Uchaguzi wa Senegal 🇸🇳 umenifanya niwaelewe vizuri Vijana wa hapa Nchini

Pantosha

JF-Expert Member
Sep 22, 2022
347
462
Bila shaka sisi wapenda siasa tunajua kuwa kuna kijana mwenye umri wa miaka 44 ambaye anaweza kuibuka mshindi katika uchaguzi wa urais huko Senegali.

Mitandaoni watu wanajadili kuhusu umri na uongozi wa nchi. Kutokana na assessment yangu ya haraka huko mitandaoni, nimeona kuwa vijana hawako tayari kuongozwa na vijana. Sababu kubwa zikiwa ni 1) hofu ya viongozi vijana kuweza kubadili katiba ili waendelee kukaa madarakani, 2) kutokuwaamini vijana kwa sababu hawana uzoefu, 3) wasiwasi kuwa vijana wanaweza kulewa madaraka.

Sababu hizo ni za msingi ila nasikitika kuona kuwa zinatolewa na vijana wenyewe. Hapo ndiyo naelewa kwa nini vijana wengi hawajitosi kwenye siasa na wachache waliopo wanaishia kuwa chawa na wachumia tumbo.

Ikiwa vijana wenyewe hawajiamin, hata wazee hawawezi kutuamini. Nadhani hii ndiyo sababu hata mzee akistaafu anapewa tena extension ya mkataba coz hakuna vijana wanaojiamini.

Katika kampeni zake FAYE alisema wao wanahitaji mageuzi makubwa na kuwa wazee waliopo wameshindwa kwa kiasi kikubwa.

Ikumbukwe kuwa vijana wawili walijitokeza kuwania nafasi ya juu zaidi katika nchi yao (Senegal).

1. BASSIROU D. Faye (Jinsia: Me Umri: 44)

2. ANTA B. Ngomu (Jinsia Ke, Umri: 39).

IMG_5018.jpeg
 
Chadema inaongozwa na mzee, tena kimuonekano tu anaonekana ameshachoka na mikiki mikiki ya kuongoza chama cha aina ya Chadema.

Ukitoa wazo kwamba huyo mzee ameshakaa muda mrefu uongozini sasa awapishe vijana waongoze chama. Utaona fasta chawa wake ambao wengi wao ni vijana hapa mtandaoni wakim defend boss wao kuwa hatakiwi kuachia uongozi wa chama hicho, kwani akifanya hivyo atakosekana mtu mungine wa kuongoza (wakiwemo vijana wenyewe)

Sasa huu ndio utamaduni uliojengwa hapa nchini kuwa ni bora mtu afie juu ya uongozi wa chama akiwa na miaka zaidi ya 70 au 90 kuliko kutoka na kumuachia kijana wa miaka 30 au 40 aongoze chama au taasisi yoyote ya serikali nk.
 
Chadema inaongozwa na mzee, tena kimuonekano tu anaonekana ameshachoka na mikiki mikiki ya kuongoza chama cha aina ya Chadema.

Ukitoa wazo kwamba huyo mzee ameshakaa muda mrefu uongozini sasa awapishe vijana waongoze chama. Utaona fasta chawa wake ambao wengi wao ni vijana hapa mtandaoni wakim defend boss wao kuwa hatakiwi kuachia uongozi wa chama hicho, kwani akifanya hivyo atakosekana mtu mungine wa kuongoza (wakiwemo vijana wenyewe)

Sasa huu ndio utamaduni uliojengwa hapa nchini kuwa ni bora mtu afie juu ya uongozi wa chama akiwa na miaka zaidi ya 70 au 90 kuliko kutoka na kumuachia kijana wa miaka 30 au 40 aongoze chama au taasisi yoyote ya serikali nk.
nzuri sana hii
 
Usitizame ujana kwa namba/miaka ya umri peke yake, ukiona nchi inapata Rais kijana km huko Senegal fahamu kwamba upo msingi imara unaowaandaa vijana kwa majukumu mbali mbali..ya kifamilia, ya kiraia, ya kiimani, ya kiuongozi nk..mfano waangalie Senegal na timu yao ya taifa, hawana timu kubwa ngazi ya klabu km zilizopo hapa simba, yanga, azam nk lkn wana timu bora kabisa ya Taifa na inafanya vizuri! Sabab ni nini..

WANAANDALIWA, maandalizi yako wapi? Ngazi ya familia na elimu ya darasani, maandalizi yao yanafanikiwa kuondoa au kupunguza tabia hasi za asili zinazotokana na ukoo, kabila, itikadi za vyama au hata imani na kuwafanya wawe tayari kutumika kwa majukumu mbali mbali kwa faida ya nchi yao...kijana wa Senegal hawezi kuwa sawa na kijana wa Tanzania hata kama wanalingana kwa umri! Tofauti ni MAANDALIZI kwa ajili ya majukumu kwa nchi na watu wake!
 
Usitizame ujana kwa namba/miaka ya umri peke yake, ukiona nchi inapata Rais kijana km huko Senegal fahamu kwamba upo msingi imara unaowaandaa vijana kwa majukumu mbali mbali..ya kifamilia, ya kiraia, ya kiimani, ya kiuongozi nk..mfano waangalie Senegal na timu yao ya taifa, hawana timu kubwa ngazi ya klabu km zilizopo hapa simba, yanga, azam nk lkn wana timu bora kabisa ya Taifa na inafanya vizuri! Sabab ni nini..WANAANDALIWA, maandalizi yako wapi? Ngazi ya familia na elimu ya darasani, maandalizi yao yanafanikiwa kuondoa au kupunguza tabia hasi za asili zinazotokana na ukoo, kabila, itikadi za vyama au hata imani na kuwafanya wawe tayari kutumika kwa majukumu mbali mbali kwa faida ya nchi yao...kijana wa Senegal hawezi kuwa sawa na kijana wa Tanzania hata kama wanalingana kwa umri! Tofauti ni MAANDALIZI kwa ajili ya majukumu kwa nchi na watu wake!
Akibisha arudi darasani. Kuna nchi moja huko kusini mwa Kenya vijana wao wana andaliwa kuwa MACHAWA na sasa aliye andaliwa kuwa chawa anawaunga mkono kuwa wako vizuri.
 
Sijakimbia! Ni kweli umeandika vizuri. Binafsi huwa nasema Mbowe anatakiwa kupisha wengine waongoze. Pia nilitoa pongezi kwa ZZK kwa kupisha wengine waongoze.
Kupisha ndio nini? Hiyo gharama anayoibeba Mbowe kuwa Mwenyekiti unaona kuna kijana CHADEMA anaweza kuibeba? gharama kwa maana ya madhila anayopata na familia yake...
 
Kupisha ndio nini? Hiyo gharama anayoibeba Mbowe kuwa Mwenyekiti unaona kuna kijana CHADEMA anaweza kuibeba? gharama kwa maana ya madhila anayopata na familia yake...
Unaposema hakuna kijana, hiyo ndiyo shida yenyewe.
 
Back
Top Bottom