Niliachana na ajira nikaingia kwenye kilimo, na kweli mambo yamejipa

Nesi mkunga

JF-Expert Member
Nov 28, 2022
701
1,849
Yule aliyesema ajira ni uti wa mgongo aisee hakukosea hata kidogo na kiukweli kilimo nitakiheshimu na nitazidi kukiheshimu kusema za ukweli ukubali au ukatae

Baaada ya kuachana na ajira niliingia kwenye kilimo maeneo ya Mpanda mkoani Katavi.Nilienda kufanya kilimo cha mpunga.

Aisee kilimo kilinipa pesa mpaka nikaanza kujilaumu kwanini nilichelewa kuingia huku.

Wakuu msimu uliopita tu nimelima hekari 20 nikapata gunia 150 plus za kununua kama 150 jumla nikawa na gunia mia tatu nikauza kwa 2500 mkoani singida na nilipata kilo 24000 piga mahesabu ni kama milioni 60 na ukitoa gharama zote faida niliyopata aiseee ningeweza kufanya kazi miaka kadhaa nisingepata hiyo.

Na sio mpunga tu, nililima maharage na mahindi mkoani Chunya faida niliyoipata wewe uliyepo kwenye ajira hauwezi kuipata hata kidogo na pia nililima ufuta wilayani Chunya nasema faida niliyoipata ni zaidi yako ya mshahara wako wewe uliyepo kwenye ajira haunifikii hata ukifanya kazi kwa miaka 10

Karibuni sana haters kwa makasiriko na wale wanaotaka kufanukiwa kwenye kalimo

Yaani inashangaza lijitu limemaliza SUA yupo barabarani kutwa kutembeza bahasha za kaki aiseee! Karibuni mpanda, chunya, Lindi na morogoro where my money is there
 
Hongera kiongozi, japo miaka ya 2014 niliacha ajira nikazama Mpanda kulima niliangukia pua Hadi nikatumiwa nauli ya kurudi home,Ila sikuridhia nilirudi tena kuchukua mke huko.

Ila sijui upo pori gani maana heka 20 Kwa gunia 150 Kwa mpanda kwa gharama za uendeshaji wa Kila heka kama shamba si lako, upandaji ni hela ,kung'olea ,kukata kupiga na kubeba kutoka mbugani gharama inakuwa 600000 Kwa heka 20 inakuwa kama 12!0000;000 mtaji si haba japo bado inalipa Sana Ila kawaida kuna mbuga ya senta mesha kijiji cha kamsanga inatoa 20 Kila heka maana yake ungepata gunia 350 au 400 jitahidi msimu huu tembelea huko Mimi nilienda kulima vitunguu ndo vilinikatisha tamaa nikachukia kilimo Ila nimeishi pande hizo muda Hadi mwaka juzi
 
Hongera kiongozi, japo miaka ya 2014 niliacha ajira nikazama Mpanda kulima niliangukia pua Hadi nikatumiwa nauli ya kurudi home,Ila sikuridhia nilirudi tena kuchukua mke huko.

Ila sijui upo pori gani maana heka 20 Kwa gunia 150 Kwa mpanda kwa gharama za uendeshaji wa Kila heka kama shamba si lako, upandaji ni hela ,kung'olea ,kukata kupiga na kubeba kutoka mbugani gharama inakuwa 600000 Kwa heka 20 inakuwa kama 12!0000;000 mtaji si haba japo bado inalipa Sana Ila kawaida kuna mbuga ya senta mesha kijiji cha kamsanga inatoa 20 Kila heka maana yake ungepata gunia 350 au 400 jitahidi msimu huu tembelea huko Mimi nilienda kulima vitunguu ndo vilinikatisha tamaa nikachukia kilimo Ila nimeishi pande hizo muda Hadi mwaka juzi
Upo mpanda sehemu gani mkuu
 
Hongera sana, nitakuja huko nami kulima mahindi mpunga siwezi labda kununua nitakutafuta ili uwe mwenyeji wangu
 
Hongera kiongozi, japo miaka ya 2014 niliacha ajira nikazama Mpanda kulima niliangukia pua Hadi nikatumiwa nauli ya kurudi home,Ila sikuridhia nilirudi tena kuchukua mke huko.

Ila sijui upo pori gani maana heka 20 Kwa gunia 150 Kwa mpanda kwa gharama za uendeshaji wa Kila heka kama shamba si lako, upandaji ni hela ,kung'olea ,kukata kupiga na kubeba kutoka mbugani gharama inakuwa 600000 Kwa heka 20 inakuwa kama 12!0000;000 mtaji si haba japo bado inalipa Sana Ila kawaida kuna mbuga ya senta mesha kijiji cha kamsanga inatoa 20 Kila heka maana yake ungepata gunia 350 au 400 jitahidi msimu huu tembelea huko Mimi nilienda kulima vitunguu ndo vilinikatisha tamaa nikachukia kilimo Ila nimeishi pande hizo muda Hadi mwaka juzi
kitu gani kilikufelisha kwnye kitunguu?
 
Sikia we mkulima stadi, tulienda shule kusomea kuajiriwa tupate hela bwerere za uhakika kila mwezi bila stress plus pensheni ya uzeeni, ni hicho tu ndicho tunachopendea kuajiriwa. Ila kwa wale walioajiriwa kule pa hovyohovyo bila hata pensheni uzeeni bora wakajikite kwenye kilimo wasije wakafa masikini kwa kujitakia
 
Yule aliyesema ajira ni uti wa mgongo aisee hakukosea hata kidogo na kiukweli kilimo nitakiheshimu na nitazida kukiheshimu kusema za ukweli ukubali au ukatae

Baaada ya kuachana na ajira niliingia kwenye kilimo maeneo ya Mpanda mkoani Katavi.

Nilienda kufanya kilimo cha mpunga Aisee kilimo kilinipa pesa mpaka nikaanza kujilaumu kwanini nilichelewa Kuingia huku?

Wakuu msimu uliopita tu nimelima hekari 20 nikapata gunia 150 plus za kununua kama 150 jumla nikawa na gunia mia tatu nikauza kwa 2500 mkoani singida na nilipata kilo 24000 piga mahesabu ni kama milioni 60000000 na ukitoa gharama zote faida niliyopata aiseee ningeweza kufanya kazi miaka kadhaa nisingepata hiyo.

Na sio mpunga tu nililima maharage na mahindi mkoani chunya faida niliyoipata wewe uliyepo kwenye ajira hauwezi kuipata hata kidogo na pia nililima ufuta wilayani chunya nasema faida niliyoipata ni zaidi yako ya mshahara wako wewe uliyepo kwenye ajira haunifikii hata ukifanya kaxi kwa miaka 10

Karibuni sana haters kwa makasiriko na wale wanaotaka kufanukiwa kwenye kalimo

Yaani inashangaza lijitu limemaliza SUA yupo barabarani kutwa kutembeza bahasha za kaki aiseee! Karibuni mpanda,chunya,Lindi na morogoro where my money is there
Hicho kilimo ni kama kazi nyinginezo tu, kuna kutoboa na kufeli


ila wewe unaongelea kufaulu tu, kuna watu washawekeza huko na sasa hawatamani.



Kikubwa shukuru kwa kuona mwanga wa mafanikio ila sio kudharau watu
 
Back
Top Bottom