Twende mbele turudi nyuma, wanawake waliteseka sana

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
TWENDE MBELE TURUDI NYUMA, WANAWAKE WALITESEKA SANA

Anaandika, Robert Heriel

Licha ya kuwa Mimi ni mfuasi mzuri wa mfumo dume lakini nachukizwa na tabia ya utesaji, unyanyasaji na uzalilishaji wa Wanawake. Mfumo Dume ni Amani, haki, upendo na heshima Kwa dunia yetu.

Acha Wanawake wafanye watakavyo, Acha wawapeleke mputamputa wanaume wapumbavu, Acha wafurahie Uhuru wao. Waliteseka Sana. Hata kama zipo changamoto za Uhuru wao lakini ni akheri changamoto hizo kuliko Mateso waliyoyapata Mama zao.

Wanawake waliteswa na mababu zetu, walichapika, walifanywa Kama Punda.

Yaani unakuta Mwanaume anampiga Mkewe Kama Ngoma, ati kisa yeye ni mume au mwanaume. Haipendezi! Huo ni ukatili, na Dalili ya unyama.

Uchunguzi wangu ambao kimsingi siku zote haupendelei wala kusema uongo, ulibaini kuwa Wanawake waliowengi WA miaka ya 80 Kurudi nyuma 90% hawajawahi kufurahia Ndoa wala mahusiano.

Ubaba ni ubabe ndio hata Taikon ninakubali hivyo. Lakini uwe Ubabe wenye akili sasa, ubabe katika mambo ya Msingi. Taikon ni Muumini wa HAKI, najua haki ndio huleta Amani na Furaha!

Uchoyo ni miongoni mwa Mateso waliyoyapata wanawake. Hata hivi leo wapo wanaume ni machoyo, mabinafsi na yenye kujipendelea. Nani alikuambia Mkeo hapendi Paja la kuku Kama wewe, unakuta mwanaume mchoyo, vitu vyote vizuri awekewe yeye tuu. Akiulizwa, ati yeye ndio anatafuta pesa. Acha uchoyo Bata wewe. Kutafuta pesa sio kisingizio cha kujipendelea, Weka utaratibu wa kugawana vitu vizuri katika familia yako.

Wanawake ni viumbe wanaojifunza kutoka Kwa Wanaume, hiyo iweke akilini. Ukiwa mbinafsi Mkeo lazima Naye awe mbinafsi. Wanawake kisaikolojia wao wapo chini yetu hivyo hutegemea upendeleo kutoka kwetu.
Wanawake ni Lastborn hivyo hupenda kudeka na kupendelewa. Kutompa mwanamke Haki ya U-lastborn ni moja ya Mateso Kwa mwanamke.

Mwanaume popote Ulipo tambua kuwa wewe ni Firstborn hata kama Mkeo amekuzidi umri au kipato au Jambo lolote lakini Nature inakutambua hivyo.

Ni kweli Wanawake ni dhaifu Hilo wala halina Ubishi, lakini udhaifu wao hauondoi lolote katika thamani Yao.

Wanaume wengi hutumia vipato vyao kuwanyanyasa wanawake, kuwaonea na kuwatesa. Wanawake wengi kutokana na umasikini wao au kwenye familia watokazo hujikuta wakivumilia Mateso hayo. Chepuka uwezavyo lakini unashindwaje kujificha mpaka Mkeo akajua?

Ni kweli wanaume hatuwezi kuwa na Mwanamke mmoja hilo ni kweli. Lakini tutumie akili kusudi kulinda mioyo ya Wake Zetu. Wanaumia Sana.

Oooh! Wanawake hawaeleweki. Oooh! Wanawake ni chombo cha STAREHE. Ni kweli Wanawake hawaeleweki, na ni kweli ni chombo cha STAREHE. Sasa ndio uwatese na kuwanyanyasa?

Taikon ninajua kuwa, Matokeo ya wanawake kuwanyanyasa wanaume pale wawapo na vipato ni matokeo ya wao kunyanyaswa na Wanaume.

Binti ambaye Baba yake hakuwahi kumtesa Mama yake, ni nadra Sana kumkuta binti huyo akimnyanyasa mwanaume hata akiwa na kipato. Kinachofanya Wanawake wanyanyase Wanaume ni kutokana na tabia walizoziona Kwa Baba Yao alivyokuwa anamfanyia Mama Yao.

Maneno Kama, Ninawalisha tuu hapa, mnajaza Choo, wewe mwanamke ni Masikini Kama huko kwenu,
Kama nisingekuoa wewe ungekuwa hivi, ulikuja umekondeana sasa umenona unaanza kuleta kiburi,
Usiniletee tabia zenu za hovyo hapa, na maneno ya Dharau Kama hayo.

Maneno hayaishi, ukimwambia mtu neno Baya jua hatalisahau KAMWE!

Mwanaume ndiye anayeweza kumbadilisha mwanamke tabia. Tabia hizi mbofumbofu za wanawake Sisi Wanaume ndio tumesababisha.

Mwanaume kujiamulia kuoa vile atakavyo, kisa yeye ni mwanaume, hajali hisia za mkewe, walah! Yeye anachojua ni kufuata matamanio yake. Huo ni Ubinafsi.

Hujakaa na Mkeo mkajadili kuwa unataka kuongeza mke unajiamulia tuu. Hiyo sio HAKI na Mwanaume siku zote anayejitambua lazima azingatie HAKI.

Haya Mumechuma Mali, imetokea mnataka kutengana, kitu gani kinakufanya upate shida kumgawia hiyo mwanamke sehemu ya Mali mlizochuma? Kitu gani Kama sio ushetani.

Mkeo kama anakujua wewe ni mtu wa HAKI kamwe hawezi kuchukua kimabavu Mali ambayo hutompa wewe mwenyewe.

Unamdhulumu mwanamke Mali, unamfukuza licha ya kuishi na wewe miaka nenda Rudi, kisa alikuwa hafanyi kazi za kuzalisha, Ila alikuwa anaitunza familia yako na kukuhudumia mumewe ili ukazalishe lakini wewe hilo unaona kwako sio Mchango. Unafukuza. Hayawani mkubwa weee!

Taikon Kama Mwanaume mfuata mfumo Dume. Anapenda kuwaambia vijana wa kileo. HAKI na upendo ndio msingi wa Maisha.

Huwezi ukamdhulumu Mkeo ukabaki salama.
Na huwezi ukamdhulumu Mumeo ukabaki salama.

Mpe mtu haki zake.
Kama mmeshindwana, kaaeni muongee mnaachanaje, pigeni Hesabu Kwa Haki.
Mke achukue 40% au 30% au kadiri ya mlivyoishi na muda mliokuwa pamoja.

Au mume achukue 40 au 30 ikiwa mke atabaki na watoto.

Kuendekeza ubinafsi na Kupenda penda Mali kutakufanya usiwe na Amani na furaha hasa ukiwaonea watu wako wa muhimu katika maisha yako.

Zingatia, Haki ni Haki.
Mkeo akiwa mwema mlipe Mema.
Mkeo akiwa Mbaya basi mlipe Mabaya.
Jitahidi uwe hakimu mzuri katika maisha.

Baya moja lisiondoe Mema elfu moja.
Na jema moja lisifute mabaya elfu moja.
Haki bin Haki
Kuna Wale Wadada wa mjini wanaofunga ndoa kwaajili ya Mali alafu baada ya miaka mitatu wanavunja ndoa ili mgawane Mali. Hao usiwachekee. Haki bin haki. Ubaya ubaya, wema Kwa wema

Usikubali Mkeo au mumeo muliyewahi kuishi Kwa furaha mwenye Mchango mkubwa katika maisha yako, akakususia Mali mlizochuma pamoja, hazitakusaidia.

Usione shida kupata kidogo Kwa Yule aliyekufanya ukapata vingi.

Yule Mtibeli,

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Kulikua na njia nzur ya kuwasilisha ulichadhamilia kuwasilisha

Ila hili Kashfa kwa mababu zako wa zamani Ni utovu mkubwa sana wa nidhamu kwa miiko na makuzi yetu waafrika

Nna wasiwasi na umri wako,
Huenda unaendeshwa mihemko na ushabiki zaidi kuliko akili, uhalisia na busara

Sijapenda
 
Ila Twende mbele, turudi nyuma

 
Unapokua mwongo,
Hakikisha Uwe na kumbukumbu

Sio leo unaleta hili,
kesho unaleta Lilingine linalokinzana na lililotangulia.

Unakua unatukanganya Sana mkuu

Kuna mda utatufanya tuhisi haya sio Maneno yako, bali unatumika TU.

Nanukuu
 
Kulikua na njia nzur ya kuwasilisha ulichadhamilia kuwasilisha..

Miiko ya kiafrika inahitaji maboresho, nyeusi iwe nyeusi, nyeupe iwe nyeupe.

Ukishafanya uhuni au ubaya lazima matokeo yake yawe Kashfa, kejeli, matusi, dhihaka, na Dharau. Hiyo ndio haki bila kujali aliyefanya ni Babu, Baba au mtoto.

Mtu akifanya wema na Jambo zuri lazima matokeo yake yawe, sifa, utukufu, majigambo, majivuno, heshima, na kumbukumbu nzuri Kwa kizazi na kizazi. Hiyo ndio Haki.

Haki haiangalii nani, yukoje.

Wazee kuna sehemu walizingua lazima tuseme.
Yapo Maeneo waliyopatia pia lazima tuseme.

Masuala ya unafiki wengine hatuna.
Lugha niliyoyumia kuwakosoa na kuwakejeli. Ndio lugha hiyohiyo nitakayotumia kuwapongeza walipopatia.

Hata Mimi nikiwa Baba Bwege, mjinga, Mhuni, Acha watoto wangu wanitambue Kwa kejeli, dhihaka, na vijembe. Hao ndio watakuwa wanangu niliowazaa Mimi mwenyewe. Copy yangu. Na sio Matoto yatakayonionea haya na kuniletea unafiki wa wapuuzi.

Hivyo ndivyo Taikon na watu wa Tibeli tulivyo.

Hakuna mwenye adabu zaidi ya Yule ashikaye adabu. Hakuna mwenye Haki zaidi ya Yule afanyaye Haki.

Umri haukufanyi uheshimiwe, isipokuwa Matendo yako.
Ubaba au uanaume haukufanyi uheshimiwe isipokuwa matendo yako.

Unafiki wengine hatunaga
 
Unapokua mwongo,
Hakikisha Uwe na kumbukumbu

Sio leo unaleta hili...

Mimi ni mfumo dume na sijawahi kubadilika.

Kufuata mfumo dume sio kunyanyasa, kutesa, kudhulumu wanawake au kuleta Ubabe usio na Akili.

Uanaume ni Akili, busara, upendo, Haki, maamuzi n.k.
 
Ulipoandika hivi,
Ulikua umelewa au ?

 
Ulipoandika hivi,
Ulikua umelewa au ?


Nilikuwa nipo sahihi kabisa.

Na msimamo wangu upo palepale.
Tatizo ili unielewe itakupasa ufanye jitihada
 
Nilikuwa nipo sahihi kabisa.

Na msimamo wangu upo palepale.
Tatizo ili unielewe itakupasa ufanye jitihada
Inapofikia hatua mtu mzima huoni umuhimu wa tasnia ya ndoa,


Sidhan Kama una mamlaka ya kuwashaur chochote walio kwenye ndoa zao,

Zaidi zaidi utajikuta unashaur yasiyofaa na unaharibu ndoa za Watu kwa sababu tayar una chuki inafukuta kifuani mwako dhidi ya tasnia ya ndoa
 
Inapofikia hatua mtu mzima huoni umuhimu wa tasnia ya ndoa,


Sidhan Kama una mamlaka ya kuwashaur chochote walio kwenye ndoa zao,

Zaidi zaidi utajikuta unashaur yasiyofaa na unaharibu ndoa za Watu kwa sababu tayar una chuki inafukuta kifuani mwako dhidi ya tasnia ya ndoa

Ndoa iwepo isiwepo ninachozungumzia ni HAKI.
Haki na ndoa ni muhimu zaidi kuliko ndoa yenyewe
 
Kulikua na njia nzur ya kuwasilisha ulichadhamilia kuwasilisha

Ila hili Kashfa kwa mababu zako wa zamani Ni utovu mkubwa sana wa nidhamu kwa miiko na makuzi yetu waafrika

Nna wasiwasi na umri wako,
Huenda unaendeshwa mihemko na ushabiki zaidi kuliko akili, uhalisia na busara

Sijapenda
Mtu anakuwa defined kwendana na mambo anayoyafanya/ aliyoyafanya, kama wazee walifanya upuuzi hakuna njia nyingine ya kuwa define zaidi ya kupitia upuuzi wao. Nyerere alikuwa very straight kwenye mambo ya kipuuzi na hakupenda soft words. Ukitenda mazuri utaitwa mwema, ukitenda mabaya utaitwa mwovu, simple as that.
 
Mtu anakuwa defined kwendana na mambo anayoyafanya/ aliyoyafanya, kama wazee walifanya upuuzi hakuna njia nyingine ya kuwa define zaidi ya kupitia upuuzi wao. Nyerere alikuwa very straight kwenye mambo ya kipuuzi na hakupenda soft words. Ukitenda mazuri utaitwa mwema, ukitenda mabaya utaitwa mwovu, simple as that.

Tatizo la baadhi yetu wanaume tunakuwa tunafurahi pale tunaoowasema Wanawake wakikosea mfano, kuwakosoa single mother, au Malaya tunajisikia Raha Kwa vile Sisi sio wanawake.

Lakini akitokea mtu atukosoe Sisi wanaume Kwa baadhi ya tabia zetu mbaya tunaona shida.
Hiyo ni tabia ya ubinafsi, kutokukubali ukweli. Na kujiona miungu watu.

Mimi kama Baba sioni shida kujikosoa mwenyewe na kukosolewa na watoto au wajukuu wangu pale nikipuyanga.

Ukiwa Free mind huwezi kuwafanya watu wengine Wafungwa Kwa makosa yako. Ati wasiseme kisa ni Baba au Babu yao
 
Kwaiyo Unajikuta mwanaharakati flani Hivi wa Haki za wanawake sio?


😂😂
Mkuu umenifanya nicheke Sana.
Mimi Muumini wa Haki.

Hao wanawake wanahaki zao Kama tulivyosisi.

Wapo wananiita mnyanyasaji na mdhalilishaji wa wanawake ninapowakosoa hao wanawake. Na Leo mpo mnaniona najikuta mtetezi wa haki za wanawake pale ninapowatetea wao na kujikosoa
 
Tatizo la baadhi yetu wanaume tunakuwa tunafurahi pale tunaoowasema Wanawake wakikosea mfano, kuwakosoa single mother, au Malaya tunajisikia Raha Kwa vile Sisi sio wanawake.

Lakini akitokea mtu atukosoe Sisi wanaume Kwa baadhi ya tabia zetu mbaya tunaona shida.
Hiyo ni tabia ya ubinafsi, kutokukubali ukweli. Na kujiona miungu watu.

Mimi kama Baba sioni shida kujikosoa mwenyewe na kukosolewa na watoto au wajukuu wangu pale nikipuyanga.

Ukiwa Free mind huwezi kuwafanya watu wengine Wafungwa Kwa makosa yako. Ati wasiseme kisa ni Baba au Babu yao
Tatizo linaanzia kwenye mentality. Mwanaume kujiona supreme kwenye familia ni mambo ya stone age. Mwanaume unakuta anajisifia kwa ku- terrorise familia- kwa kutengeneza unnecessary fear kwa wanawake au watoto as if baba ni Mungu which is totally nonsense. Baba anapaswa kuwa kiongozi na siyo mtawala. Nw days chunguza-watoto/wake wengi hawaelewani na Baba/waume zao kwa ajili ya utemi wa kijinga. Wanaume ni lazima waelewe kwamba uelewa wa watoto/wanawake wa sasa na jinsi wanavyopambanua mambo umeshabadilika-very very significantly.
 
Tatizo linaanzia kwenye mentality. Mwanaume kujiona supreme kwenye familia ni mambo ya stone age. Mwanaume unakuta anajisifia kwa ku- terrorise familia- kwa kutengeneza unnecessary fear kwa wanawake au watoto as if baba ni Mungu which is totally nonsense. Baba anapaswa kuwa kiongozi na siyo mtawala. Nw days chunguza-watoto/wake wengi hawaelewani na Baba/waume zao kwa ajili ya utemi wa kijinga. Wanaume ni lazima waelewe kwamba uelewa wa watoto/wanawake wa sasa na jinsi wanavyopambanua mambo umeshabadilika-very very significantly.

Ni kweli kabisa Mkuu
 
""Muishi nao kwa akili " Kumnyanyasa mwanamke ndo akili zenyewe hizo......ile siyo kuwanyanyasa ndo stahili yao...unapoteseka na jua kuuza maji pale tazara mara ukoswe koswe kugongwa. Je yale siyo mateso?
 
Mtazunguka sana, lkn tatizo ni mke mwenyewe si aanze tu km anaona vepi bana??....jitu unalipikia unalilaza usingizi kwa nini usliwekeee sumu litembee limekufa??

Mungu alisema muishi nao kwa akili halafu wewe uje useme wanateswa???ngoja siku wakuroge uwe punda ndo utajuwa wanawake siyo wa mchezo!....wana runnDunia weye unasema wanateswaaa??

mie naona wewe umesharogwa hasaaa na huchomoki usichezeee ke weye.....pesa mnazo tafuta ni ajili ya nini??....vita hizi zooote kisa ni ke tu!!

Mwanamke ana nguvu za aina mbili akishindwa ile ya Mungu anatumia ya shetani ambayo hii kamwe me hataielewa kamwe lazima akuondoe ukimuona mwanamke hata km ameachwa msalimie shikamoo mwanamke!

Mlivo wajinga mnapatwa halafu mnaona mmepata kimasihara kuuumbe mmeliwa...endelea kutupamba tuwaue mpK mukome
 
aani unakuta Mwanaume anampiga Mkewe Kama Ngoma, ati kisa yeye ni mume au mwanaume. Haipendezi! Huo ni ukatili, na Dalili ya unyama.
Duniani koote Hakuna mnyama Dume! anaye mpiga mnyama jike (mkewe) km ngoma! km huyo mnyama yupo muweke hapa! Ndege/mnyama yeyote km kuku jogoo anampenda sana mtetea,

Mfano jogoo anampa panzi mitetea hata km jogoo ana njaa vipi, na jogoo linakula la mwishooo!

Jogoo kamwe hatoki nje ya Nyumba bila kumtanguliza mtetea kwanza, na kam mtetea hatoki kwanza jogoo kamwe hatoki ndani mpe nafasi pumba ujuavyo lkn hamuachii mtetea!

ivo ivo kwa wanya km farasi, ngombe , mbuzi, kondoo nk! huko kwenu Musoma si ni wafugaji bana??chunguza uone!...kma umeawafananisha wanaume na hawa wanyama, basi me ni Bomba sana!

Jamani mutu apigwe kama ngoma??..... ili iweje??... mbona me mnawaonea sana!! au ndo harakati??...imefika wkt me tunawaonea hata huruma,...... haya yooote yametokea wapi??

Me nao wametuliaaa hawatii neno! sijui wanaharakati mmewarogea nini?? me mjue mie nawasaidia msiwe vilaza!!...ke awe mnyama/ ndege/mdudu/mtu wanabembelezwa saaana mpaka basi!

hkn kiumbe mtu eti ''ke kinadhalilishwa! km mleta mada anavosema! punguzeni makali ya maneno, km ukiona ivo mmoja wao ni mgonjwa wa akili!
 
Back
Top Bottom