Maadui wakubwa wa Taifa hili kwa sasa

Maadui wakubwa wa Taifa hili kwa sasa

Life2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,387
Reaction score
4,880
Kama hukupoteza ndugu yako 29 Oct mwambie Mungu asante, ile siku kwa kifupi ni siku mbaya ni siku ambayo shetani na majeshi yake walivuna haswa damu za Watanganyika.

Endeleeni kupumzika kwa amani makamanda, leo mnazingiziwa kila kitu, mlikua na Bunduki, Mabomu, Vifaru, Air to Air missiles, Land to Air Missile, Air defences weapons, ICBM etc.

Enzi za Mwalimu Nyerere alitwambia maadui watatu wa taifa ni hili ni:
Ujinga
Umaskini
Maradhi

Nafikiri kwa sasa tumefanikiwa angalau kwa asilimia 75 kupunguza changamoto hizo, Shule, vyuo vimekua vingi, hospitali zimekua nyingi, vipato vya watu vimekua angalau milo miwili sio haba kwa Watanganyika.

Bahati mbaya wameibuka maadui wengine ambao ni hatari kuliko hata silaha za nyuklia ambazo ni:
Vyombo vya habari.
Waandishi wa habari
Baadhi vya viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Wasomi
Viongozi wa ngazi za juu Wastaafu.
Timu za mipira haswa football.
Wabunge
Mawaziri.etc

Hao ni wengineo wamekua ni hatari mno kwa watanganyika wapo radhi taifa hili lipigwe mnada kisa tamaa zao binafsi.

Wapo radhi Watanganyika wote mfe kisa kuendekeza uchawa na ujinga ujinga usio na mantiki kwa taifa hili.

Kuanzia asubuhi mpaka jioni wao ni kusifu na kuabudu tu, tena bora wangefanya yao kwa sifa na utukufu kwa Mungu. La hasha wanafanya hayo kwa sifa za Binadamu.

Tukiweza kudili na hao maadui wapya tutakua tumekomboa taifa hili.
 
Mwanafalsafa Julian Brenda amewahi kusema usaliti mkubwa ni wa wasomi kuacha kutafuta ukweli na kuanza kutafuta madaraka au fedha.
 
Umewasahau Wazee kuanzia 1950-75.
Hiki jizazi kina watu wajinga sana wengi hawataki kabisa Changes.
 
Back
Top Bottom