Tuwafiche wapi watoto wetu wa kike?

Tuwafiche wapi watoto wetu wa kike?

stable woman

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
3,883
Reaction score
4,484
Habarini!?

Nimesikitishwa na tukio nililoliona wiki hii kwenye pitapita zangu ni binti Wa darasa la 4 amekataa shule akitaka aendelee na maisha ya kujiuza!

Ni binti ambae kwa mahesabu ya haraka atakuwa na miaka12 na kamwili kakuvutia kalikoletwa na kuvunja ungo mapema!

Baada tu ya kuvunja ungo ndipo akafundwa yale mambo ya pwani kuhusu ukubwa na tabia zake tangu hapo zikawa si nzuri!

Mtoto huyu kulala kwenye vigodoro ni kawaida kwake kupigwa mitungo na mengineyo!

Je hizi tamaduni zetu hatuwezi kuziacha? Au kupunguza makali ya mafunzo? Mbona watoto wetu wanaharibikiwa baada ya kufunzwa?

Tuwafiche wapi watoto wetu Wa kike?

Nawasilisha.
 
si ndo jando,sijui kufundwa huku mnajua system imebadilika unategemea nini
 
Ndio kwanza vigodoro vinasambaa kama bushfire
 
Aisee mimi natamani niwameze watoto wangu maana mtaani kuna vitoto vivulana nasikia vina tabia ya kuwafanya watotot wadogo wadogo including wakiume!!Nimetamani kupasuka leo baada ya kupata izo habari, halafu vikikataliwa vinawapiga hao watoto. May God protect our kids, Amen.
 
jiulize
hizo tamaduni zilianza leo? na miaka hiyo iliyopita waliofundwa walikuwa wanafanya haya ya waleo?
 
Dawa ni uwajibikaji wa wazazi na walezi.

Watu wasiwe wanazaa hovyo hovyo kama hawawezi kulea (ingawa najua hii ni utopia yangu tu).
 
Asiefunzwa na *****, hufunzwa na ulimwengu. Ifike mahali tough love ihusike!
 
inatia uchungu jaman yan darasa la nne??? mtoto bado mdogo jaman
 
jiulize
hizo tamaduni zilianza leo? na miaka hiyo iliyopita waliofundwa walikuwa wanafanya haya ya waleo?

Mimi naona Wa kipindi hiki wameharibika sana sijui kwanini? Mila zilikuwepo tangu!
 
Habarini!?
Nimesikitishwa na tukio nililoliona wiki hii kwenye pitapita zangu ni binti Wa darasa la 4 amekataa shule akitaka aendelee na maisha ya kujiuza! Ni binti ambae kwa mahesabu ya haraka atakuwa na miaka12 na kamwili kakuvutia kalikoletwa na kuvunja ungo mapema!
Baada tu ya kuvunja ungo ndipo akafundwa yale mambo ya pwani kuhusu ukubwa na tabia zake tangu hapo zikawa si nzuri! Mtoto huyu kulala kwenye vigodoro ni kawaida kwake kupigwa mitungo na mengineyo!

Je hizi tamaduni zetu hatuwezi kuziacha? Au kupunguza makali ya mafunzo? Mbona watoto wetu wanaharibikiwa baada ya kufunzwa? Tuwafiche wapi watoto wetu Wa kike?


Nawasilisha

Huo ndo utamaduni wa mwafrika shule asomw kwani yeye mzungu!
 
Mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha kamwe....!!!!
 
  • Thanks
Reactions: ram
From no where tu mtoto akatae shule? Tabia inafugwa kama kitambi pwani.
 
Unaweza kuwa mkali na uso mkavu, mtoto akaharibika, waweza kuongesha upendo, umlee mtoto kwa kumeinyesha upendo na kumwelekeza kwa upendo pia akaharibika. Unaweza tumia msahafu/biblia na maombi kwa Sana, mtoto akaharibika...hata sijui wazazi mnatumia fomyula gani katika malezi.
 
Wewe Sio pwani tu Njoo mitaa ya villa Mwanza ujionee majanga,huku Sio std4 huku hawajaenda xule kabisa vitoto vya miaka 9 mibaba inaponea huku so nijanga lakitaifa br tuombe sana mungu.
 
jiulize
hizo tamaduni zilianza leo? na miaka hiyo iliyopita waliofundwa walikuwa wanafanya haya ya waleo?

dunia imebadilika sn thats y inafikia wakat hata tamaduni ambazo mwanzo zilikuwa nguzo za maadili zimebadilika kuwa uvunjifu wa maadili, so inabidi tuziangalie upya tujiulize wapi tunakosea
 
Dear children, keep away from anything that might take God's place in your hearts...!!
 
Back
Top Bottom