Tusipotoshane, ajira ina nafuu na uhakika zaidi kuliko kujiajiri

Tuache kudanganyana alichosema ndugu kuhusu ajira kina ukweli ndani yake kwa asilimia kubwa sana ...kwa nchi maskini Kama tz kujiajiri risk kubwa Sana pia kutokana na circulation ya pesa ya Sasa kufanikiwa ni kwa extent ndogo Sana na hata ukifanikiwa itategemea vitu vingi Sana ..Kama kiwango Cha mtaji wako..maarifa na Aina ya biashara pamoja na bahati ...kumbuka Africa watu wenye vipato vya uhakika ni wachache Sana hivyo hii inaathiri purchasing power...hivyo hii inafanya mazingira ya kujiajiri kuwa magumu...tatizo la wabongo wanafiki na wazandiki Sana unakuta jitu linasema kujiajiri ni kuzuri wakati lenyewe limeajiriwa ..kwa zilizoendelea na zilizo na watu wengi walioajiriwa biashara ni rahisi lakini tusidanganyane kwanza biashara Africa hazina garantii hata uwekezaji ni mgumu Africa na ndio maana serikari inatoa tax holiday ya miaka mitatu for new investment kozi wanajua mazingira ya kupata faida ni magumu oneni matajiri wa kiarabu wanavyopigana vikumbo kununua timu za uingereza kozi wanajua ukiwekeza kupata faida ni rahisi lakini sio Africa mazingira ya biashara na kujiajiri ni magumu na hayana assurance tuacheni kudanganyana...strive mayisiwa tajiri wa zimbambwe aliwahi kusema serikari za kiafrica ziache kukimbia tatizo la ajira kwa kigezo Cha kujiajiri....inabidi ajira zitengenezwe kwa wingi ndio wengine wachache wajiajiri....pia Cha mwisho hata mindset za watu hawaamini kijana alijiajiri kutoboa unaonekana Kama unapoteza mda coz inajulikana mazingira ni magumu...Mimi mwenyewe nimemaliza chuo mwaka 2016 na nimejiajiri najua ugumu na changamoto zake ..
 
Mleta mada nitajie tajiri yeyote mkubwa nchini au duniani kote alietajirika kupitia mshahara

I could show ya how to juggle anything and make it double Weed, blow, real estate, liquor sto' wit' no trouble - Grand Hustle.
 
Acha kuongea yaani huku kwetu ambako mnapaita mwisho wa nchi kuna jamaa anauza vifaa vya ujenzi, kulingana na mimi ni fundi na tumezoeana sana huwa sometime naingia kwa duka lake naenda kumsaidia kuuza kama wateja wamembana aisee kwa hesabu ya haraka haraka huwa anakunja millioni 2 au 1.5 faida kwa kila siku. Harafu unasema kuajiriwa ni bora, haujui chochote mkuu
 
swala la kujiajiri au kuajiriwa ina tegemea na kichwa cha mtu kuna mwingine kuajiriwa ni utumwa na mwingine anaona ndio ame win maisha labda tujiulize swali hili ,majengo manzuri ,manzuri yaliyo mengi kwenye mkoa wako unaloishi sasa ni waajiriwa au walio jiajiri jibu atakalo toa ndio upande wenye mafanikio .
 
Namshukuru Mungu nimeshaachana na utumwa wa ajira. Nimewahi kufikia Hadi mshahara level ya mlion 2 na stahiki zingine ila nikaja kupiga chini na kupambana kivyangu mtaani.


Ninachojivunia Ni kutengeneza 100 au 200 kwa nguvu zangu .

Kwa mtu mvivu na asie risk taker ajira Ni kimbilio lake ila kwa aggressive Hustlers kitaa ndio kimbilio. Wadau mitaa Ina hela. Tafuta docho Zama. Umiza kicha. Hakuna shimo la hela utaambiwa kiurahisi.


I'm done
 
Kwa mtu mvivu na asie risk taker ajira Ni kimbilio lake
Lengo / Goal huwa ni kuingiza kipato: mtu aliejiajiri anaweza kufungua duka kila siku saa 12 na kufunga saa 3 usiku, akawa anapata kipato kilekile kama cha mwenzake anaefika kazini saa mbili kasoro na kutoka saa 10 na ana siku 150 kati ya 365 za kupumzika mwaka mzima.

Nimewahi kufikia Hadi mshahara level ya mlion 2 na stahiki zingine ila nikaja kupiga chini na kupambana kivyangu mtaani.
mkuu, nimepitia post zako za nyuma, ulipata chumba cha kulala ??

1637100178921.png
 
tuliza kichwa utajua kujiari na kuajiriwa kipi bora kuajiriwa ni utumwa hatari sana usiniambie
Utumwa upi?

Mtu kaajiriwa anapewa siku 28 kila mwaka kwenda likizo, anapewa siku 128 za likizo akiumwa na analipwa, anapewa wiki 2 akipata msiba na analipwa, anapewa siku 80 akijifungua na analipwa, huyo aliejiajiri vp?

Alieajiriwa anaweza kuingia kazini saa mbili na kutoka saa 10 kasoro,waliojiajiri wengi tunawaona wanaingia alfajiri na kutoka usiku, hapo vp??

Alieajiriwa anaweza akawa anaenda kazini jumatatu hadi ijumaa tu, siku za weekend anafanya shughuli nyingine, pia sikukuu za serikali na dini zipatazo siku 20 haendi, kwa wengi waliojiajiri bado wanaendaga hata kukiwa na sikukuu hizi na mbaya zaidi wengi hawanaga weekend na ikiwepo basi ni j2 tu, utumwa uko wap?

Motivational speakers wamewatia sumu kali mno aisee.....

Mtu una ajira yako huna haja ya kusota ili kupata faida yako ya kwanza ama kurudisha mtaji ama kuwaza hasara,,,,Unaingia kazini mshahara unalamba vizuri kabisa, unajiongeza unaingia kundi la pili.
 
ninakueleza haya kwasababu niliajiriwa na kuacha na sasa mm ni mtu huru. ilikua inanirazimu kuamuka saa kumi na moja nijiandae ili angalau saa moja niwe kazini kutokana na usumbufu wa foleni za dar ilikua kila siku kuanzia saa mbili mpaka saa moja nipo kazini kwani kulingana na kazi yangu wakati mwingine kazi haikuisha uibebe kuifanyia nyumbani ili siku inayofuata uwe umekamilisha nikajikuta niko busy siku saba zote kuwaza kazi ya mwajiri unaweza kuona upo huru barabarani ukaona upo bichi ila akiri yote inawaza jumatatu unaanzia wapi kazi ya boss na unaikamilishaje kiporo kiufupi sikuweza kua na mda hata wa kufikiri juu ya mpangilio wa pesa au nifanye nn hivo maisha yangu ikawa ni mshahara mshahara na mm nilijikuta baada ya miaka minne sijafanya investiment ya namna yoyote zaidi ya suti na shati jeupe kuonekana ninanawili kumbe kiumbo tu moyo ni sonona tupu. baas nikaamua kuacha hata bila maandaliz mazuri nikazama kitaa nimepigika kwa kipindi cha miez sita nikiwa nimebana sana yaan ninamanisha hata kula ilibid nihesabu tofauti na nilipokua nineajiriwa nilikua nikuamuka saa kumi nipo barabarani nikasema acha nipigike kwani nimependa mm kwasasa nipo kitaa mwaka wa pili sasa ila sina nia ya kujisifu nipo kwangu bunju A maweni nyumba imekamilika ninamke na mtoto ninabiashara ambapo mm nimelala vijana wanakuja kuchukua maelezo nikiwa kitandani ninaweza lala mpaka saa tatu nikaamuka nikaanza kupitia vimiradi vyangu wewe tulia utajua utamu wa kujiajiri. ninakubaliana na ww kwamba kuna mateso mwanzoni ila si kama ya kushikiwa akili na mtu yaani ufokewe uambiwe fanya hili kama mtoto mdogo mh siwez kabisa kurudi kuajiriwa
Utumwa upi?

Mtu kaajiriwa anapewa siku 28 kila mwaka kwenda likizo, anapewa siku 128 za likizo akiumwa na analipwa, anapewa wiki 2 akipata msiba ba analipwa, endapo ni mwanamkwa anapewa siku 80 akijifungua na analipwa, huyo aliejiajiri vp?

Alieajiriwa anaweza kuingia kazini saa mbili na kutoka saa 10 kasoro, aloejiajiri wengi tunawaona wanaingia alfajiri na kutoka usiku, hapo vp??

Alieajiriwa anaweza akawa anaenda kazini jumatatu hadi ijumaa tu, siku za weekend anafanya shughuli nyingine, pia sikukuu za serilali na dini zipatazo siku 20 haendi, kwa wengi waliojoajiri bado wanaendaga hata kukiwa na sikukuu hizi na mbaya zaidi wengi hawanaga weekend na ikiwepo basi ni j2 tu, utumwa uko wap?
 
Lengo / Goal huwa ni kuingiza kipato: mtu aliejiajiri anaweza kufungua duka kila siku saa 12 na kufunga saa 3 usiku, akawa anapata kipato kilekile kama cha mwenzake anaefika kazini saa mbili kasoro na kutoka saa 10 na ana siku 150 kati ya 365 za kupumzika mwaka mzima.


mkuu, nimepitia post zako za nyuma, ulipata chumba cha kulala ??

View attachment 2013507
Kumbe ww mtoa mada akili hauna, uwezi copy uzi wa mtu akiulizia vitu vingne kwa ajili ya uzi wako, what if alikua anamtafutia mdogo wake hiko chumba au even ni yeye? Ina mnyima nn kutoa maoni kwenye uzi wako.

Pathetic.
 
Kwanza kabisa naomba tuyaelewe haya makundi matatu

KUNDI LA KWANZA - ALIEJIAJIRI / SELF EMPLOYED
View attachment 2008017View attachment 2008020

Huyu biashara inamuhitaji ili iende, yeye ndie ngvu kazi kuu ya kuieiendesha biashara kwa bidii yake na hata akiajiri bado yeye inabidi ahusike kwa level ya juu sana ili biashara iende, Wengi wao inabidi aende dukani kila siku alfajiri mpaka usiku, kutembeza bidhaa mitaani (machinga), fundi cherehani, n.k kundi hili mara nyingi asipoenda ofisini hakuna pesa inaingia hapo, akiumwa hakuna malipo, n.k Kundi hili kusema kweli hakuna uhuru, mtu ukiwa kundi hili usije kujichanganya hata siku moja kujifananisha na watu wa kundi la pili, wenzetu wengi wa nchi zilizoendelea kwenye maarifa, mtu akiingia hili kundi anasota miaka hata mitano ili aingie kundi la pili, cha ajabu huku Tanzania ni kama vile watu wa hili kundi wamridhika kuwepo hili kundi ama hawanana mikakati ya kuingia kundi la pili, wengi nimewajua tangu nipo shule ya msingi bado wapo pale pale, nahisi ni kukosa maarifa kwa kudhani kwamba wapo kundi moja na kundi la pili.


KUNDI LA PILI - MMILIKI WA BIASHARA / BUSINESS OWNER
View attachment 2008018View attachment 2008019


Hawa sifa yao kuu ni kwamba wameajiri watu wengine wawasaidie kuzalisha pesa, hawafanyi kazi ili wapate pesa kama kundi la kwanza na la tatu,
pesa ndio inawafanyia kazi ..Yeye anaweza akanunua kiwanja akapageuza kuwa car wash, vijana wanakuja kuosha magari, ikifika jioni anakuja kuchukua mgao wake. Anaweza akawa ni Mo au Bakhresa ikifika asubuhi watu wanawahi kwenda kwenye viwanda vyao kufanya kazi ili kuwatengenezea pesa na wao kulipwa mishahara,

hata kwa upande wa wasanii, Diamond yupo kundi la pili, kaajiri mameneja, wasanii, n.k ana magari ya kufahari kama rolls royce toleo la mwaka huu, escallade toleo la mwaka jana, v8 kama ya wabunge, n.k , wasanii wengi wapo kundi la kwanza wanatembelea toyota za mwaka 2014 zilizotumika mno.


KUNDI LA TATU- ALIEAJIRIWA (EMPLOYED)

View attachment 2009001View attachment 2008023

hili kundi lina nafuu kuzidi kundi la kwanza hasa wakiwa wanapata kipato sawa
  • kazi anayoifanya haifanyi peke yake huwa wanasaidiana na wengine kwa hio mzigo haujamuelemea​
  • Mshahara wake atalipwa hata akiumwa ama kuwa na sababu maalum ya kutofika kazini​
  • anaweza kuingia kazini saa 2 na kutoka saa 10 / 11 jioni na kupata muda wa kukaa na watoto kama mzazi.​
  • bima ya afya​
  • mikopo kupatikana kirahisi​
  • anapumzika siku za weekend zipatazo 104 , sherehe za kidini na sherehe za kiserikali siku 20, kkizo ya mwezi siku 30, n.k​
  • Kipatoo ambacho ni mshahara atakipata kwa uhakika bila longo longo, pia kuna posho​
  • Anapata status kwenye jamii mfano baba flani ni mwanajeshi, injinia, muhasibu, dokta, hakimu, n.k. ukipata tatizo flani anaweza kutumia nafasi yake kukusaidia.​
  • anaweza kuingia kundi la pili bila kupitia taabu za kundi la kwanza maana tayari ana mshahara na anapata mkopo bila longo longo unaoweza kuwa mtaji na ukagharamia mfanyakazi wa kumtengenezea fedha​

TUREJEE KWENYE MAADA.....

Huwa nashangaa sana mtu wa kundi la kwanza anaeshinda dukani masaa zaidi ya 12, anapigwa na jua mchana akitembeza bidhaa, n.k na faida yenyewe haizidi hata elf 30 kwa siku, Sijui ni wapi anautoa ujasiri wa kumdharau mtu wa kundi la tatu kwa kauli kama "ajira ni utumwa" hapo ikumbukwe yeye na mwenzake wanaingiza kipato sawa lakini mwenzake anafanyia kazi zake ofisini kwenye kiyoyozi, umeme ukikatika generator inawashwa, anafana kazi mpaka saa 10 tu jioni, ana siku siku 150 kati ya 365 za kupumzika kila mwaka, akiumwa bado anapata analipwa, kuna posho za ziada, anaweza kufungua biashara na kuajiri wasimamizi, n.k,

Kauli nyingine ya kijinga ya kujifariji ni kuuliza swali "nitajie tajiri yeyote mkubwa nchini alietajirika kupitia mshahara?" Hapa mtu anauliza hili swali kwa maksudi kabisa ili kujifariji huku akijidanganya kwamba yupo kundi moja na kina bakhresa waliopo kundi la pili, anasahau kabisa kwamba watu wa kundi la pili ni Business owners (wamiliki wa biashara) wanaoajiri watu wawatafutie pesa, hata wakiuchapa usingizi mpaka saa nne pesa inaingia tu.

Kuponda ajira ni utumwa kwa mtu aliejiajiri ni sawa na "sizitaki mbichi hizi", nimeshushudia ajira zikitangazwa, hao waliojiajiri wanazishambulia sio mchezo, mtu anafunga duka lake kapata safari ya kwenda dar kufanya interview,

Kuna vijana wadogo wengi tu wameajiriwa, wanakunja mshahara zaidi ya milioni 2 kila mwezi na wamepiga hatua ya ziada kufungua biashara zao za kuajiri wenzao (kuwa business owners), kujenga wakiwa bado vijana wadogo, n.k Niambie vijana wangapi wa kundi la kwanza wanakuwa wamefika hizo level?

Jiulize kwanini hata wazazi wengi ambao wapo kundi la kwanza wanapigana kufa kupoma kuwapeleka watoto kusoma na kuwaambia wasome ili wapate ajira ?? kwanini wasiwaambie wasome ili wawe kama wao ??
watumwa mpo wengi katika nchi hii
 
Naona uyo jamaaa ajakosea kulingana namazo yake but akikua atajua pia anaye sema kujiajil unaweza kuangukia pua anasaau kunawangap wanafukuzwa kazi pia anayesema mshahara wa milion 3 nibora kuliko kijilipa lakitano ajajua lakitano inaweza kufika milion 5 kwa mwezi lakini milion 3 itafika milion 3.5kama boss ataamua
 
B
Watu wa humu ndani hujawazoea kwani 🤣🤣🤣🤣ndani ya ajira watu wanapata fursa kibao especially position za juu jiulize hao wakina mbowe si wafanya business wakubwa wanashika parefu ila wanataka ubunge na urais ili mambo yawe mazuri zaidi
oss tofautisha ajira siasa na biashara
 
Nimeshaajiriwa na kujiajiri!
Mara zote nikirudi kujiajiri, coz ajira nilitumia napangilia mambo yangu, kama source ya Ku boost mtaji wangu!

Namshukuru Mungu niko kujiajiri, nalima, nafuga, nakusanya mazao, Nina mambo mengi yanayozungusha pesa!

Sijawahi kujua kwanini masomo ya biashara, Commerce, booking, accounts, hayafundishwi kuanzia darasa la 5, sayansi inafundishwa tokea darasa la kwanza. Concept Tu za biashara!

Hili litasaidia mpaka magepu ya ajira, mtu anaajiriwa miaka 5-10 baadaye anajiajiri, wengine wanachukua nafasi yake wanaajiriwa, hivyo hivyo!
 
Fac
Nimeshaajiriwa na kujiajiri!
Mara zote nikirudi kujiajiri, coz ajira nilitumia napangilia mambo yangu, kama source ya Ku boost mtaji wangu!

Namshukuru Mungu niko kujiajiri, nalima, nafuga, nakusanya mazao, Nina mambo mengi yanayozungusha pesa!

Sijawahi kujua kwanini masomo ya biashara, Commerce, booking, accounts, hayafundishwi kuanzia darasa la 5, sayansi inafundishwa tokea darasa la kwanza. Concept Tu za biashara!

Hili litasaidia mpaka magepu ya ajira, mtu anaajiriwa miaka 5-10 baadaye anajiajiri, wengine wanachukua nafasi yake wanaajiriwa, hivyo hivyo!
t
 
Back
Top Bottom