Tuwe wakweli: Diploma vs Degree kwenye ualimu

Tuwe wakweli: Diploma vs Degree kwenye ualimu

CK Allan

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2013
Posts
2,784
Reaction score
6,180
kuelekea ajira mpya za walimu hebu tuwe wakweli wanaJF ni mwalimu yupi anaandaliwa vizuri kiuwezo na kimaadili pamoja na mbinu za kufundisha kati ya diploma na degree? ikumbukwe kuwa mwalimu wa diploma hufanya mtihani wa mwisho chini ya necta na akifeli somo moja (SUP) Haajiriwi wakati yule wa chuo kikuu husoma kwa semister..nina mifano ya watu kadhaa ambao walifeli diploma wakaamua kwenda chuo kikuu leo hii wana degree! pia hata shule nyingi za binafsi hawapendi wenye degree unless huyo mtu kapitia diploma kwanza! sitasema mengi najua kuna watu watanielewa tofauti....hata hivyo sina nia mbaya karibuni tujadili
 
Nia yako ni nini? Unapoongelea elimu unaongelea individuals..uwezo wa mtu mmoja mmoja.
 
wa diploma ni mzuri zaidi kuliko wa degree hilo nina ushahidi nalo mwaka jana walikuja walimu wa btp kutoka sekomu walikuwa mwaka wa 3, MUNGU wangu kuandaa hawajui kabsa walipokuja wakaguz wao ilibid tuwasaidie kuandaa vipindi na kuwaelekeza jinsi ya kutumia zana, walipokaguliwa walipewa big up.
 
Nia yako ni nini? Unapoongelea elimu unaongelea individuals..uwezo wa mtu mmoja mmoja.

Mada inajieleza mkuu...uwezo wa mwalimu..au yupi ni mwalimu hasa!
 
Upi? u degree au udiploma au huu uzi? mkuu mbona una hasira?
mimi binafsi nawakubali diploma kwa maadili wako juu kuliko degree, pia wako chini ya grade A, lakini kwa competence kuvunja madude degree wako juu, pia wakati mwingine inategemea na aina ya chuo ambacho yule mtu alisoma, pamoja na juhudi binafsi. Unaweza ukawa na degree ukazidiwa content na diploma holder.
 
wa diploma ni mzuri zaidi kuliko wa degree hilo nina ushahidi nalo mwaka jana walikuja walimu wa btp kutoka sekomu walikuwa mwaka wa 3, MUNGU wangu kuandaa hawajui kabsa walipokuja wakaguz wao ilibid tuwasaidie kuandaa vipindi na kuwaelekeza jinsi ya kutumia zana, walipokaguliwa walipewa big up.

Kama walikuja wa BTP ni wa Diploma hao, wa Degree huwa wanafanya TP.
Pia hao wa Diploma wanafundshwa na wa Degree.
 
anaJF ni mwalimu yupi anaandaliwa vizuri kiuwezo na kimaadili pamoja na mbinu za kufundisha kati ya diploma na degree?
  • Diploma full stop.
  • tEACHING Methodology kiundani zaidi kuliko ngazi ya Degree
  • Ngazi ya Diploma Huwa wanafundisha mpaka aina za nguo anazopaswa kuvaa mwalimu awe she au me - Kitu HAIBA YA MWALIMU
 
Ukimpata aliyeanzia Certificate hadi kufikia Degree, huyo ni jembe sana.
Kwa Mtazamo wangu, kwenye Degree mambo mengi yanakwenda kinadharia sana, lengo likiwa ni kukamilisha Semester. Kwny Diploma ya Ed, muda wa mazoezi ya Ualimu na Ufundishaji ni mwingi sana.
Nimekutana na vijana wengi wa Vyuo vikuu wakiwa mazoezi, (mniamini) ni majanga.
Asiyeamini aende kwny mashule ajionee
 
Diploma anasomea 'Ualimu'
Degree anasomea "Elimu"
kuna tofauti kati ya kusomea ualimu na kusomea Elimu! Sio wote wAnaosomea Elimu ni walimu! ndo maana vile vya diploma na certificate vinaitwa TTC-Teachers' Training Colleges!! Na hao wa diploma wanafundishwa na wenye degree, ila mleta mada uko biased na huenda pengine una diploma na umekosa qualifications za kusoma hyo degree! #nenda kasome acha kulalama hapa!
 
mbona kuna watu wanafeli kwenye digrii wanarudi kusoma diploma hao hujawaona?mimi ninao ushahidi
kuelekea ajira mpya
za walimu hebu tuwe wakweli wanaJF ni mwalimu yupi anaandaliwa vizuri
kiuwezo na kimaadili pamoja na mbinu za kufundisha kati ya diploma na
degree? ikumbukwe kuwa mwalimu wa diploma hufanya mtihani wa mwisho
chini ya necta na akifeli somo moja (SUP) Haajiriwi wakati yule wa chuo
kikuu husoma kwa semister..nina mifano ya watu kadhaa ambao walifeli
diploma wakaamua kwenda chuo kikuu leo hii wana degree! pia hata shule
nyingi za binafsi hawapendi wenye degree unless huyo mtu kapitia diploma
kwanza! sitasema mengi najua kuna watu watanielewa tofauti....hata
hivyo sina nia mbaya karibuni tujadili
 
nashangaa sana maana huyu wa diploma anafundisha na mwalimu wa degree kule chuoni
 
Diploma anasomea 'Ualimu'
Degree anasomea "Elimu"
kuna tofauti kati ya kusomea ualimu na kusomea Elimu! Sio wote wAnaosomea Elimu ni walimu! ndo maana vile vya diploma na certificate vinaitwa TTC-Teachers' Training Colleges!! Na hao wa diploma wanafundishwa na wenye degree, ila mleta mada uko biased na huenda pengine una diploma na umekosa qualifications za kusoma hyo degree! #nenda kasome acha kulalama hapa!

Mkuu kweli nina diploma na kutokana na nilivyoona uwezo wa wale degree holder nimeona sina haja ya kuchukua degree maana hakuna walichonizidi ! pia kuhusu sifa kuanzia za form 6 hadi matokeo yangu ya dip yananiruhusu kuchukua degree...sasa nifuate nini huko? kuongeza mshahara au? maana maujuzi...hahaha!
 
Diploma anasomea 'Ualimu'
Degree anasomea "Elimu"
kuna tofauti kati ya kusomea ualimu na kusomea Elimu! Sio wote wAnaosomea Elimu ni walimu! ndo maana vile vya diploma na certificate vinaitwa TTC-Teachers' Training Colleges!! Na hao wa diploma wanafundishwa na wenye degree, ila mleta mada uko biased na huenda pengine una diploma na umekosa qualifications za kusoma hyo degree! #nenda kasome acha kulalama hapa!

Umeongea vema mkuu, kitu kingine mtu wa degree anaandaliwa kwaajili ya management, kufundisha ni kidogo sana wakati dip. Wao ni wafanya kazi.

Ukiona mkuu wa shule ana diploma basi jua ni experience imembeba na ni mzee, lakine wakuu wengi wa shule wana degree, na waraka wa elimu wa 1995 unasema wakuu wa taasisi zote lazima wawe na degree na kuendelea (haijalishi ni shule ya msingi au sekondari na taasisi zote za elimu)

Uwezo na ubora wa walimu wa degree hutegemea mambo mengi,
1: Chuo alichosoma mhusika
2: mtu binafsi.
Na sababu nyinginezo.
Suala la watu wa degree kukataliwa, inategemea na aina ya chuo, waajiri wengine huchagua aina ya vyuo wanavyo taka.
Kitu kingine ni suala la minimum cost=cheap labor. Kumlipa mtu wa degree ni kazi kuliko wa diploma-they are cheap to pay na hawana challenge sana kwenye management ( They are administrators-they only do what the management want)
 
Mkuu kweli nina diploma na kutokana na nilivyoona uwezo wa wale degree holder nimeona sina haja ya kuchukua degree maana hakuna walichonizidi ! pia kuhusu sifa kuanzia za form 6 hadi matokeo yangu ya dip yananiruhusu kuchukua degree...sasa nifuate nini huko? kuongeza mshahara au? maana maujuzi...hahaha!

kaka ulisha soma hiyo degree au unaisikia? Unaposema degree na diploma hamna tofauti nakuwa na wasi wasi na uelewa wako na wanafunzi unao wafundisha! Kasome degree kisha ulete uzi hapa ukihitimu.
 
ndo maana vile vya diploma na certificate vinaitwa TTC-Teachers' Training Colleges!!

Mkuu hakuna ttc nowdays kuna tc...neno training limetolewa
 
kaka ulisha soma hiyo degree au unaisikia? Unaposema degree na diploma hamna tofauti nakuwa na wasi wasi na uelewa wako na wanafunzi unao wafundisha! Kasome degree kisha ulete uzi hapa ukihitimu.

Ukihitimu au ukipewa?
 
diploma anasomea 'ualimu'
degree anasomea "elimu"
kuna tofauti kati ya kusomea ualimu na kusomea elimu! Sio wote wanaosomea elimu ni walimu! Ndo maana vile vya diploma na certificate vinaitwa ttc-teachers' training colleges!! Na hao wa diploma wanafundishwa na wenye degree, ila mleta mada uko biased na huenda pengine una diploma na umekosa qualifications za kusoma hyo degree! #nenda kasome acha kulalama hapa!

well said mkuu degree asifananishwe na diploma wa diploma wameachwa mbali na degree, ndo maana degree anaweza fundisha a level ila dip mmmh
 
Back
Top Bottom