Ubora wa camera ya Tecno camon cx

Mkuu nimeshaelezea sana humu ndio maana naona hata uvivu kuelezea, na kuanza kuchambua kimoja kimoja naweza andika hata page 100 u zaidi za A4, maana mambo ni mengi sana ukiingia deep zaidi ndio jinsi unavyoona. Hebu tuangalie hayo mambo matatu yaani storage, ram na camera.

Storage.
Kwenye simu kuna storage za aina nyingi sana, ila iliyo maarufu sana ni emmc, na hizi emmc zipo nyingi, yaani version tofauti tofauti, kama sijakosea emmc 5 ndio latest. Mwaka 2015 samsung akabadilisha kabisa soko la simu na kutuletea kitu kinaitwa ufs, ufs ni storage ambazo zina speed sana, mpaka leo hii simu kubwa zote aka flagship zinatumia ufs, iwe ni oneplus, HTC, samsung, huawei etc kifupi hazina mpinzani, hebu tuangalie utofauti wa speed wa emmc na ufs.

Hapo ukiangalia utaona utofauti mkubwa wa ufs ambayo imeanza 2015 kwenye s6 na simu za nyuma kama note 4 kushuka, mpaka leo hii 2017 bado flagship za Tecno zinakuja na emmc na hata hatuambiwa ni version gani,

Hivyo mtu kusema tu simu yangu ni 32GB au ni 64GB haitoshi sababu speed ya storage pia unatakiwa uijue, hii huathiri sana kufungua apps na speed ya vitu kumove toka storage ya simu hadi ram, hapa unakuta simu mbili ila moja kufungua game hadi kuanza inachukua dakika nzima na nyengine sekunde 10 tu.

tuje kwenye ram
Ram ni vile vile, zipo ddr2 za kizamani zaidi, ddr3 na ddr4 za kisasa, simu za flagship kama hio s7 inatumia ram za kisasa za ddr4 na tena ni dual chanell, yaani cpu inawasiliana na ram kwa njia mbili hivyo bandwidth inapita kwa wingi na kuongeza perfoamnce.

Cpu za mediatek zinazotumia ddr4 ni kama helio x30, lakini cpu hizi hutaziona Tecno akizitumia, anawadanganya watu na cpu xa kizamani kama helio x10 ambazo zinatumia ram za kizamani za ddr3 na pia ni single chanell, hebu tuangalie utofauti wa speed wa ram.

Na pia ikumbukwe hizi ram zina speed, zote zinaweza zikawa ni ddr4 ila moja ikawa 3200mhz na nyengine 2400mhz speed zake hazitafanana.

Na sababu simu haina dedicated gpu, ram pia hio hio hutumika kwenye matumizi ya gpu, unapoinstall launcher, unapocheza games na mambo mengine ya graphics itakusaidia.

tumalizie camera
Mkuu megapixel sio quality ya camera na hata uwe na megapixel ngapi haimaanishi camera yako itakuwa nzuri, vitu kama sensor na lens vinachangia sana quality ya picha, na camera ikiwa na megapixel nyingi huku sensor ni ndogo basi quality ya picha pia itakuwa ndogo sababu pixel zitakuwa ndogo ndogo zisizo na mwanga na noise za kutosha.

Mfano tuangalie simu kama s7 specs za Camera yake.
12 MP, f/1.7, 26mm, phase detection autofocus, OIS, LED flash, check quality
Video 2160p@30fps, 1080p@60fps, 720p@240fps, HDR, dual-video rec.,
Secondary 5 MP, 1/4.1" sensor size, 1.34 µm pixel size, f/1.7, 22mm,
Hapo kila kitu kina maana yake mkuu, kuanzia ukubwa wa sensor, ukubwa wa pixel, aperture, uwezo wa video, aina ya flash etc, tecno je?

Maisha yangu yote sijawahi ona wakitoa specs za camera zaidi ya phantom 6 plus, wakati wanaizindua wakasema wametumia sensor gani na ilikuwa ni imx 230,

Hii ni sensor ya 2014 miaka 3 iliopita na simu zote ilizotumika ni za bei ya chini kuliko hio Tecno, unaweza angalia zaidi hapa
Smartphones with IMX230 Exmor RS lens model

Then mtu huyo atakuja kujitamba hapa na tecno yake ya laki 8 kuwa ni kali balaa, wakati wenzake wananunua xiaomi za dola 100 anapata sensor hio hio.

Mkuu mambo ni mengi sana kama nilivyokuambia, kila kitu unachogusa kina maana,

Usb yenyewe kwa watu wengi ni tundu tu la kuchomekea chaja ila ina mambo mengi sana kuanzia usb otg uwezo wa kuchomeka flash, kuna usb 2 au 3 na transfer speed, kuna MHL na uwezo wa kuchomeka waya kwenye simu ukaangalia kwenye tv, etc

Kila ukiingia deep ndio unaona class za hizi simu ni tofauti na unakuta kila unapogusa Tecno wapo nyuma, kama una vyengine unataka nivielezee nitavielezea
 
Huyo jamaa hana mkono wa picha, ametetemeka. He would have made a better shot than that with steady hands.
hata mimi nimehisi hivyo, ila still inakuja weakness nyengine camera haina OIS,

simu ya kisasa yenye OIS inapunguza effect ya mtikisiko, hata kama mkono una shake picha inatoka vizuri kiasi.
 
Unapolinganisha simu ili kujua uwiano wa uwezo ni lazima uzingatie bei Samsung ya sh mil1 ilinganishe na tecno ya sh mil 1 kama ipo kwaiyo ukiangalia uwezo wa tecno na ubora per price tecno is the BEST EVER
mbona rahisi tu? phantom 6 inauzwa kiasi gani? mwanzo around laki 6 maybe now imeshuka around laki 5?

hebu compare na galaxy s6, A5 2017, J7 2017 etc ambazo zote bei ni humo humo, unakuta phantom 6 inapitwa kila idara. kuanzia camera, battery life, quality ya display etc
 
mkuu mimi sio pro wa camera hivyo sifahamu kiundani zaidi,

kwenye video naona its ok, sababu inachukua 1080p kwa 60fps, ime miss 4K ila kibongo bongo hiyo inatosha kabisa, tv zetu, chanell zetu bado hazijawa 4K, ukishoot kipindi cha tv au harusi itaonekana vizuri maeneo yote.

dpreview naona hapa pia wameisifia inatoa video nzuri kwenye mwanga mdogo, kwenye motion etc angalia hapa

Nikon D3300 Review

hata picha za kawaida ni nzuri mkuu
Nikon D3300 Review

sababu ni DSLR naamini itafaa matumizi hayo, cha muhimu tu jifunze zaidi online kupiga picha vizuri, then utapiga picha nzuri kushinda wenye camera za bei ghali zaidi.
 

Ninachokiona hapa ni kujaribu kuorodhesha properties za attributes mbalimbali, tena ukiwa unaelezea za sumsung zaidi. Kusema maarufu, ina speed sana, inatumia storage aina ya emmc, etc., haviwezi kuwa calculated quantitative na qualitative measure. Unaelezea kuhusu sensor, megapixels, etc., kwa kusema kwa mfano sumsung ina sensor nzuri, au megapixel nyingi lakini sensor ndogo picha zitakuwa noisy or whatever. Maneno kama ndogo, nzuri, speed sana, ni maarufu, quality ndogo, kutaja spec bila kuielezea maana yake ni nini, na inachangia kwenye quality au performance ya simu kivipi hayawezi kuwa ni uchambuzi linganifu. Halafu unataja sensor kirahisi tu, na uhusino wake na megapixel na resolution ya picha. Hayo ni mambo ya signal processing na optics, yakiambatana na calculations. Unapoongelea picha unaongelea 3D object, kuna super calculations mpaka unapokuja kuiona image rendered na camera yako. Halafu kingine, mambo hayapo kirahisi kama unavyoyachukulia. Tatizo la humu hamtumii utaalamu, au huwa hamkiri kuwa sielewi vizuri au sielewi kabisa kitu fulani kinafanyaje kazi. Halafu kila kitu kina strength na weakness yake, simu sio exceptional.

Eleza technically, sio kulist technical terms, what do I mean? Badala ya kuandika 720p@240fps, autofocus, 1.4 GHz, 5 MP, etc., eleza 720p ni nini, 240fps ni nini, 1 GHz maana yake nini, MP ni nini, and then inamaanisha nini tunaposema 720p@240fps, 1.5 GHz, 12 MP, etc., huku ukilinganisha specs za sumsung na tecno, kwa kila attribute, then sum up kwa kuonyesha one is better than another.

Unaweza kufanya uchambuzi wa ubora wa kamera tu kama alivyoomba mwuuliza swali. Unapoongelea camera unaongelea mambo ya optics na signal processing. Waambie watu nini maana ya 12 MP, sensor, ni bora kwa sababu gani, kwa sababu ya material yake? Yapi? architecture yake? Ipi? Kwa sababu ya modeling (maths behind it), kwa sababu ya lens yake? Aina gani? Kwa sababu ya sampling rate? Kwa sababu ya resolution yake? etc., na kwa nini hivyo vyote ni bora kwa simu moja kuliko nyingine. Unapoongelea resolution na sensor, unaongelea light signals/photons na uwezo wa lens/camera kuona na kucapture signal, kwa quality gani (arseconds/pixels), na kwa umbali gani.

Ongea kama mtaalamu. Ujue huwezi kuulizwa swali, then dakika 2 tu tayari umepata majibu, serious? Wataalamu wanainvest muda, skills, energy, na resources zingine kufanya research, sio kitu chepesi kama unavyochukulia.
 
huyo ambae hajui atauliza, au atagoogle, ukiandika tu megapixel inakuja google maana yake,

huwezi ukaanza kudefine kila kitu, mimi sio dictionary,

na naomba nitajie mtaalamu mmoja tu duniani zunguka mamilioni yote ya website ambaye aki review kitu au kutoa comparison anaanza chini kudefine kila kitu ni nini. huwa mambo hayaendi hivyo.
 
Ok,ahsante sana mkuu kwa mchango wako wa mawazo mazuri...umekuwa ukinisaidia sana mkuu
 

Naelewa ninachokuambia, huwezi kutumi terms nyepesi (they carry meaningless meanings, mfano ni maarufu sana, how does this explain quality?) kama hizo kufanya ulinganifu. Explain technically, tena ni sehemu mwafaka kwa sababu sio kila mtu mtaalamu kama wewe.

Kwa hiyo unadhani hao wanaofanya review wote ni wataalamu? Mfano blogger akifanya review ili kurefer watu links Amazon wanunue hicho kitu kupata asilimia fulani ya income ni mtaalamu? Sasa soma publications ambazo ni officially accepted na published kwenye journals, ndio utaona watu huwa wanaelezeaje vitu, hasa technical researches. Hata hao kwenye internet ambao wewe unawaona wote kama wataalamu wapo wengi mno, ambao huelezea mambo from scratch.

Kama unaamini wataalamu kama wewe huwa hawaelezi kila kitu wanapofanya review, basi wewe vunja huo mwiko, tufanyie review ya tofauti.
 
Kwa nini Jf imejaa rubbish mno? Kwa sababu ya pretty insanely cheap talks na cheap researches.
 

1. nimekuonesha storage na speed zake nikakuonesha hadi picha na nikakwambia jinsi speed ya storage inavyoathiri ufunguaji wa apps je nini unahitaji zaidi?

2. nimekuonesha ram nikakuonesha kwa picha speed ya ram na nikasema ram pia husaidia gpu na vitu kama games na apps nyengine za graphics,

kitu gani zaidi unataka hebu niambiae

mkuu seems hujui maana ya forum ni nini, forum si kitabu kitu kidogo uandike page nzima ya maelezo, forum ni sehemu tu ya discussion ambayo watu hubadilishana mawazo, huyu ana hiki yule ana kile.

kuna wikipedia, kuna google, kuna amazon, etc zote zina kazi zake hizo, hujajua maana ya kitu kufuate sehemu husika usiforce mtu akuelezee each and evertything humu sio maana ya forum hio.
 

Mkuu nasubiri picha zako ulizosema utapiga zikiwa mbali ili tuprove quality maana ulisema zitamaliza MB zetu tunazitaka tuzione ,halafu nataka za simu ya samsung na Iphone tu...Nokia tumuweke pembeni.
 
Mkuu nasubiri picha zako ulizosema utapiga zikiwa mbali ili tuprove quality maana ulisema zitamaliza MB zetu tunazitaka tuzione ,halafu nataka za simu ya samsung na Iphone tu...Nokia tumuweke pembeni.
duh napangiwa simu tena? sasa mkuu nimetumia Nokia 808 hapo kumuonesha ndugu yangu wa 1020 hao kina samsung na iphone wameingiaje? hakuna simu ya samsung wala iphone yenye lossless zoom kama ya 808 na 1020

na mimi sina iphone ya kutumia labda nikaombe kwa jirani,
 

Hahahah kumbe ndio hivyo,sasa hizo samsung unazozipa sifa kwa camera nzuri kuzidi tecno uweki picha zake tuzione,mara nyingi nakufatilia naona samsung ndio simu bora kwako na sisi watumiaji wa tecno ni kama tumepotea vile yani cheap user.

Na ntakutumia picha za tecno nilizopiga ili tuone utofauti maan kuna jamaa tulibishana sana ohh samsung camera kali kuna tecno ya laki2 camera kali na samsung ya laki 3 camera mbovu tu.
 

msiseme tu camera ya laki 2 na laki 3 mtaje na hizo simu, kuna jamaa siku moja humu kaponda samsung weeh anasema amenunua sijui laki 4 lakini haina kitu, mwisho wa siku tunamuuliza samsung gani? anasema galaxy s duos, kumbe kapata mjanja huko kamshikisha kanjanja.

na thread kibao humu mimi naziponda low end za samsung na kushauri watu wanunue simu za xiaomi na motorola, samsung si kampuni inayotengeneza low end nzuri.

laki 3 mimi napata galaxy s5 nitakuekea sample zake uone na wewe pamoja na hizo sample za kuzoom za king mwenyewe pia sitazisahau, sijapata tu muda wa kutoka nje mchana, nakuwa kazini.
 
Ukitaka kujua utofauti chukua hiyo c9 yako iweke kwenye ndoo ya maji na galaxy s6 halafu rudi hapa utupe majibu.
 
Naomba kujua hivi kwanini hizi Tecno Phantom bei zake ziko juu kulinganisha na Tecno nyingine?
Tecno Phantom zinakuwa na feature nzuri kidogo kuliko zingine kama amoled display,finger print reader,sensor ya sony na nimeona specs za 6 plus phantom wana processor ya deca core nadhani ndivyo vinafanya kuwa na bei.
Lakini haimaanishi ndio kuizidi high end za samsung.
 
Haisee na mm nitayaweka ya kwangu usiku na nataka nitoe ushahidi kwa picha za camera zenyewe. Maana mmezoea kuandikiwa kwa maneno hamuelewi. Sasa mm nakuja nimezipasua camera zote ili hzo specfications tuzione kwa undani kabsa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hakuna kitu kipya unachonieleza mimi, hivyo unavyoeleza kwangu ni too obvious na navijua muda mwingi sana. Wewe ulichotakiwa kufanya ni kuonyesha technically uzuri wa kitu kimoja kwa kulinganisha na kingine, chukua kipengele kimoja tu, cha camera, eleza ili kila mtu hata yule ambaye hajui kabisa akuelewe. and let's find out if you really understand what you're trying to tell us.

Huhitaji kuniambia mimi, tell the audience, acha njia za kienyeji kama kupiga picha na kulinganisha kwa macho.

Na nimekupa mfano mdogo, eleza kwa nini camera ya tecno pamoja na kuwa na pixel nying sio nzuri (maana ulishasema hili kwa kulinganisha picha, hiyo ni njia ya kienyeji), in relation to sensor na vitu vingine kama.

Kuhusu kama najua maana ya forum au sijui, nakuhakikishia kuwa najua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…