Tutakumbushana tena 2025 Magufuli kama atakubali kuachia madaraka basi atalazimisha kutuachia Rais anayependa yeye

Siwezi puuza huu uzi watu waoga huwa wanaweka kinga ili wasiumizwe ila kuna mawili
1.KUKOMAA MADARAKANI
2.AU KUKIMBIA NCHI/KUISHI UHAMISHONI ILI WATU WASILIPE KISASI
3.KUMCHAGUA SHOSTI MWENYE MAELEKEZO YA KUMLINDA kama mtoa mada asemavyo humu
1 na 2 ndo zenye usalama zaidi
 
Viongozi wa awamu hii wanaishi kwa woga sana, kama vile hajashinda uchaguzi. Jana Majaliwa alikua anapita, nusu saa kabla bara bara iliachwa wazi na traffic, magari yote yalipack pembeni. Majaliwa alipita kama mwewe.
Hili nalo linakuumiza?
Dah
 
2.Paul Makonda, kwa Muda huu anatuzuga kamsahau lakin kwa Mabalaa na Maajabu ya Tanzania ukashangaa 2026 anapigiwa mizinga
Huyu hana shahada ya chuo kikuu kama Katiba inavyotaka.. Labda kwa kuwa awamu hii Katiba "imepumzishwa".

Ila ikimpendeza anaweza kununua PhD mapema
 
Mbona tunasikia Nyerere alishindwa kumuweka mtu anayemtaka,Mkapa naye alishindwa na mwisho Kikwete nae pia alishindwa.
 
Sijui kama tutafika 2025 salama, maana kwa ninavyo uona mwelekeo kama dereva gari limesha mshinda na limeshaacha njia.

Sio kwa hali hii ya sasa hivi mpaka kufikia hatua "TRA KUANZISHA KODI ZA VITANDA". Wenyewe kwa lugha ya malkia eti wanaita "BED LEVY".
Mshamba kama we we ndio unaishangaa hiyo kodi. Kama ungekuwa " well informed " ungelijua kuwa Tanzania tulichelewa sana kuwa na hii kodi.
 
Kwa la ushoga Mungu alitupitisha mbali kwa kutomchagua Lissu!


Tatizo ni katiba na sio Lissu, Katiba yetu (the national constitution) inaweka wazi juu ya falagha ya mtu, kwa kauli hiyo hatua inayofuata ni kutangaza Ushoga ni ruksa.

Unamlaumu Lissu wakati katiba yenyewe ipo mid-way toward ushoga !!!. Katiba ingesema wazi kwamba italinda faragha ya mtu lakini ushoga ni jinai hapo tungekuwa salama.
 
Atajaribu but hatafanikiwa.
Hata sisi wananchi wenyewe tukishindwa kumzuia, rafiki zetu wazungu watahakikisha hicho hakitokei!
 
Kuna Vitetesi fulan japo 2025 ni mbali ila kwa uoga wa Rais Magufuli, endapo akikubali kuachia madaraka basi atauingilia Uchaguzi kuanzia mchakato wa Mgombea ndani ya Chama hadi Uchaguzi Mkuu kwa ujumla kuhakikisha anayebaki ni yule atakayefanya yafuatayo

1. Hataruhusu kujadiliwa kwa aliyofanya rais mstaafu

2. Hataibua hoja au hataruhusu hoja za kuhoji matumizi yasiyofuata taratibu za Manunuzi kama vile ununuzi wa Ndege, na ujenzi wa miradi mbali mbali Ambayo haikufuata utaratibu na hatuoni uwazi

3. Hataruhusu kuhoji haki za watu zilizopotea na haki za watu waliouwawa au kufichwa kabisa

4. Hataruhusu kuhojiwa Kwa wafanya biashara Walidhulumiwa na serikali na wengine kufungwa kwa kisingizio cha Uhujumu uchumi na utakatishaji pesa,

5. Hataruhusu kabisa uwazi wa namna yeyote

KATIKA WATU ANAOWAONA WATAIWEZA KAZI HIYO

1. Bwana Hussein Mwinyi wa Zanzibar, huyu atakuwa ni yule wa Ndiyo mzee wangu mstaafu pumzika usiguswe

2. Paul Makonda, kwa Muda huu anatuzuga kamsahau lakin kwa Mabalaa na Maajabu ya Tanzania ukashangaa 2026 anapigiwa mizinga

3. Kassim Majaliwa, Huyu naye yuko Obedient Sana kwa Magufuli

4. Hamis kigwangalla,


Si lazima jina liwe kwenye hayo ila atapitishwa mwenye sifa za hao

Tukumbushane July 2025

Mungu atuweke na yeye amuweke pia maana ya Mungu Mengi hapa kati kati

Amen

Britannica
Mjihadhali kutumia point zilezile zilizopelekea mkashindwa vibaya sana kwenye chaguzi zilizopita!

Tafuta point mpya. Maana hizi za watu kupotea, TRA, kununua ndege, maendeleo ya vitu, eti kuchukua hela za watu na pia mambo ya demokrasia - hizi haziwapi kura yoyote!

Tafuta vitu vitakazo wapa ushindi na ushawishi. Bila hivyo unga juhudi.
 
Ulitaka kumpopoa mawe e🤔
Viongozi wa awamu hii wanaishi kwa woga sana, kama vile hajashinda uchaguzi. Jana Majaliwa alikua anapita, nusu saa kabla bara bara iliachwa wazi na traffic, magari yote yalipack pembeni. Majaliwa alipita kama mwewe.
 
Ni usonji wa kiwango cha icc mtanzania kuwa na fikra kama za huyu mtoa uzi.eti "atapanga rais awe nani" hiyo ndo akili ya hapo ufipa? Unafaham mchakato wa kumpata mgombea ndani ya ccm??
Yani asubuhi hii watu hawajapiga hata mswaki unawaamusha kwa ugori kama huu??
Mkuu jarbu kufikiria tena tafadhali😐
Kuna Vitetesi fulan japo 2025 ni mbali ila kwa uoga wa Rais Magufuli, endapo akikubali kuachia madaraka basi atauingilia Uchaguzi kuanzia mchakato wa Mgombea ndani ya Chama hadi Uchaguzi Mkuu kwa ujumla kuhakikisha anayebaki ni yule atakayefanya yafuatayo

1. Hataruhusu kujadiliwa kwa aliyofanya rais mstaafu

2. Hataibua hoja au hataruhusu hoja za kuhoji matumizi yasiyofuata taratibu za Manunuzi kama vile ununuzi wa Ndege, na ujenzi wa miradi mbali mbali Ambayo haikufuata utaratibu na hatuoni uwazi

3. Hataruhusu kuhoji haki za watu zilizopotea na haki za watu waliouwawa au kufichwa kabisa

4. Hataruhusu kuhojiwa Kwa wafanya biashara Walidhulumiwa na serikali na wengine kufungwa kwa kisingizio cha Uhujumu uchumi na utakatishaji pesa,

5. Hataruhusu kabisa uwazi wa namna yeyote

KATIKA WATU ANAOWAONA WATAIWEZA KAZI HIYO

1. Bwana Hussein Mwinyi wa Zanzibar, huyu atakuwa ni yule wa Ndiyo mzee wangu mstaafu pumzika usiguswe

2. Paul Makonda, kwa Muda huu anatuzuga kamsahau lakin kwa Mabalaa na Maajabu ya Tanzania ukashangaa 2026 anapigiwa mizinga

3. Kassim Majaliwa, Huyu naye yuko Obedient Sana kwa Magufuli

4. Hamis kigwangalla,


Si lazima jina liwe kwenye hayo ila atapitishwa mwenye sifa za hao

Tukumbushane July 2025

Mungu atuweke na yeye amuweke pia maana ya Mungu Mengi hapa kati kati

Amen

Britannica
 
Back
Top Bottom