Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

Hivi huyu meya KIMBISA aliwahi kuongoza nini na kwa mafanikio gani kabla ya nafasi hii.
ni aibu kuwa meya wa jiji kama dar halafu huna ubunifu wowote hata wa kuelekezwa jinsi gani kuboresha huduma zake.
Jamani naomba hii nafasi ipigiwe kura na WAKAZI WOTE WA DAR na wagombea nafasi wawe watu makini katika kuleta mabadiliko. SI LAZIMA MGOMBEA UMEYA AWE DIWANI, TUBADILI TARATIBU TUSONGE MBELE.

Hivi haya mabango yanayowekwa mjini kila kona bila mpangilio ndio nini?

Najua jiji wanataka kukusanya revenues lakini naona sasa yataanza kusababisha ajali barabarani. Hivi kwa nini wasiweke standards na kuwalazimisha kuweka dimensions zinazoeleweka na zaidi ya hayo kuwauliza local councils na wananchi kabla hawajaweka residential areas
 
Haswa,
mimi simjui Kimbisa kwa undani ila labda ni kwa kuwa utendaji wake hauonekani au ni kwa kuwa tuko bize na ufisadi.
Ila matangazo yanakera,
pia kuna haya ya vitambaa, muda wake ukipita, asipokuja mtu kulitumia kama dasta litaishia hapo hapo, ni nani wa kusimamia uwekwaji na utolewaji wake?
pamoja na yote jiji limerudia uchafu wake wa asili, hawa wamama wa kufagia wako very selective na takataka, nyingine wananabeba nyingine wanaacha,
m
MJI MCHAFU,
NENDENI MOSHI MKAPATIWE SEMINA.
Mlivyoenda Arusha kuona utendaji wao mlijifunza kitu? au mlishangaa na kurudi bila agenda za kubalisha utendaji wenu?
inatia aibu.
 
Kama ni suala la kutafuta revenue, nasikia shughuli ya kutoza ushuru wa parking jijini DSM ameachiwa mtu mmoja. Jiji wangeifanya shughuli hiyo bila shaka wangelijiingizia mabilioni kwa mwaka.
 
Kama ni suala la kutafuta revenue, nasikia shughuli ya kutoza ushuru wa parking jijini DSM ameachiwa mtu mmoja. Jiji wangeifanya shughuli hiyo bila shaka wangelijiingizia mabilioni kwa mwaka.
Kapewa mwekezaji mzalendo! Halafu nasikia jamaa wanasumbua sana na minyororo yao... Dar ilianza kuwa safi lakini nowadays inarudi kulekuleee...
 
Jiji ni ufisadi juu ya ufisadi ukichungulia report zao wanavyo zieleza utasema tumepiga hatua lakini in reality ukitoka nje na kuangalia kisha kufanya tathmini utaishia kuguna tu.
Huyu Meya pamoja na Mkuu wa Mkoa wanajisifia kila mala wanatengeneza barabara za mitaani kila mala wanaonyesha mfano barabara moja ya Gerezani hata 5km hazijafika lakini ndo hiyo kila kukicha wanajisifia uliza wametumia mabilioni mangapi hapo?Utaishia kukuna kichwa.
Huyu Mkuu wa mkoa anaulizwa pesa za mchango wa shule watu tulizo changia anakuwa mkali tuonyeshe madarasa yaliyo jengwa anaishia kufoka.Hivi ni kweli hatuna haki ya kuhoji matumizi ya pesa zetu tulizo changia?watu wamechangia mamilioni lakini sijui zimeishia wapi hata madarasa huko Chanika na kungineko sidhani kama zimejengwa!
Hii ni Tanganyika usanii kila sector hadi kwenye kuzoa taka nako usanii mtupu,utoaji wa tender nao ni usanii mtupu watu wanavifaa vya kisasa wanatoswa.Hii kujuana itatufikisha mahala tusipo kujua.
 
Haya ya Mabango nadhani hayako JIJI, yako kwenye MANISPAA zetu tatu. Kimbisa ni MWANAMTANDAO maarufu kupitia kwa mama Regina, ni "shemeji" wa EL. Nadhani bado pia ni katibu wa RED CROSS(T). Kapata vijisenti vya Wakimbizi kule kaingia siasa.
 
Ni kweli kabisa haya mabango yamekuwa uchafu ktk jiji letu.
walipokuwa wanakata miti pale Morocco kwenye ukuta sijui wa Tanesco ule sikujua ni kwa sababu gani lakini baada ya muda nikaona ujezi wa mabango unaendelea , sasa najiuliza yaani haya mabango ndo yafanye miti zaidi ya mitano ikatwe ili hayo matangazo ya kwenye mabango yaonekane???????? ama kweli hili jiji. pale si bure lazima kitu kidogo kilipita kwa manispaa au jiji.
 
Kimbisa ameshindwa kuendesha jiji. hata Mkurugenzi Kingobi naye sijui anafanya nini kwa sababu kwa kiasi kikubwa jiji linaendeshwa kwa amri kutoka kwa wakubwa. Suala la usafi mpaka aseme PM, msongamano wa magari alisema Lowassa, naamini hata hilo la Mabango, akisema mkuu mmoja huko juu, yatafanyiwa kazi mara moja
 
Hivi haya mabango yanayowekwa mjini kila kona bila mpangilio ndio nini?

Najua jiji wanataka kukusanya revenues lakini naona sasa yataanza kusababisha ajali barabarani. Hivi kwa nini wasiweke standards na kuwalazimisha kuweka dimensions zinazoeleweka na zaidi ya hayo kuwauliza local councils na wananchi kabla hawajaweka residential areas

2. Uwekaji wa mitaro ya wazi ili hali kuna mchanga kwenye maeneo ya waenda kwa miguu, matokeo yake ni mitaro kujaa michanga na kuziba.

3. Usafishaji wa mitaro

4. Ufagizi wa barabara sanasan kuondoa michanga.

[Tafadhali wakuu ongezeni mengine na uchafu yanayowakera wakazi wa jiji]

Kikubwa cha msingi, ni sisi wakazi wenyewe kuwa wasafi.Kila kona Dar ni uchafu tu tena uchafu wetu sisi wakazi wenyewe.mtu anakunywa maji na kutupa kiroba au chupa popote pale.

Sisi wakazi wa Dar ni wachafu wa kutupwa, tubadilike.
 
PP Hakuna sehem safi bila usimamizi, serikali au manispaa lazima isimamie....mtu atakae tupa taka Order si IPO?...nani wa kufuata order ikiwa wakuu wenyewe mafisadi...
 
Watendaji wakitekeleza majukumu yao, hao wanaotupa takataka hovyo watawajibishwa.
 
Kama kuna suala ambalo linakera pia ni uchafuzi wa mazingira. Sio kwamba huwa ni kero tu, lakini uchafu huleta magonjwa mbali mbali na hatimae vifo ambavyo mara nyingi ni vya kujitakia. Na mara nyingi itokeapo hivi..msemo wa “Ni mapenzi ya Mungu” hutumika. Mimi sidhani ni sahihi wakati Mungu alitupa akili na vipawa mbali mbali ili tuishi maisha bora. Na ni Mungu wa Upendo na Rehema, sio wa kuangamiza.

Nina pendekezo, kwa nini kampeni kabambe isianzishwe ili kuweka nchi katika hali ya usafi, tukianzia vitongojini, wilayani hatimae mijini.
Ninachopendekeza ni vyombo vya habari i.e "Radio, Magazeti na Television” vitumike katika kuutangazia UMMA katika kudumisha usafi wa mazingira.
Mfano kama ni Radio kila siku, zijitolee kutoa matangazo ya bure kwa dakika moja tu, na iwe angalau mara tano kwa siku. Vitoe ujumbe unaoeleweka mfano “USITUPE TAKA OVYO, UTAOKOA MAISHA YA KWAKO, BABA, MAMA AMA ndugu yako yoyote” au ujumbe wowote ule utakaomgusa atakayesikia. Na magazeti na television vivyo2. Ninaamini hili likitenda ndani ya mwaka mzima tutaona mabadiliko sana katika mazingira tunayoishi. Tena sasa hivi mikoa mingi ina Radio stesheni, hii itatia msukumo sana ks at least ujumbe utagusa sehemu nyingi.

Ila Kampeni hizi zinatakiwa ziambatane na vitendea kazi, I mean mapipa ya taka kuwa sehemu mbali2. Viwanda vinavyotengeneza vyombo vya plastic, kwa nini visitengeneze yale mapipa ya taka ya plastic kama yanatengeneza basi upatikanaji wake uwe rahisi na bei rahisi kama “ndoo” au “beseni” unapozikuta katika maduka mengi. Watengeneze pia mifuko mikubwa ya plastic inayopatikana kwa urahisi kama vile ipatikanavyo mifuko midogo. Sidhani kama upatikanaji wa haya mapipa ukiwa rahisi, mtu atathubutu kuiba. Kampeni ikishaanza ina maana kutakuwa na mapipa ya taka sehemu nyingi, serikali then iweke mikakati aidha za kuongeza tender za sekta binafsi kuhakikisha takataka zinachukuliwa mara kwa mara na kwenda kutupwa dampo.

Hali ilivyo sasa INAKERA, mfano barabara ya Ali Hassan Mwinyi utakuta wakina mama wako busy wanafagia barabara. Lakini ks watu hawana hulka ya usafi , mara nyingi nimeshahudia niko nyuma ya gari tena yenye nakshi..haitachukua dakika 2 utaona chupa ya maji n.k imerushwa nje ya dirisha. Daladala ndio kabisa usiseme, upande huu viplastice vya maji vinarushwa, the other side mifuko ya plastic n.k. “Hivi ni kwa nini mtu asiuhifadhi uchafu wako uje utupe kwenye pipa la taka unapofikia mwisho wa safari yako”???. Halafu utastaajabia mtu huyu huyu akipita sehemu yenye rundo la uchafu, utamsikia mhhh!!! Aisee mji mchafu hadi unatia kinyaa. Amejisahau kuwa yeye kurusha kitu nje ya dirisha ni kuanzisha mrundikano wa uchafu usio wa lazima. Yeye atatupa, mwingine atatupa baada ya wiki mtaa hauelezeki..takataka kila sehemu, na harufu juu..Sasa hapo kweli tunategemea kuokoa afya zetu???. Sasa sio mitaa yote husafishwa kama Ali hassan Mwinyi. Mitaani uchafu unatupwa tu, hatimae mifereji yote inajaa uchafu..Ije mvua sasa..ndio balaa ..mifereji yote imeziba. Halafu tunaanza kulaumu, kumbe source ni ile mimi na wewe kutupa chupa ya maji na mfuko wa plastic n.k. Je kwa namna hii tutapona…???

Maoni binafsi, wahusika kama mnasoma humu please serikali ilisisitize hili kwa sababu ikifanikiwa kubadilisha MINDSET ya mtu ya kutotupa uchafu ovyo…mabadiliko yatakuwa makubwa sana. Hatuna miundo mbinu wala settlements za kuvutia sana basi tujitahidi tuwe na mazingira safi.

Mimi hainiingii akilini, mfano jijini DAR kuna mipango ya kuweka mabasi yaendayo kwa kasi, au uporomoshaji wa vikwangua anga wakati sanitation ni mbovu….Ukweli badala ya kupendeza mji utaonekana ni “CHAOS”.
Kwa kumalizia, badala ya kukazana kuwapa kampuni binafsi tenda za kusafisha jiji, mkazo utiliwe pia katika kubadilisha MINDSET za watu ili waweze kuwa na hulka ya usafi, na jinsi ya kufanya hivyo dawa yake ni “KAMPENI TU” likewise kampeni za utumiaji Condom. Au sivyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.


Samahani its a long article, lakini in short mimi binafsi "UCHAFU HUNIKERA SANA" na madhara yake ni mabaya wakati solution za kucontrol uchafu zipo nyingi....
 
MissKitim nakuunga mikono na miguu. Hakuna tabia inayonikera kwa kuanzia, kama kutupa uchafu ovyo, mfano mtu anatupa chupa/mifuko ya plastick kutoka kwenye gari.

Ilikuwepo kampeni ya kuhakikisha kuwa kwa mfano mabasi yote yaendayo mikoani yanakuwa na dust bins kwa ajili hiyo, lakini sina hakika kama polisi wetu wanacheki hilo au wako bize na yale mambo mengine. NEMC walilauch kampeni kama hii.

Ukiangalia hifadhi ya mikumi wanatumia gharama kubwa kusafisha kila mara kutokana na uchafu unaotupwa na wasafiri mbali mbali wapitao kule.

nadhani kuna haja pia ya kufanya hima sheria ili watakaoainika wafikishwe kizimbani iwe mfano kwa wengine kwa sababu sheria ipo, sema haisimamiwi ipasavyo.

Mji wowote ule ni usafi kama sio msafi basi hata uwe na majengo mazuri kiasi gani haileti maana!
 
Yaani Kaizer hapo umenena, wengi hatuna hulka ya usafi..inasikitisha.
na mie nimeshaona baadhi ya watu unakuwa nao for them ni norm kabisa kutupa takataka popote pale. Ukimuuliza kwa nini usishikilie huo uchafu ukatupa sehemu yenye bin, anadai mbona hapa pako okay..au ndio safarini anadai aah huku mbona ni porini....sasa imagine wangapi wana fikra hizo??

Halafu watu hawafikirii magonjwa yatokanayo, mfano yanayosababishwa na hewa chafu au kula vyakula vichafu simply ks ya uchafu uliozagaaa...Mfano Cholera kila mwaka inachukua ndugu zetu wengi lakini bado hatujifunzi

Mfano dar....yaani mitaaani mji ni mchafu kwa kweli...achia hiyo Ali H mwinyi inayofagiliwa kila siku. Halafu utashuhudia kilele cha uchafu huo siku mvua inyeshe..masaa 2 tu mfululizo..mifereji yote inaziba...

Kampeni dhidi ya uchafu wa mazingira ndiyo inayohitajika kwa sasa kubadilisha "Mindset za watu" kuwa its not norm kutupa takataka popote pale...iende sambamba kama kampeni za matumizi ya Condom...media zijitolee tu kuporomosha haya matangazo bure kwa manufaa ya wote

Vile vile kama unavyosisitiza kampeni zikianza basi na adhabu ziwekwe za wanaochafua mazingira...

Bora kuwa na nyumba za nyasi lakini mazingira yawe safi kuliko vice versa.
 
Yaani Kaizer hapo umenena, wengi hatuna hulka ya usafi..inasikitisha.
na mie nimeshaona baadhi ya watu unakuwa nao for them ni norm kabisa kutupa takataka popote pale. Ukimuuliza kwa nini usishikilie huo uchafu ukatupa sehemu yenye bin, anadai mbona hapa pako okay..au ndio safarini anadai aah huku mbona ni porini....sasa imagine wangapi wana fikra hizo??

Halafu watu hawafikirii magonjwa yatokanayo, mfano yanayosababishwa na hewa chafu au kula vyakula vichafu simply ks ya uchafu uliozagaaa...Mfano Cholera kila mwaka inachukua ndugu zetu wengi lakini bado hatujifunzi

Mfano dar....yaani mitaaani mji ni mchafu kwa kweli...achia hiyo Ali H mwinyi inayofagiliwa kila siku. Halafu utashuhudia kilele cha uchafu huo siku mvua inyeshe..masaa 2 tu mfululizo..mifereji yote inaziba...

Kampeni dhidi ya uchafu wa mazingira ndiyo inayohitajika kwa sasa kubadilisha "Mindset za watu" kuwa its not norm kutupa takataka popote pale...iende sambamba kama kampeni za matumizi ya Condom...media zijitolee tu kuporomosha haya matangazo bure kwa manufaa ya wote

Vile vile kama unavyosisitiza kampeni zikianza basi na adhabu ziwekwe za wanaochafua mazingira...

Bora kuwa na nyumba za nyasi lakini mazingira yawe safi kuliko vice versa.

wakati mwingine wanasahau kuwa watu wengi zaidi wanafariki kutokana na magonjwa yatokanayo na uchafuzi wa mazingira au kutozingatia usafi, kwa mfano malaria, kipindupindu, kuharisha nk. wao wamekazania tu 'dume kondomu' wanaacha mambo mengine ya msingi!
 
Huwa najiuliza kuwa yote yasemwayo juu ya uchafuzi wa mazingira ni kwamba binaadamu hawaelewi, au ni kwamba hizi ni porojo tu zisizo na msingi wowote hasa kwa jamii ya Kitanzania hususan wakazi wa Dar es salaam?

Ndugu wana Jamiiforums ni mengi yanasemwa kuhusu kuto-haribu mazingira na athari zake kwa viumbe kama mazingira yakicharuka, lakini hatua zinazochukuliwa na wanajamii mmoja mmoja juu ya utunzaji naona kama haitoshelezi.

Ilishawahi kusemwa kwamba hali ya ukame unaojitokeza katika maeneo mengi ni moja ya athari za uchafuzi wa mazingira, vivyo hivyo kwa ongezeko la joto na majanga mengine ya kimaumbile. Kwa wale wanaofuatilia utabiri wa hali ya hewa luningani watakubaliana nami kwamba maeneo mengi ambapo hapo kabla yalikuwa yakisifika kwa hali nzuri isiyo ya joto kama Kilimanjaro sasa hali ni tofauti.

Pengine wengi hujitetea kwamba kuzuia uhalibifu wa mazingira kama kutochoma mkaa na kuchimba mchanga ni vigumu kwakuwa kutazuia shuhuli za wengi kujipatia kipato ukizingatia kwamba watanzania ni maskini, lakini kilichonipelekea leo hii kuandika thread hii ni tabia mbaya ninayojionea ya wakazi wa mijini hasa Dar es salaam ya kutojali mazingira yetu isiyohusiana na hali ya umaskini. Mimi naamini kuwa mambo mengine tufanyayo si sababu ya umaskini wa kipato bali ni umaskini wa akili.

Utalikuta jitu (sasahivi msimu wa machungwa) linatembea barabarani huku linakula chungwa halafu maganda linatupa chini bila kujali kitu chochote (tembelea maeneo yote yenye meza ya muuza machungwa jirani), au jingine limo ndani ya gari, linakunywa maji halafu chupa linatupa barabarani... hii akili kweli??.

Ukizunguka mitaani ni rahisi kukuta mtu amejibanza ukutani au kwenye mti anakojoa na wengine wanathubutu hata kuvua suruali na kunya katika sehemu hizo...... sasa najiuliza kama kweli wewe ni maskini na umeshindwa kuraise hata sh100 kwa siku ya kwenda kujisaidia Public toilet sasa una haja gani ya kuendelea kuishi mjini..si bora urudi shamba.

Nimeshawahi kuishi miji ya Pretoria, Bloemfontein, Capetown na Gabarone mazingira yao ni safi hadi inatia raha. Hata pate Parktown (Johannesburg city centre) penye msongamano wa watu mkubwa kuliko hata Kariakoo mazingira ni safi sana.

Hivi kweli sababu ni umaskini wa kipato au ukosefu wa akili? (umaskini wa akili).
Wewe mwana-Jamiiforums ukiwa kama Critical Thinker umeshachukua hatua gani? NAOMBA TUJADILI.
 
sheria mbovu, kutosimamiana na uzembe wa kufikiri. kwa tulio serikalini ni kwamba, kule chain of comand haipo. ukiuliza nani anashughurika na taka ngumu na laini kwa miji mikubwa,utalia. kwani swala hilo halipo kwa manispaa, mganga mkuu, bwana afya wala viongozi wa mtaa. ni habari mchanganiko.
CHANZO KIKUU KAKA NI HICHO.
 
Tatizo letu kwuba ni mentality, tumejengwa kwenye dhana ambayo neno uchafu ni narrow sana kwa mfano majority wanaamini kuwa uchafu ni kinyesi na mkojo sio uchafu, gazeti sio uchafu, ganda lachungwa sio uchafu, gari bovu sio uchafu.

Juhudi inabidi ifanyike, toka majumbani ,( kids at infancy level) mashuleni ,( nursery,primary, secondary) , vyuoni na makazini kupanua defination ya uchafu ili at least iwe uchafu ni" kuwa na kitu kisichotumika mahali kisipotakiwa kuwepo"

Hii ikisink akilini at indivividual level itaenda mpaka institutional level kiasi kuwa itafika time chupa tupu hazitakuwepo, watu watajisaidia mahali panapotakiwa,maganda ya machungwa yatakwisha na hata municipal authorities watakuwa also responsible etc etc.
 
Back
Top Bottom