Tuunganishe Ukerewe na nchi kavu

Tuunganishe Ukerewe na nchi kavu

1. Kuunganisha Ukerewe na Mwanza na kuunganisha Ukerewe na Mara wapi pana unafuu wa gharama?

2. Kwa kigezo cha idadi ya watu katika mkoa kutengeneza consumer market, Mara ina faida kiuchumi kwa Ukerewe kuliko Mwanza. Japokuwa Mwanza inakadiriwa kuwa na watu 2ml dhidi ya Mara 1.9m bado Mara inaizidi Mwanza kwa kuwa inapokea watu wa nchi jirani wanaovuka mpaka mara kwa mara kuja kutafuta huduma Mara. Ukerewe ina utajiri wa uchumi wa bluu, mbogamboga, ndege wa aina mbalimbali, matunda, ndizi nk, vyote hivi vinahitaji walaji wengi. Mara imepakana na nchi jirani hivyo Mara itakuwa na competitive advantage na comparative advantage over Mwanza kuhusu Ukerewe.

3. Dialects za Mara kama Kijita, Kiruri, Kikwaya, ni dialects zinazoshabihiana na Kikerewe kuliko Kisukuma. Kumbe asili ya Ukerewe ni Mara kuliko Mwanza.

Consider this Case Study.
Kutoka Wilaya ya Mafia kwenda Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani, mwananchi analazimika kwenda Wilaya ya Rufiji, aje Wilaya ya Kibiti, aje Wilaya ya Mkuranga, aje Mkoa wa Dsm ndipo aende Mkoa wa Pwani Kibaha. Kumbe basi kutoka Mafia mtu anatoka nje ya Mkoa wa Pwani anaingia Mkoa wa Dsm alafu anatoka Mkoa wa Dsm ndipo aende Mkoa wa Pwani Kibaha palipo Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani!!

Mafia ipelekwe Mkoa wa Dsm na Ukerewe ipelekwe Mkoa wa Mara.
Sidhani kama wilaya kuwa mkoa fulani kunazuia biashara na mkoa mwingine. Ukerewe kuwa mwanza kuzuie biashara na mkoa wa mara?? Dialects za kikerewe hazishabihiani na za kijita au kiruri kulko na za wazinza walioko sengerema. Ukihusianisha hivyo bora uchukulie wazinza, wahaya na wakerewe kulko wakerewe, wajita na waruri au wakwaya.
 
Nakataa wazo la kuipeleka Ukerewe mkoa wa Mara, lakini kutangeneza daraja pale Ngoma/Kisorya ni wazo la msingi sana. Ukerewe inafanya biashara ya chakula na mkoa wa Mara kuliko Mwanza. Ukweli ni kwamba mkoa wa Mara unaitegemea UK kwa chakula kwa kiwango kikubwa na wao hawawezi kukanusha hili. Kwa upande wa Mwanza ni rahisi kwenda kwa meli kuliko kutumia hii barabara ya kupita Bunda kwani itahitaji masaa 5 wakati kwa meli ni masaa 2.30 hadi 3 na kama italetwa fast ferry itatumia saa 1 tu.
Naunga mkono wazo lako 💯 kwa 💯
 
Ukabila unawatesa sana Watanzania kwa sasa kuliko wakato wowote. Kwa kuwa Wakerewe na Wakara wanasikilizana kilugha na Wajita wa Bunda ndio maana mnatamani sana hili litokee bila kuzingatia Wazinza, Walongo na Wasumbwa nao wana nasaba na nchi jirani za Uganda na Rwanda.

Kwa busara na kuzingatia upunguzaji wa gharama za kiutawala na mzigo kwa walipa kodi ingekuwa ni vyema kubadili tu jina la mkoa wa Geita na kuwa mkoa wa Chato ila makao yake makuu kuwa Geita kwa kumega kipande cha wilaya y a Sengerema ili kuepuka kuanzisha mkoa mpya.

Wilaya ya Kwimba ni mfano ulio hai kwa kuwa makao yake makuu yako Ngudu. Viongozi na wanannchi waanche ubinafsi kwamba lia kiongozi atokeapo paanzishwe mkoa sio vizuri mnawabebesha wananchi mzigo usiowahusu na hauna tija.

Mpaka sasa kuna mkoa mkubwa kuliko yote Tanzania umenyamaza kimya (TABORA) maana haujawahi kudai kugawanywa ila uliongezewa majukumu kwa kupewa eneo la Kaliua lililokuwa kwa kiasi kikubwa kwenye mkoa wa Kigoma lakini kwa sasa ni wilaya ya mkoa wa Tabora.

Msigawe mikoa kwa kufuata asili ya wenyeji walioko maeneo hayo bali kwa kuzingatia mahitaji ya huduma za kijamii na uwezo wa kiuchumi. Wanasiasa mnaharibu mstakbari wa nchi
Umeongea ukweli mtupu. Kuna Tabora, Morogoro na Lindi hii mikoa ni mikubwa sana ila huwezi kuwasikia wanalamimika.
 
Dialects za Mara kama Kijita, Kiruri, Kikwaya, ni dialects zinazoshabihiana na Kikerewe kuliko Kisukuma. Kumbe asili ya Ukerewe ni Mara kuliko Mwanza. Dialects za Mara kama Kijita, Kiruri, Kikwaya, ni dialects zinazoshabihiana na Kikerewe kuliko Kisukuma. Kumbe asili ya Ukerewe ni Mara kuliko Mwanza. Lakini pia Kikerewe kwa uchache kina misamiati ya Kihaya kuliko Kisukuma na kuna simulizi kwamba asili ya Wahaya ni Ukerewe.
Kama vile unapoint hivi🤔
 
Hapa watu wamejikita kujadir kuhusu swala la mipaka ya kiutawala wakasahau swala la kuonganisha aridhi(kijenga daraja) ili kurahisisha huduma ya usafirishaji. na jambo la muhimi ni daraja lijengwe wapi kati ya mwanza-ukerewe au bunda- ukerewe?
 
Hapa watu wamejikita kujadir kuhusu swala la mipaka ya kiutawala wakasahau swala la kuonganisha aridhi(kijenga daraja) ili kurahisisha huduma ya usafirishaji. na jambo la muhimi ni daraja lijengwe wapi kati ya mwanza-ukerewe au bunda- ukerewe?
Lengo ni kuifungua wilaya ya Ukerewe iwe inaingilika masaa 24. Waanze na daraja fupi hapo Kisorya ambapo ni km chache zaidi kuliko km 54 kuiunganisha na ilemela Mwanza.
 
Dialects za Mara kama Kijita, Kiruri, Kikwaya, ni dialects zinazoshabihiana na Kikerewe kuliko Kisukuma. Kumbe asili ya Ukerewe ni Mara kuliko Mwanza. Dialects za Mara kama Kijita, Kiruri, Kikwaya, ni dialects zinazoshabihiana na Kikerewe kuliko Kisukuma. Kumbe asili ya Ukerewe ni Mara kuliko Mwanza. Lakini pia Kikerewe kwa uchache kina misamiati ya Kihaya kuliko Kisukuma na kuna simulizi kwamba asili ya Wahaya ni Ukerewe.
Hii kampeni inakupa faida gani kichwani? Au ni nafasi ya kueleza kila unchohisi unakifahamu. Ukabila tu! Kikerewe kinafanana sana na kihaya na kizinza na siyo lugha zote za mkoa wa Mara. lugha ya kijita na kikerewe zinashabihiana kwa maingiliano ya kiutawala wakati wa watemi. Mtemi wa Ukerewe alikuwa na himaya hadi kwa wajita na ndo maana unasikia hata majina yakifanana. Hayo unayoyaeleza ni hadithi zako tu!

Ulichotakiwa kuombea kitokee ni daraja na kuiunganisha Ukerewe na mkoa wa mara kwa kuwa hiyo ni barabara kuu iliyo na sifa za kuunganisha mkoa wa Mwanza na mara.
 
Huna hoja hata kidogo katika bandiko lako lote.
Mifano ya Lesotho na eSwatini wala haileti maana yoyote hapa, sasa sijui wewe uelewa wako upo vipi hasa.

Unaingiza "ukoloni" hapa kwa mantiki ipi? Kwani kuwepo na maji kati ya sehemu mbili katika nchi hiyo hiyo kunafanya pawe na mipaka kati yake?

Huu sio mjadala ninaoweza kupoteza muda wangu nao.
Consider this Case Study.
Kutoka Wilaya ya Mafia kwenda Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani, mwananchi analazimika kwenda Wilaya ya Rufiji, aje Wilaya ya Kibiti, aje Wilaya ya Mkuranga, aje Mkoa wa Dsm ndipo aende Mkoa wa Pwani Kibaha. Kumbe basi kutoka Mafia mtu anatoka nje ya Mkoa wa Pwani anaingia Mkoa wa Dsm alafu anatoka Mkoa wa Dsm ndipo tena aende Mkoa wa Pwani Kibaha palipo Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani!!

Mkuu, ukiendelea kukataa kuelewa basi nadhani toba inakuhusu!
 
Wewe ndiye msemaji wa hao wana Ukerewe?

Kama kweli ndio wamekutuma upuuzi huu watakuwa wamepungukiwa akili kichwani. Inaonekana siku hizi 'furu' (samaki wadogo) wamekuwa adimu na akili za hao wakerewe zimepotea kama wewe ni mmoja wao; na tena wanakuamini kuwa na mawazo mgando kama haya.
As a leader it is also a mistake to think that you need to have all the right answers all the time. Trying to be right all the time is stressful, slows progress and causes procrastination Skip Prichard, (2016).

Nakunukuu:
"Kama kweli ndio wamekutuma upuuzi huu watakuwa wamepungukiwa akili kichwani" NA "Akili za hao Wakerewe zimepotea kama wewe ni mmoja wao"

Jibu:
Ukerewe Island in Lake Victoria is the only place in the planet presumed to have produced about 70 professors who are natives of the 38 archipelago.

Mkuu,

Nadhani Tiktok panakufaa zaidi kuliko JF. Tukufanyie send-off urudi Tiktok?
 
Consider this Case Study.
Kutoka Wilaya ya Mafia kwenda Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani, mwananchi analazimika kwenda Wilaya ya Rufiji, aje Wilaya ya Kibiti, aje Wilaya ya Mkuranga, aje Mkoa wa Dsm ndipo aende Mkoa wa Pwani Kibaha. Kumbe basi kutoka Mafia mtu anatoka nje ya Mkoa wa Pwani anaingia Mkoa wa Dsm alafu anatoka Mkoa wa Dsm ndipo tena aende Mkoa wa Pwani Kibaha palipo Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani!!

Mkuu, ukiendelea kukataa kuelewa basi nadhani toba inakuhusu!
Aisee, nadhani utakuwa na upungufu fulani.

Kwanza mada uliyoleta hapa haina mantiki kabisa. Hoja uliyotanguliza mbele ni kuwepo na "muunganiko wa nchi kavu" kuwa ndiyo kigezo cha hayo unayoyapigia kampeni hapa! Sababu ulizotanguliza kwa Ukerewe kuwekwa Mara ni sababu hafifu kabisa na wala hazina kitu cha kuangalia hapo kwamba ni faida kwa wilaya kuwepo huko unakopapendekeza wewe.

Kuna jambo unalificha, hutaki kuliibua hapa linalokufanya uibue hoja hafifu namna hii.

Lakini zaidi ya yote, ni kukosa kwako uwezo wa kutetea hoja kiasi kwamba inakulazimu useme hadi uongo katika mambo usiyokuwa nayo ufahamu.
Sasa nikueleze ukweli wako: Huko unakodhani Ukerewe itapata nafuu usitegemee unafuu huo, tena ndiko itakakonyongwa zaidi. Na kwa bahati mbaya sana, tunapokuwa na watu kama wewe katika uongozi ndani ya wilaya hiyo ndipo wilaya inapopoteza matumaini yote kabisa.

Kama viongozi wameshindwa/wameogopa kupigania maslahi ya wilaya yao huko waliko sasa, wataweza vipi kuyapigania huko kwingine?

Simama upambane, acha kukimbia mapambano huko wilaya iliko sasa. Taratibu zipo wazi kabisa katika kusimamia maslahi ya wananchi mahali popote. Kwa uzembe wenu, mnaacha kusimama na kuyapigania maslahi hayo, mnaishia tu kuja huku pembeni na kutafuta njia zisizokuwa na manufaa yoyote kwa wananchi.

Kama bado hunielewi, utakuwa unakichwa cha jiwe.
 
Ninakunukuu,
Mpaka sasa kuna mkoa mkubwa kuliko yote Tanzania umenyamaza kimya (TABORA) maana haujawahi kudai kugawanywa ila uliongezewa majukumu kwa kupewa eneo la Kaliua lililokuwa kwa kiasi kikubwa kwenye mkoa wa Kigoma lakini kwa sasa ni wilaya ya mkoa wa Tabora.

Jibu.
Mkoa wa Tabora ulimegwa kutengeneza mkoa wa Katavi kufuatia Kapuya na Sitta kuogopana, ikabidi Kapuya aangukie Katavi.

Msigawe mikoa kwa kufuata asili ya wenyeji walioko maeneo hayo bali kwa kuzingatia mahitaji ya huduma za kijamii na uwezo wa kiuchumi. Wanasiasa mnaharibu mstakbari wa nchi.

Jibu.
Hakuna serikali inagawa mikoa yenyewe, serikali inaweka vigezo, wanaoomba mikoa igawanywe ni wananchi wenyewe alafu serikali inaangalia kama vigezo vinatimia, visipotimia hata wananchi wakiandamana hawapewi mkoa.
Chattle iliombwa na muombolezaji
 
Sidhani kama wilaya kuwa mkoa fulani kunazuia biashara na mkoa mwingine. Ukerewe kuwa mwanza kuzuie biashara na mkoa wa mara?? Dialects za kikerewe hazishabihiani na za kijita au kiruri kulko na za wazinza walioko sengerema. Ukihusianisha hivyo bora uchukulie wazinza, wahaya na wakerewe kulko wakerewe, wajita na waruri au wakwaya.
Imbalance of historical perspectives.
 
Consider this Case Study.
Kutoka Wilaya ya Mafia kwenda Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani, mwananchi analazimika kwenda Wilaya ya Rufiji, aje Wilaya ya Kibiti, aje Wilaya ya Mkuranga, aje Mkoa wa Dsm ndipo aende Mkoa wa Pwani Kibaha. Kumbe basi kutoka Mafia mtu anatoka nje ya Mkoa wa Pwani anaingia Mkoa wa Dsm alafu anatoka Mkoa wa Dsm ndipo tena aende Mkoa wa Pwani Kibaha palipo Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani!!

Mkuu, ukiendelea kukataa kuelewa basi nadhani toba inakuhusu!
Ukitoka Kiteto, Manyara kwenda Bahati Makao Makuu ya Mkoa wa Manyara, inabidi upite Wilaya za Kibaigwa, Chamwino, Bahi na Dodoma ambazo zipo Dodoma.

Kwa hiyo mgonjwa akipata Rufaa kutoka Wilaya ya Kiteto, itabidi aipite hospitali ya Rufaa ya Dodoma akiwaishwa kwenda hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara iliyopo Babati Mjini
 
Back
Top Bottom