

Leo amwajiri Mashuke.

Mashuke --- Mizani

Mizani --- Mshale

Mshale --- Mbuzi

Mbuzi --- Ndoo

Ndoo --- Samaki

Inatakiwa iwe hivyo ili kupunguza hasara na lawama zisizo na sababu linapokuja suala la kumtafuta business partner.

Aidha, in case una uhitaji wa pesa, usiende kwa mtu ambaye hamna spiritual connection kwenye fedha, mwendee ambaye kiroho fedha zako ni zake na zake ni zako, yaani yule ambaye nyota zenu kifedha zinaendana.
Je, imewahi kukutokea mtu akaja kwako na hitaji la fedha ukamnyima alafu akaja mwingine mwenye hitaji hilo hilo ukajikuta huwezi kumnyima?
Au ukaenda kwa mtu unayemwamini atakusaidia au kukukopesha fedha akakunyima, alafu ukabahatisha tu kwa mtu usiyemdhania na akakupatia?
Ni kwa sababu ya mashirikiano baina ya Nyota zenu wala sio uganga au maombi!

Kuna kitu umeelewa?

Nishirikishe kwenye comment hapo chini .


Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi

DOGOLI (Phd) , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho
 
NYOTA YAKO LEO JUMATANO JULAI 23/2025:

UKIWA NA SHIDA YOYOTE YA KINYOTA NA TIBA, NIPO MOROGORO MJINI NAPATIKANA KILA SIKU OFISINI KWANGU FOREST KILEKA KUANZIA SAA 12 ASUBUHI MPAKA SAA 12 JIONI.

MAALIM ANAPATIKANA MUDA WOTE.



★SIMBA LEO 🦁 (Julai 23– Agosti 22)

Jamaa zako wako kàtika hali ya uhitaji kuwa karibu na wape misaada Leo utapokea maombi mengi ya watu kutaka kusaidiwa au kukopeshwa Shughulika suala la elimu na mahitaji ya mtoto Kuna jamaa yako wa karibu atakupa msaàda kama ukiuhitaji.

•Safari zako sio nzuri ingawa utaenda na kufika salama ila njiani maudhi mengi.

★MASHUKE– VIRGO ♍(Agosti 23– September 23)

Shughulika masuala ya nyumbani leo hakuko vizuri Kuna taarifa za magonjwa na kutokuelewana na wazee au viongozi Lipo jambo hujalifanyia kazi kama ulivyotakiwa litakuletea shida ikiwa utaendelea kudharau.

•Utapoteza kitu muhimu Leo na itakufikia habari mbaya ya huzuni au utashuhudia tukio la kukuhuzunisha leo Mungu akusimamie kwa yote.

★MIZANI– LIBRA ⚖️ (September 24– Oktoba 23)

Utapokea msaada mkubwa kutoka kwa mwenzio mahusiano mapya yatakuletea neema Leo uko kwenye nafasi nzuri ya kupokea mkopo uliouomba fuatilia utapata Utaingia makubaliano ya kupewa unachotaka siku nzuri kwa kujistarehesha na mwenzio Timiza ahadi ulizojiwekea zitakunufaisha siku zijazo.

•Kazi yako haitapokelewa vizuri na utalaumiwa au kupuuziwa na ikiwa unatafuta kazi kwa leo haijakaa vizuri upande wako ngoja upite muda kidogo au siku ya Leo ipite.

★NG'E– SCORPION 🦂 (Oktoba 24– November 21)

Acha tabia yako yako ya kulazimisha mambo leo kuwa mpole siku haijakaa sawa kwako Utajikutà unagombana na kuzozana na kila mtu chunga majibu yako yatakufikisha pabaya Usifanye mambo kwa haraka haraka au papara utapata tatizo ambalo litahitaji msaada Omba na utasaidiwa japo kwa uchache.

•Maswala yako ya kikazi yapo vizuri na utapata faida na wateja wapya kwenye biashara yako na kazini mwako wataongezeka marafiki wapya.

★MSHALE– SAGITTARIUS 🏹 (November 22– December 21)

Utapokea mgeni ambaye ni rafiki yako mkubwa kuna taarifa za mbali kutoka kwa mtu uliye anzisha nae mahusiano hivi karibuni Mipango yako inahitaji makubaliano ya maandishi siku nzuri kwa maelewano kwa waliohitilafiana Habari za ndoa na posa zitasogezwa mbele.

•Safari zako ni nzuri hazina shaka yoyote.

★MBUZI– CAPRICORN 🐐 (December 22– January 20)

Vizingiti vimekuwa vingi na leo usifanye jambo ambalo unategemea litakuletea faida Mafanikio yako yataanza kudidimia chukua hatua mapema leo utajikuta unagombana na mtu na utapata lawama na taarifa za ugonjwa.

•Utapata habari nzuri Leo na kuna mtu atakupa kitu kizuri kwa namna usiyoitarajia.

★NDOO– AQUARIUS 🏺 (January 21– February 19)

Tarajia kufifia au kuzorota mfumo wako wa biashara au kazi hii inatokana siku ya jana jumanne haukuifunga vizur watu walikuwekea husuda majira ya jion leo utapokea ujumbe utakao kupa matumaini na utaiona nuru kidogo.

•Kazi zako Leo zitakuwa nzito nzito na lawama nyingi juu yako ikiwa ni kazi mpya basi subiri siku ipite ndio uendelee na mipango hiyo na ikiwa ya zamani vumilia ni mapito tu.

★SAMAKI– PISCES 🐟 (February 20– March 20)

Mpangilio mpya katika shughuli zako utakuletea mafamikio una nafasi kubwa ya kufanya vizuri Biashara na kazi zitakuinua na kukujengea heshima katika jamii Leo utapata jukumu la kusimamia jambo na kupewa kitengo ukiongoze.

•Kazi zako zitaenda vizuri na mipango yako itaenda vizuri haswa ile mikubwa na yenye faida kwako.

★PUNDA– ARIES 🐏 (March 21– Aprili 20)

Siku ambayo utakuwa na pilika pilika za kushughulikia msuala ya kikundi au wanachama weka mkazo katika jambo hili Una nafasi kubwa ya kufanya vizuri utafanikiwa kupata marafiki wapya Ambao watakunyanyua usikose kuhudhuria mkutano utakao itishwa hivi karibuni.

•Siku yako leo itakuwa ya utulivu furaha na faraja zaidi haswa kwenye mahusiano yako ndoa yako au mapenzi yako mtu wako wa karibu atakufurahisha zaidi na anaweza kukupa moja ya vitu vizuri kwa namna usiyoitarajia au akakupa maneno ya faraja kwako.

★NG'OMBE– TAURUS 🐂 (Aprili 21– May 20)

Ule mtiririko wa mambo kwenda vizuri hauko kama inavyokuwa Kutakuwa na vikwàzo na kukwama tafuta msaada kwa wanaojua Kuna uadui unafanywa kukuvugia kazi na biashara zako hali ya ya kipato itaporomoka.

•Utapokea taarifa nzuri sana leo na mambo mazuri yatakutokea haja zako nyingi zitatimia na utafanikiwa.

★MAPACHA– GEMINI ♊ (May 21– Juni 20)

Rudisha mahusiamo mazuri kwa jamaa zako leo panga safari ya kukutana nao
Mpango wa kuanzisha shughuli yoyote ile kwa sasa hautakwenda vizuri iwapo hutamshirikisha ndugu au jamaa yako Leo utapata au kupokea kitu kipya ambacho kitakufurahisha kutoka kwa mtu wako wa karibu.

•Safari zako ni nzuri ila usiwahi utapata maudhi maudhi lakini utafika salama.

★KAA– CANCER 🦀 (Juni 21– Julai 22)

Utapata utakacho na utapokea pesa na taarifa za kupatikana kwa kazi uliyouwa unaitafuta Hali ya kipato itakuwa imenyooka fuatilia madai na stahiki zako.

•Leo uko kwenye nafasi nzuri ya kufanikisha malengo yako jihadhali na matumizi yâsiyo ya lazima Mpamgilio wa nyumbani uko vizuri kaa wazee kwa ushauri mzuri.

★★★★★★★★★★★★★★★
Kwa ushauri na mengineyo wasiliana na maalim,niwatakie siku njema na mafanikio mema

MAALIM DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️ MTABIRI WA NYOTA NA MTAALAM WA MAMBO MBALI MBALI YANAYO HUSIANA NA NYOTA ZENU.
IMG-20250629-WA0012(25).jpg
 
Jana rafiki yangu aliyetumwa na maadui zangu kaja kunichora na mimi nikamchora .

Leo ni mwendo wa mafanikio nitaenda kilabuni ,na hivi umesema kuna cheo nawezq kupewa natamani iwe hivyo haswa udiwani wanipe mimi huyu mpinzani ajitoe mwenyewe tu
 
Jana rafiki yangu aliyetumwa na maadui zangu kaja kunichora na mimi nikamchora .

Leo ni mwendo wa mafanikio nitaenda kilabuni ,na hivi umesema kuna cheo nawezq kupewa natamani iwe hivyo haswa udiwani wanipe mimi huyu mpinzani ajitoe mwenyewe tu
Ajitoe mwenyewe bila kutumia Ile 4-4-2 ya ubaya ubwela 🤪🤪😂🏃🏽‍♂️
 
MAFUSHO YA KILA NYOTA NA SIKU ZAO ZA BAHATI

(Dogoli kinyamkela 💀 ☠️ (Dr)


Kwa wale ambao mmeshajua nyota zenu na siku zenu za bahati ni muhimu sana kwa sasa, muanze kuzifusha/kuzisafisha nyota zenu ili mambo yenu yaanze kuweendea vizuri.
Hapa nimeweka nyota zote 12,
Ili kujiridhisha kuwa masomo haya mnayasoma, naomba mtu aniambie nyota yake ameiona namba namba ngapi na mafusho yake ni yapi,
Ahsante

1. PUNDA Aries ♈

Hii ni nyota ya kwanza katikati mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 21/3 hadi 20/4 ya mwaka wowote

Siku yao bahati ni Jumanne. Siku yao mbaya ni Jumanne usiku na jumatano mchana. Rangi yao ya bahati ni Nyekundu. Asili yao ni Moto. Namba yao ya bahati ni 9. Sayari yao ni Mars (Marikh).

Mafusho yao yanaitwa Qist, yako kama vijiti, yana rangi ya kahawaia. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuvuta bahati zako. Unachoma kati ya saa 12 - 1 asubuhi na saa 7 - 8 mchana. Kuomba matatizo yako uliyonayo nayo yaishe au kupata unachokihitaji kwa kumuelekea Mwenyezi Mungu.

2. NG'OMBE Taurus ♉

Hii ni nyota ya pili katika mlolongo wa nyota 12. Na nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 21/4 hadi 20/5 ya mwaka wowote,

Siku yao ya bahati ni Ijumaa. Siku yao mbaya ni jumamosi na jumatano usiku. Rangi yao ya bahati ni kijani. Asili yao ni Udongo. Namba yao ya bahati ni 6. Sayari yao ni Venus (Zuhura).

Mafusho yao ni ubani mashtaka, yapo kama vijiwe vidogo vidogo vyenye vumbi na vina rangi ya kijivu jivu. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuomba unayoyataka kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu. Muda wa kuchoma ni saa 12 - 1 asubuhi na saa 7 - 8 mchana.

3. MAPACHA Gemin ♊

Hii ni nyota ya tatu katika mlolongo wa nyota 12. Hii ni kwa waliozaliwa kati ya tarehe 21/5 hadi 21/6 ya mwaka wowote,

Siku yao bahati ni jumatano. Siku yao mbaya ni Jumanne usiku na jumatatu mchana. Rangi yao ya bahati ni njano na blue isiyoiva. Asili yao ni upepo. Namba yao ya bahati ni 5. Sayari yao ni Mercury (Utwaridi).

Mafusho yao ni Kachiri yako kama mauwa yaliyokauka na rangi yake ni kahawaia. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuomba unayohitaji kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu. Muda wa kuchoma ndio huo huo uliyotajwa kwenye hizo nyota za juu.

4. KAA cancer ♋

Hii ni nyota ya nne katika mlolongo wa nyota 12. Hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 22/6 hadi 22/7

Siku yao ya bahati ni jumatatu. Siku yao mbaya ni Jumanne mchana. Rangi yao ya bahati ni nyeupe. Asili yao ni Maji. Sayari yao ni Mwezi (kamari). Namba yao ya bahati ni 2 na 7.

Mafusho yao ni ubani maka huu ni maarufu sana au unaweza kutumia ubani wowote tu wa kawaida. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kama zilivyo hizo nyingine muda ni huo huo tajwa.

5. SIMBA LEO ♌

Hii ni nyota ya tano katika mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 23/7 hadi 22/9

Siku yao ya bahati ni jumapili. Siku yao mbaya ni Alhamisi mchana na jumatatu mchana. Rangi yao ya bahati ni njano au rangi ya dhahabu. Asili yao ni moto. Rangi yao ya bahati ni 1 na 4. Sayari yao ni jua. Hawa ni watu wenye matumizi sana ya pesa pia wanapenda matanuzi.

Mafusho yao ni Sandarus yako kama mawe yenye rangi ya njano. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kama tulivyoelekeza hizo nyingine.

ITAENDELEA...........


Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi

Dogoli kinyamkela 💀☠️ (Phd) , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho
 
MAFUSHO YA KILA NYOTA NA SIKU ZAO ZA BAHATI

(Dogoli kinyamkela 💀 ☠️ (Dr)


Kwa wale ambao mmeshajua nyota zenu na siku zenu za bahati ni muhimu sana kwa sasa, muanze kuzifusha/kuzisafisha nyota zenu ili mambo yenu yaanze kuweendea vizuri.
Hapa nimeweka nyota zote 12,
Ili kujiridhisha kuwa masomo haya mnayasoma, naomba mtu aniambie nyota yake ameiona namba namba ngapi na mafusho yake ni yapi,
Ahsante

1. PUNDA Aries ♈

Hii ni nyota ya kwanza katikati mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 21/3 hadi 20/4 ya mwaka wowote

Siku yao bahati ni Jumanne. Siku yao mbaya ni Jumanne usiku na jumatano mchana. Rangi yao ya bahati ni Nyekundu. Asili yao ni Moto. Namba yao ya bahati ni 9. Sayari yao ni Mars (Marikh).

Mafusho yao yanaitwa Qist, yako kama vijiti, yana rangi ya kahawaia. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuvuta bahati zako. Unachoma kati ya saa 12 - 1 asubuhi na saa 7 - 8 mchana. Kuomba matatizo yako uliyonayo nayo yaishe au kupata unachokihitaji kwa kumuelekea Mwenyezi Mungu.

2. NG'OMBE Taurus ♉

Hii ni nyota ya pili katika mlolongo wa nyota 12. Na nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 21/4 hadi 20/5 ya mwaka wowote,

Siku yao ya bahati ni Ijumaa. Siku yao mbaya ni jumamosi na jumatano usiku. Rangi yao ya bahati ni kijani. Asili yao ni Udongo. Namba yao ya bahati ni 6. Sayari yao ni Venus (Zuhura).

Mafusho yao ni ubani mashtaka, yapo kama vijiwe vidogo vidogo vyenye vumbi na vina rangi ya kijivu jivu. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuomba unayoyataka kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu. Muda wa kuchoma ni saa 12 - 1 asubuhi na saa 7 - 8 mchana.

3. MAPACHA Gemin ♊

Hii ni nyota ya tatu katika mlolongo wa nyota 12. Hii ni kwa waliozaliwa kati ya tarehe 21/5 hadi 21/6 ya mwaka wowote,

Siku yao bahati ni jumatano. Siku yao mbaya ni Jumanne usiku na jumatatu mchana. Rangi yao ya bahati ni njano na blue isiyoiva. Asili yao ni upepo. Namba yao ya bahati ni 5. Sayari yao ni Mercury (Utwaridi).

Mafusho yao ni Kachiri yako kama mauwa yaliyokauka na rangi yake ni kahawaia. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kuomba unayohitaji kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu. Muda wa kuchoma ndio huo huo uliyotajwa kwenye hizo nyota za juu.

4. KAA cancer ♋

Hii ni nyota ya nne katika mlolongo wa nyota 12. Hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 22/6 hadi 22/7

Siku yao ya bahati ni jumatatu. Siku yao mbaya ni Jumanne mchana. Rangi yao ya bahati ni nyeupe. Asili yao ni Maji. Sayari yao ni Mwezi (kamari). Namba yao ya bahati ni 2 na 7.

Mafusho yao ni ubani maka huu ni maarufu sana au unaweza kutumia ubani wowote tu wa kawaida. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kama zilivyo hizo nyingine muda ni huo huo tajwa.

5. SIMBA LEO ♌

Hii ni nyota ya tano katika mlolongo wa nyota 12. Nyota hii ni kwa wale waliozaliwa kati ya tarehe 23/7 hadi 22/9

Siku yao ya bahati ni jumapili. Siku yao mbaya ni Alhamisi mchana na jumatatu mchana. Rangi yao ya bahati ni njano au rangi ya dhahabu. Asili yao ni moto. Rangi yao ya bahati ni 1 na 4. Sayari yao ni jua. Hawa ni watu wenye matumizi sana ya pesa pia wanapenda matanuzi.

Mafusho yao ni Sandarus yako kama mawe yenye rangi ya njano. Unachoma kwenye siku yako ya bahati kama tulivyoelekeza hizo nyingine.

ITAENDELEA...........


Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi

Dogoli kinyamkela 💀☠️ (Phd) , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho
Tunasubiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom