Mkuu olmo,
kwanza kabisa nakupongeza kwa mtazamo wako wa nje ya sanduku na jinsi unavyofuatilia mambo ya kitaifa. Hata hivyo, nadhani mtazamo wako wa kuona kila tukio kubwa la soka nchini kama mbinu ya kisiasa ya kupumbaza watu ni mtazamo uliopitwa na wakati, kwani soka la sasa nchini Tanzania limeshaacha kuwa burudani tu na limekuwa tasnia rasmi ya kibiashara inayojitegemea.
Kuhusu suala la Sele Mwalimu au mchezaji mwingine yeyote kukuzwa, huo ni mkakati wa kibiashara wa kawaida unaojulikana kama "hype" na uuzaji wa chapa. Vilabu vya Simba na Yanga kwa sasa vinaendeshwa kama kampuni; vinahitaji namba kubwa za wafuatiliaji mtandaoni ili kuvutia wadhamini wenye fedha nyingi, na siyo kwa ajili ya kufunika kesi za mahakamani au matukio ya kisiasa kama unavyohisi.
Kwenye soka la kisasa, mchezaji hahitaji kuwa mfungaji bora namba moja au tatu kwenye ligi ili klabu itengeneze naye biashara. Ushawishi wa mchezaji nje ya uwanja na uwezo wake wa kuvutia mashabiki ni mtaji mkubwa wa kibiashara unaosaidia kuuza jezi na tiketi za mechi, jambo ambalo ndilo linalomfanya Hersi au wasemaji wa klabu kupiga kelele kila uchao kwa maslahi ya vilabu vyao na sio maagizo ya kisiasa.
Wazo lako la kutaka kuziblok au kuzisusia hizi timu mbili kwa mwezi mmoja linaweza kuonekana kama adhabu kwao, lakini kiuhalisia litakuwa ni kujiumiza sisi wenyewe kiuchumi. Tasnia ya soka kwa sasa inaajiri maelfu ya Watanzania wenzetu kuanzia wachezaji, waandishi wa habari, wauzaji wa vifaa vya michezo, hadi mama ntilie na bodaboda, hivyo kususia soka ni kuua vipato vya wananchi wa kawaida wanaotafuta riziki kwa jasho lao.
Mkuu wangu, naelewa kwanini umekuwa frustrated na upo sahihi kabisa kuwa frustrated, lakini kusingizia kila kitu kuwa kinatumiwa na serikali ni kuwakosea Watanzania wenzako heshima na kukufanya wewe uonekane huna tofauti na kina Mwashambwa na wenzake.