Huu uhuru utakuje wakati kuuza mahindi Kenya tu unahitaji kibali cha serikali.
Ndugu zangu hata tukienda nchi za "mabeberu" nako kuna regulations tena nyingi tu.
Hakuna nchi isiyo na regulations.
Kimsingi namna gani tunatumia regulations in place to work in "farmers favor" ikiwa ni anaelima shambani, anaefanya processing and packaging au anae-export.
Ni namna gani kuna kuwa na urahisi wa kupata vibali vya biashara ya export baada ya kupata soko. Kwa anaefanya export anafanya processing na packaging kwenye ubora upi ambao unashindana na bidhaa toka duniani kote.
Pia serikali (wizara ya mambo ya nje, wizara ya fedha, wizara ya kilimo, wizara ya usafirishaji/uchukuzi) ina mkakati gani kwa kushirikiana na sekta binafsi, vyama vya ushirika ua kampuni za ubia kati ya serikali na sekta binafsi.
Soko la nje ukitoa Comoro ambako mwanabodi kaleta hoja lina uhitaji mkubwa sana wa vyakula sio kwa kg chache. Ni tani (quantity) za kutosha na kuwa na continuity, kwa kuzingatia ubora(quality)
Tanzania ikipata forex iwe kwa private au public maana yake wizara hizo hapo juu zinafaidika moja kwa moja.
Bank ya Kilimo na Bank ya uwekezaji, zimekaa mkao gani kuwa sehemu ya ushindi kwenye mchakato kuanzia mwanzo.'
Mifumo ya bank zetu anavizia biashara ishakuwa kubwa ambapo huenda akawa na access hata kukopesheka nje ya Tanzania, ndiyo maafisa mikopo wanakimbizana kutafuta mteja kumkopesha.
Kwanini toka mwanzo(drawing board) bank, bima, zikae na potential investors na ku-project tunakuza vip exports. Hata kabla ya commitment ya kutoa hela, kupata access ya watajwa hapo juu huwa sio jambo rahisi.
Ndiyo maana wakija wachina, indians au mabeberu ambao wako financed na nchi walizotoka wananunua mpaka udaga. Kwanini wasisubiri sisi tuwapekee unga hata kama ni udaga? Wakija na machine zao wakanunua udaga Tanga waka-process we remain with a small value ya lion share.
Tuna safari ndefu, yaweza kuwa fupi kama tunakaa chini kwa issues za maana including hii. Huwa navunjika moyo tuna doria ya wahalifu mitandaoni na mpaka sheria na jeshi lipo kwa uhalifu kama huo; ila hatujawahi kuwa na "doria", vetting, scouting ya innovators na creators of investment project. hapo ndipo sehemu ya kwanza tunapokwana