sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Ikiwa alieajiriwa Serikalini na aliejiajiri wote wanaingiza kipato sawa kila mwezi
1. Aliejiajiri anaondoka kwake asubuhi kurudi hadi usiku, alieajiriwa Serikalini anaondoka asubuhi anamaliza kazi zake jioni na bado huko ofisini kuna muda anapata kufanya mambo yake.
2. Aliejiajiri anaweza asizijue weekend lakini alieajiriwa Serikalini anapumzika Jumamosi na Jumapili.
3. Aliajiajiri hana sikukuu za kiserikali, alieajiriwa Serikalini haendi kazini idi (hata kama ni mkristo), mwaka mpya, Mei mosi, sabasaba, siku ya Nyeyere, siku ya uhuru, mapinduzi, nanenane, idi, pasaka, n.k
4. Aliejiajiri akiumwa inabidi ajikaze aende tu lasivyo kipato kinaweza kutikisika, alieajiriwa Serikalini akiumwa anatoa notisi.
5. Aliejiajiri hana likizo, muajiriwa ana likizo siku 30 kila mwaka.
6. Aliejiajiri anaweza kufilisika endapo duka likiungua, akiumwa kwa muda mrefu, akiibiwa, n.k. alieajiriwa Serikalini nafasi yake na mshahara wake ni uhakika
7. Aliyeajiriwa Serikalini ni rahisi kukusanya mtaji, mkopo anapata kwa masharti nafuu sana na kwa haraka sambaamba na kudunduliza mshahara
8. Alieajiajiriwa na Serikali ana muda mwingi wa kuwa na familia yake kuzidi aliejiajiri. ikifika jioni, weekend, sikukuu za serikali, likizo, n.k. ana muda wa kutosha wa kuwa na familia yake
9. Alieajiriwa Serikalini anaweza kuwa ma biashara zake za kumuongezea kipato, hizi biashara zinaweza kumtunza baada ya kustaafu na watoto wake kuzirithi, Mifano ni kina Robert Kiyosaki mwenye kitabu cha Rich Dad Poor dad, Vunja Bei, Marehemu cpa Mengi, n.k. walianza kwa kukusanya mitaji wakiwa wameajiriwa.
Mwisho niseme Kujiajiri watu wanameki bingo lakini ni wachache, wengi wanaanguka na wengine wapo pale pale miaka nenda rudi. wachache wenye wenye roho ngumu, ubunifu, juhudi, kujibana, uvumilivu na connections ndio wanatoboa.
1. Aliejiajiri anaondoka kwake asubuhi kurudi hadi usiku, alieajiriwa Serikalini anaondoka asubuhi anamaliza kazi zake jioni na bado huko ofisini kuna muda anapata kufanya mambo yake.
2. Aliejiajiri anaweza asizijue weekend lakini alieajiriwa Serikalini anapumzika Jumamosi na Jumapili.
3. Aliajiajiri hana sikukuu za kiserikali, alieajiriwa Serikalini haendi kazini idi (hata kama ni mkristo), mwaka mpya, Mei mosi, sabasaba, siku ya Nyeyere, siku ya uhuru, mapinduzi, nanenane, idi, pasaka, n.k
4. Aliejiajiri akiumwa inabidi ajikaze aende tu lasivyo kipato kinaweza kutikisika, alieajiriwa Serikalini akiumwa anatoa notisi.
5. Aliejiajiri hana likizo, muajiriwa ana likizo siku 30 kila mwaka.
6. Aliejiajiri anaweza kufilisika endapo duka likiungua, akiumwa kwa muda mrefu, akiibiwa, n.k. alieajiriwa Serikalini nafasi yake na mshahara wake ni uhakika
7. Aliyeajiriwa Serikalini ni rahisi kukusanya mtaji, mkopo anapata kwa masharti nafuu sana na kwa haraka sambaamba na kudunduliza mshahara
8. Alieajiajiriwa na Serikali ana muda mwingi wa kuwa na familia yake kuzidi aliejiajiri. ikifika jioni, weekend, sikukuu za serikali, likizo, n.k. ana muda wa kutosha wa kuwa na familia yake
9. Alieajiriwa Serikalini anaweza kuwa ma biashara zake za kumuongezea kipato, hizi biashara zinaweza kumtunza baada ya kustaafu na watoto wake kuzirithi, Mifano ni kina Robert Kiyosaki mwenye kitabu cha Rich Dad Poor dad, Vunja Bei, Marehemu cpa Mengi, n.k. walianza kwa kukusanya mitaji wakiwa wameajiriwa.
Mwisho niseme Kujiajiri watu wanameki bingo lakini ni wachache, wengi wanaanguka na wengine wapo pale pale miaka nenda rudi. wachache wenye wenye roho ngumu, ubunifu, juhudi, kujibana, uvumilivu na connections ndio wanatoboa.