Ubunge wa Tundu Lissu usitishwe

Ubunge wa Tundu Lissu usitishwe

mbunge ambaye hatahudhuria mikutano mitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika atapoteza ubunge.
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif
icon_lol.gif

Vigelegele watanzania!!
 
Wanasheria kuna kitu wanaita Judicial Notice..hivyo Spika ana Judicial Notice kwamba Lissu ni mgonjwa
 
Katika viunga vya maeneo fulani Dodoma, mtu mmoja mzito anajiuliza kwanini mbunge haudhurii miezi kadhaa Bungeni bila ruhusa ya Mkuu wake alafu anaendelea kusema bado ni mbunge?

Ameshangaa kwanini sheria zinaandikwa tu kwenye makablasha lakin hazitumiki kiuhalisia,

Anayezungumziwa ni
Lissu hayupo bungeni tangu Septemba 8, mwaka jana. Kanuni ya 117 ya Bunge, inasema mbunge ambaye hatahudhuria mikutano mitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika atapoteza ubunge.

Lissu mpaka leo ni mbunge, maana yake Spika anatambua udhuru wake kuwa ni mgonjwa. Vinginevyo angekuwa ameshafutwa ubunge, maana alishapitisha mikutano mitatu mfululizo.
Lakin pamoja na kwamba anatambua udhuru wake kuwa mgomjwa ila hana ruhusa ya kutibiwa nje hakufuata utaratibu mpaka huko nje, hana referral ya Bunge kwenda nje kupitia Muhimbili,

Mkutano mkuu ndani ya watu fulani ambao umehusisha wastaafu kadhaa kwamba ni aibu kuendelea kulea utovu wa nidhamu na spika wa Bunge kulifumbia macho,
Kwani spika yeye atakuwepo hapo kwa muda gani? Na je spika alivyokwenda kuibiwa India mwaka mzima, kulitokea nini Kongwa? Acheni husda haya maisha ni mafupi sana, acheni kiburi cha uzima.
 
Fanyeni yote mnayotaka ila Mungu si ndugu yenu..anahukumu kwa haki
Kama Mungu hayupo upande wa serikali, wasingenunua ndege, kujenga reli mpya, kujenga Barabara, ku-control mfumuko wa bei na kadhalika. Mamlaka hii ipo chini ya Mungu, wasiotii ndio wanalaaniwa.
 
Lakin mungu ndo kawapa mamlaka za duniani

Mkuu hii post kiri umecopy na kupaste maana uzi wenye mauzui haya upo hapa jukwaani. Na kwanini uzi huu umeletwa sasa?

Baada ya Waitara kwenda studio kufanya mahojiano na kufanya siasa za majitaka kwa kutaka kupotosha shambulio la Lissu. Lissu hakuchelewa akajitokeza na kujibu upotoshaji ule kwa usahihi kuhusu shambulio lake. Na ufafanuzi ule umeeleweka na wengi na kumrudisha rais kwenye jinamizi lilelile la shambulio la Lissu. Sasa hawa wanaoleta hiki kitisho wanajaribu kumtisha Lissu ili akae kimya kuliko kumvua mtu nguo. Na wanaweza kumtoa Lissu kweli kwa kisingizio cha sheria. Ila wasichofahamu ni kwamba Lissu hategemei ubunge. Na hata akipoteza ubunge bado ana uwanja mpana wa kufanya siasa na anakubalika na watu sana. Ubunge hauwezi kumzuia Lissu kuongea ukweli na uovu haufichiki daima.
 
Kama Mungu hayupo upande wa serikali, wasingenunua ndege, kujenga reli mpya, kujenga Barabara, ku-control mfumuko wa bei na kadhalika. Mamlaka hii ipo chini ya Mungu, wasiotii ndio wanalaaniwa.
Indeed!
Na asipokuwa upande wa serikali atakuwa upande wa kina nani? Saccos, please!
 
Back
Top Bottom