Uchaguzi Serikali za Mitaa 2014: Matokeo kutoka nchi nzima (TZ Bara)

Salasala kata ya Wazo Dar Chadema imeshinda kwa zaidi ya kura 700 dhidi ya 400 za ccm. Kwenye uchaguzi huo kulikuwa na vituko mbalimbali vilivyofanywa na CCM, wakati wa kuhesabu kura CCM walipoona wamedondokea pua walijipanga kupora ushindi kwa kuleta fujo. Walivurumisha mawe kwenye ofisi iliyokuwa inatumika kuhesabu kura, Makamanda wa chadema waliokuwa nje walifuatilia tukio hilo na na Kulikuta gari aina ya ESCUDO lililokuwa na mawe baada ya kushtukiwa walitoka mbio ndiyo ikawa usalama wao. Pia siku moja yaani usiku wa kuamkia tarehe 14/12/2014 kama saa nane usiku hivi makamanda wa chadema waliwakamata wazee sita waliokuwa wakipiga kamapeni na kugawa rushwa. Wazee watatu walifanikiwa kutoroka na watatu kudhibitiwa. Walipelekwa kwenye kituo cha polisi cha Wazo lakini mkuu wa kituo hicho afandde Paulo aliweza kuwaachia na kuwashauri wakalale ili kesho yake wakashiriki uchaguzi kwa amani. Katika sekeseke hilo chadema ilifanikiwa kunasa nyaraka muhimu za kuhujumu uchaguzi huo. Chadema salasala wanaamini kwamba kwa kupata nyaraka hizo chadema iliweza kudhibiti uharama kwa 100%. Hongereni sana Makamanda wa Chadema Salasala.

Maeneo mengine chadema iliposhinda ni Wazo, Ndumbwi, Mbezi chini, jogoo, kinzudi.
Eneo la Kilimahewa juu uchaguzi uliharibika baada ya mawakala wa CCM kuleta vurugu na kusababisha mtendaji kukimbia.

Kwa hiyo matokeo ya kilimahewa baada ya vurugu wameyatangaza au yatarudiwa? Vurugu inapelekea uchakachuaji.
 
Kwa matokeo mliyo yapata nawapongeza mno!
Mjitahidi sasa kujitanua wilaya za mikoa mbali mbali tz! Tutawaunga mkono!
 
Mitaa ya kimara kuna GAMBA 1 liliwekeza elf 5 kwakila mwanach aliepita karibu na kwakua ana Ukumbi wa Sherehe aliwadanganya kwamba kila mwananchi mwenye sherehe atatumia bure UKUMBI watu walishtukia hizo hadaa...walikula elf 5 J2 wamemfanya kitu mbaya hadi muda huu nnavyooandika huyo mwanadam yuko Hospt amelazwa kwa pressure jamaa wa GWANDA walikuwa wanajipongeza na KINANA zakutosha.....!

ni mtaa wa mavurunza jamaa anaitwa malima na ukumbi wake ni G5!!vijana wamemfanya kitu mbaya,kula ccm kura cdm
 
Majimoto CDM wamechukua vijiji vyote,vitongoji 4 kati ya 6,kata ya ikuba CDM waibuka kidedea,Lunguya, mbede,mabambasi,chamalendi na usevya,milumba,ilalangulu kote huko ni ushindi kwa CDM. Isipokuwa kibaoni kata anapotokea mtoto wa mkulima CDM hawajfanya vyema....
Mpka kieleweke awamu hii.
 
hayo ni mafanikio makubwa san kwa CDM, je ccm walikuwa na mitaa mingapi ktk serikali za mitaa ilipita? je ni ccm au cdm kaongeza mitaa? CDM hufahamika arusha ilikuwa kwa ngazi ya udiwani na ubunge lkn leo hii tunagawana mitaa pasu pasu that is big score! Kwa karatu ndo balaa maana kuna baadhi ya vijiji kwa mfano kuna kijiji cha Bashay Karatu yenye wajumbe 25 wote ni wa CDM yaan ccm hakuingia hata moja kwenye serikali ya kijiji.

Hivi miss world Imepita?:confused::confused:
 
KOTE MASIALA. IVI MMEWASIKIA WA BUKOBA??? HUWA NINAWAKUBALI SANA HAWA JAMAA. NASHAURI MITAANI HUKO MZIFUNGE KABISA OFISI ZA CCM MPAKA WARUDISHE ELA ZETU WALIZOIBA. ONGERWNI Bkb
 
Back
Top Bottom