Kuna tatizo moja kubwa sana Tanzania. Kununua kwa Kigezo kimoja tu ambacho umekariri
Unasikia mtu anakwambia star X mimi nnayo miaka 3 haisumbui, tecno yangu tangu ninunue sijaona tatizo
Kwakweli kununua vitu vya electronics hasa TV au Simu haiishii tu kusema kimekaa miaka mingapi.
TV kwa mfano zina mambo mengi ya kuangalia. Ikiwepo Ubora wa picha, Rangi, Kioo, speaker ukiachilia mbali tecnolojia za ziada, kama HDR, Mirroring nk nk
Sasa unakuta mtu anakwambia nna Mr Uk mwaka wa saba, kaangalie Iyo TV picha na Rangi duh unaweza kimbia. TV ukienda pembeni tu 45° unaona usiku
Kwahiyo kununua hv vitu yahtaji ki Review mambo mengi. Binafsi hata mitandaoni nakutaga Samsung inch 55 labda inauzwa mil 1, unavutiwa labda bei cheap. Lakini cha kwanza nitamuomba muuzaji Model ya TV husika. Hapo naweza kukaa sasa google hata masaa 2 nai Review taratibu.
Kuanzia Display, Colour, Finishing materials, Innovation inazokuja nazo Nk nk