Tutavikumbuka Vyombo vya Habari Tanzania na baadhi ya Viongozi wa Dini kwa kuliaibisha Taifa 2020

Superbug

JF-Expert Member
Jan 31, 2018
12,417
30,927
Kwakweli katika mambo ambayo naona ni doa kubwa katika Nchi yetu kwa mwaka huu wa 2020 na pengine miaka hii mitano yote ya utawala wa Rais Magufuli ni namna viongozi wa dini walivyoufyata mkia mbele ya dola kandamizi. Ukiwatoa viongozi wachache Kama MWAMAKULA na BAGONZA pengine na wachache wengine ambao labda sijawasikia waliobaki wootee ni machukizo mbele ya altare ya bwana.

Tumeshuhudia kwa uwazi kabisa jinsi serikali ya CCM ilivyowaonea wapinzani kana kwamba wao sio watanzania wa nchi hii. Pamoja na yote mabaya yaliyotendwa na serikali ya CCM ikiwemo mambo ya sintofahamu za kina Lissu, kushambuliwa na Ben kupotezwa viongozi wa dini wamebaki wakiisifu serikali hiyo bila aibu na kuikaribisha kwenye madhabahu za bwana. Haya mambo yamewapotezea heshima kubwa watu wa dini na kufanya waonekane wako kimaslahi zaidi na kwamba dini ni sehemu ya kujifichia ila ni wapigaji tu kama wapigaji wengine.

Waandishi wa Habari
Hawa wao ni woga na hofu yaani Mambo ya Lissu hayatangazwi utadhani Lissu ni muasi wa M23 lakini Mungu alivyo wa ajabu pamoja na kumzima Lissu bado amesikika sawia kwa viwango vilevile vya mgombea wa CCM. Hebu jiulize Lissu angepewa coverage sawa na mgombea wa CCM kwa 50:50 ingekuwaje?

Ukuu wa Mungu haufananishwi na kitu kingine.
 
Wewe hapo ulipo kama ni baba wewe ndo mchungaji wa familia yako na wengine wote ni waumini, hivyo kanisa tosha kabisa huko unakodhani kuna kanisa unaenda kulipia gharama za mazishi yako siku ukifa uonekane kwamba umezikwa na watu wa kanisa, kitu ambacho hakikusaidii mbele ya kiti cha hukum.

Swali kanisa alilokuwa anasali Ibrahim ni lipi? Funua maandiko utakuta ni familia yake yote.
 
Viongozi wengi wa dini ni wazinzi,mafisadi,washerati,walarushwa,wajasiriamali,wanafiki,wachawi na wazandiki wametufanya kukosa imani nao wanatumia maandiko kupotosha umma.
 
Acheni kumuingiza Mungu kwenye ujinga bhana, halafu ni nani wa kumpa adui coverage ya 50/50 ?? Lissu ni mtu mbaya kuliko hata JPM Hana msimamo na yupo manipulated Sana na watu wengine Kwa maslah ya taifa huyo hafai hata kidogo. Nilipofatilia nyendo zake pale pale nikawapa credit wale unknown , wafanyakazi shida yao nyongeza ya mshahara , vijana shida yao ajira Yees somehow can be blamed...lakini sio full scale kama wanavyojitanabaisha watu tubamake lyfe bila hata hzo ajira.... Ukitaka mshahara mnono piga chini kazi njoo kitaa
 
Watu wenye busara hawawezi kuunga mkono wavuta bangi na vichaa,
CHADEMA hakijui nini kinafanya, na hawajui wnataka nini.
Kama hamvuti bangi twambieni pesa za ruzuku zimetumika wapi na pesa za michango ya wabunge ziko wapi?
 
Muulize lijuakali
Watu wenye busara hawawezi kuunga mkono wavuta bangi na vichaa,
Chadema hakijui nini kinafanya, na hawajui wnataka nini.
Kama hamvuti bangi twambieni pesa za ruzuku zimetumika wapi na pesa za michango ya wabunge ziko wapi?
 
Acheni kumuingiza Mungu kwenye ujinga bhana, halafu ni nani wa kumpa adui coverage ya 50/50 ?? Lissu ni mtu mbaya kuliko hata JPM Hana msimamo na yupo manipulated Sana na watu wengine Kwa maslah ya taifa huyo hafai hata kidogo. Nilipofatilia nyendo zake pale pale nikawapa credit wale unknown , wafanyakazi shida yao nyongeza ya mshahara , vijana shida yao ajira Yees somehow can be blamed...lakini sio full scale kama wanavyojitanabaisha watu tubamake lyfe bila hata hzo ajira.... Ukitaka mshahara mnono piga chini kazi njoo kitaa
Idiot
 
Wengi Wana makando kando wamejifiachia kwenye dini ccm ni kichaka Cha kufichia wahalifu, mafisadi,matapeli,wakimbizi ili uwe salama Ni lzm uunge juhudi.Wengine wamejenga nyumba zao za ibada viwanja vya wazi, wengine utumia dini kukwepa Kodi,wengine ishu za uraia baada ya kuunga juhudi na pasipoti zao walirudishiwa na faili la uraia kufungwa, wengine usajili wa huduma zao Ni kwa wino wa pencil msajili anaweza tii maagizo usajili ukafutwa Hadi usiku wa manane.
Viongozi wa dini wa Kikristo wamemuaibisha Kristo kwa kula karamu haramu zilizotolewa kwa masanamu.
Mtu yeyeto anaeshiriki unga juhudi udhalimu sehemu huyo ni mjumbe wa shetani
 
Watu wenye busara hawawezi kuunga mkono wavuta bangi na vichaa,
CHADEMA hakijui nini kinafanya, na hawajui wnataka nini.
Kama hamvuti bangi twambieni pesa za ruzuku zimetumika wapi na pesa za michango ya wabunge ziko wapi?
Vijana wa Bashiru
 
Na kukemea maonevu dhidi ya raia..Serikali dhalimu

Wakati Magufuli anaingia madarakani sukari ilikuwa kati ya 800 na 1200 Kwa Kilo Moja. Mwaka 2016, Magufuli akaingilia Biashara ya sukari na sukari ikapanda hadi 2400.

Mwaka 2016 Magufuli alisema Matajiri wataishi kama Mashetani...alidhamiria watanzania wakose pesa, na hakusema masikini wataishi kama malaika
. Akafanya matendo makuu ya bomoa bomoa kimara bila fidia, akapora fedha za wafanyabishara za Bureu De Change, maelfu ya wafanyakazi wakakosa ajira. Mpaka leo Magufuli hajatoa riporti kwa umma kuwa ni pesa kiasi gani alichukua?

Mwaka 2019, Magufuli akaingilia tena na Sukari ikapanda, sasa sukari ni 2600 hadi 2800 Tshs

Ukiangalia mikoa Pwani, Kibaha, Chalinze, etc...Sukari ni muhimu na kipato ni kidogo.

Angalia sukari ya Malawi, Brazil, Thailand ni rahisi kuliko ya Tanzania. Why..Mfumo wa kodi ni mbovu

Burundi na Rwanda kuagiza gari ni rahisi zaidi kuliko Tanzania, wakati magari yao yanapita bandari ya Dar es salaam.

Pia ukiangalia Ngome za CCM Chalinze, Morogoro Dodoma, Shinyanga, .., nyumba za tembe ni nyingi...Gharama za ujenzi ni kubwa mno. Cementi ni ghali sana... Hakuna sababu cementi kuwa ghali sana. Maana ni mali ghafi ya hapa hapa nchini...Mfano, Mtu akiagiza Cementi Pakistani, anakuja kuuza bei chini kuliko Simba au Twiga Cementi. Bado cement ya nje kuna usafirishaji, kodi ya taifa lao na VAT ya Tanzania. Kama alivyosema Mh. Tundu Lisu, kuna tatizo TRA....
 
Wakiisifia chadema wanakuwa siyo wazinzi?
Hujui.....Wakiwa upande wetu, hao siyo kinyume chetu!.......Sijui.....Hata kwa macho huoni?
Screenshot_20200724-175445.jpg
 
Kwakweli katika mambo ambayo naona ni doa kubwa katika Nchi yetu kwa mwaka huu wa 2020 na pengine miaka hii mitano yote ya utawala wa Rais Magufuli ni namna viongozi wa dini walivyoufyata mkia mbele ya dola kandamizi. Ukiwatoa viongozi wachache Kama MWAMAKULA na BAGONZA pengine na wachache wengine ambao labda sijawasikia waliobaki wootee ni machukizo mbele ya altare ya bwana.

Tumeshuhudia kwa uwazi kabisa jinsi serikali ya CCM ilivyowaonea wapinzani kana kwamba wao sio watanzania wa nchi hii. Pamoja na yote mabaya yaliyotendwa na serikali ya CCM ikiwemo mambo ya sintofahamu za kina Lissu, kushambuliwa na Ben kupotezwa viongozi wa dini wamebaki wakiisifu serikali hiyo bila aibu na kuikaribisha kwenye madhabahu za bwana. Haya mambo yamewapotezea heshima kubwa watu wa dini na kufanya waonekane wako kimaslahi zaidi na kwamba dini ni sehemu ya kujifichia ila ni wapigaji tu kama wapigaji wengine.

Waandishi wa Habari
Hawa wao ni woga na hofu yaani Mambo ya Lissu hayatangazwi utadhani Lissu ni muasi wa M23 lakini Mungu alivyo wa ajabu pamoja na kumzima Lissu bado amesikika sawia kwa viwango vilevile vya mgombea wa CCM. Hebu jiulize Lissu angepewa coverage sawa na mgombea wa CCM kwa 50:50 ingekuwaje?

Ukuu wa Mungu haufananishwi na kitu kingine.
Kati ya watu ambao siwaheshimu kwa sasa ni viongozi wa dini ukiondoa hao baadhi!
Kwa ujumla hawana msaada wowote katika kudhibiti uovu unaofanywa na wenye mamlaka.
Ni watu waliojipa uwakilishi wa Mungu lakini wapo kwa maslahi yao binafsi!
 
Kati ya watu ambao siwaheshimu kwa sasa ni viongozi wa dini ukiondoa hao baadhi!
Kwa ujumla hawana msaada wowote katika kudhibiti uovu unaofanywa na wenye mamlaka.
Ni watu waliojipa uwakilishi wa Mungu lakini wapo kwa maslahi yao binafsi!
Hapa ulikuwa unawapigia hadi magoti
Screenshot_2020-09-10-10-53-08.jpeg
 
Back
Top Bottom