Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,636
- 25,617
Mh. Major
Nafasi za uteuzi aufanyao Mh. Rais katika ngazi yoyote haziombwi kihivyo! Lakini pia ujue kuna watanzania kibao kama wewe wanaishi nchini Tanzania. Elimu, uzoefu, uwezo na utendaji wao wa kazi unajulikana vema. Kama kweli, uko serious rudi nchini, shirikiana na watanzania wenzako katika shida na raha na wakujue pia upate muda wa kuwajua vizuri ikiwa ni pamoja na shida zao. Wananchi wakishakujua dhamira na uwezo wako, ni wao watakupatia uongozi aidha wa kuchaguliwa au wa kuteuliwa na Mh. Rais. Uteuzi hauji by chance, mara nyingi ni thru vetting na vetting ni watu wanaulizwa juu ya uwezo na utendaji wako wa kazi. Lakini pia ni lazima wajue itikadi yako, maana nafasi ya DC na RC ni kumwakilisha Mh. Rais....ikiwa ni pamoja na kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya chama husika ya 2005-2010 na 2010-2015.
Wenzako tayari wanajipitisha pitisha katika lango kuu la Ikulu Dar wakisubiria uteuzi. Mwenzangu ninadhani uko mbali.....du...Fimbo ya mbali haiui nyoka! Rudi tu nafasi ni nyingi na si lazima kipindi hiki! Samahani kama sijakusaidia...........pengine wengine watakupa moyo.
Mkuu mbona umekurupuka kujibu wazo la kijana mwenzetu?
Amekwishasema kwamba anataka kutatua tatizo la barabara za jiji la Dar-Es-Salaam na pia kuhakikisha jiji linakuwa safi.
Mimi nafikiri anafaa kuteuliwa awe mbunge wa kuteuliwa na baadae mkuu wa mkoa. Raisi kama anapitaa humu aangalie hii.
Du!